89) Sūrat Al-Fajr | Printed format | 89) سُورَة الفَجر |
| Wa Al-Fajri | 1. Naapa kwa alfajiri, | وَالْفَجْرِ |
| Wa Layālin `Ashrin | 2. Na kwa masiku kumi, | وَلَيَالٍ عَشْر ٍ |
| Wa Ash-Shaf`i Wa Al-Watri | 3. Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja, | وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ |
| Wa Al-Layli 'Idhā Yasri | 4. Na kwa usiku unapo pita, | وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ |
| Hal Fī Dhālika Qasamun Lidhī Ĥijrin | 5. Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili? | هَلْ فِي ذَلِكَ قَسَم ٌ لِذِي حِجْر ٍ |
| 'Alam Tara Kayfa Fa`ala Rabbuka Bi`ādin | 6. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di? | أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَاد ٍ |
| 'Irama Dhāti Al-`Imādi | 7. Wa Iram, wenye majumba marefu? | إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ |
| Allatī Lam Yukhlaq Mithluhā Fī Al-Bilādi | 8. Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi? | الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلاَدِ |
| Wa Thamūda Al-Ladhīna Jābū Aş-Şakhra Bil-Wādi | 9. Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni? | وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ |
| Wa Fir`awna Dhī Al-'Awtādi | 10. Na Firauni mwenye vigingi? | وَفِرْعَوْنَ ذِي الأَوْتَادِ |
| Al-Ladhīna Ţaghaw Fī Al-Bilādi | 11. Ambao walifanya jeuri katika nchi? | الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلاَدِ |
| Fa'aktharū Fīhā Al-Fasāda | 12. Wakakithirisha humo ufisadi? | فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ |
| Faşabba `Alayhim Rabbuka Sawţa `Adhābin | 13. Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu. | فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَاب ٍ |
| 'Inna Rabbaka Labiālmirşādi | 14. Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia. | إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ |
| Fa'ammā Al-'Insānu 'Idhā Mā Abtalāhu Rabbuhu Fa'akramahu Wa Na``amahu Fayaqūlu Rabbī 'Akramani | 15. Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu! | فَأَمَّا الإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلاَه ُُ رَبُّه ُُ فَأَكْرَمَه ُُ وَنَعَّمَه ُُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ |
| Wa 'Ammā 'Idhā Mā Abtalāhu Faqadara `Alayhi Rizqahu Fayaqūlu Rabbī 'Ahānani | 16. Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge! | وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلاَه ُُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَه ُُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ |
| Kallā Bal Lā Tukrimūna Al-Yatīma | 17. Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima, | كَلاَّ بَل لاَ تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ |
| Wa Lā Taĥāđđūna `Alá Ţa`āmi Al-Miskīni | 18. Wala hamhimizani kulisha masikini; | وَلاَ تَحَاضُّونَ عَلَى طَعَامِ الْمِسْكِينِ |
| Wa Ta'kulūna At-Turātha 'Aklāan Lammāan | 19. Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa, | وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلا ً لَمّا ً |
| Wa Tuĥibbūna Al-Māla Ĥubbāan Jammāan | 20. Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi. | وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبّا ً جَمّا ً |
| Kallā 'Idhā Dukkati Al-'Arđu Dakkāan Dakkāan | 21. Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande, | كَلاَّ إِذَا دُكَّتِ الأَرْضُ دَكّا ً دَكّا ً |
| Wa Jā'a Rabbuka Wa Al-Malaku Şaffāan Şaffāan | 22. Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu, | وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفّا ً صَفّا ً |
| Wa Jī'a Yawma'idhin Bijahannama Yawma'idhin Yatadhakkaru Al-'Insānu Wa 'Anná Lahu Adh-Dhikrá | 23. Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini? | وَجِيءَ يَوْمَئِذ ٍ بِجَهَنَّمَ يَوْمَئِذ ٍ يَتَذَكَّرُ الإِنْسَانُ وَأَنَّى لَهُ الذِّكْرَى |
| Yaqūlu Yā Laytanī Qaddamtu Liĥayātī | 24. Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu! | يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي |
| Fayawma'idhin Lā Yu`adhdhibu `Adhābahu 'Aĥadun | 25. Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake. | فَيَوْمَئِذ ٍ لاَ يُعَذِّبُ عَذَابَهُ~ُ أَحَد ٌ |
| Wa Lā Yūthiqu Wathāqahu 'Aĥadun | 26. Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake. | وَلاَ يُوثِقُ وَثَاقَهُ~ُ أَحَد ٌ |
| Yā 'Ayyatuhā An-Nafsu Al-Muţma'innahu | 27. Ewe nafsi iliyo tua! | يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ |
| Arji`ī 'Ilá Rabbiki Rāđiyatan Marđīyahan | 28. Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. | ارْجِعِي إِلَى رَبِّكِ رَاضِيَة ً مَرْضِيَّة ً |
| Fādkhulī Fī `Ibādī | 29. Basi ingia miongoni mwa waja wangu, | فَادْخُلِي فِي عِبَادِي |
| Wa Adkhulī Jannatī | 30. Na ingia katika Pepo yangu. * | وَادْخُلِي جَنَّتِي |