75) Sūrat Al-Qiyāmah | Printed format | 75) سُورَة الْقِيَامَه |
| Lā 'Uqsimu Biyawmi Al-Qiyāmahi | 1. Ninaapa kwa Siku ya Kiyama! | لاَ أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ |
| Wa Lā 'Uqsimu Bin-Nafsi Al-Lawwāmahi | 2. Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu! | وَلاَ أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ |
| 'Ayaĥsabu Al-'Insānu 'Allan Najma`a `Ižāmahu | 3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake? | أَيَحْسَبُ الإِنسَانُ أَلَّنْ نَجْمَعَ عِظَامَهُ |
| Balá Qādirīna `Alá 'An Nusawwiya Banānahu | 4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! | بَلَى قَادِرِينَ عَلَى أَنْ نُسَوِّيَ بَنَانَهُ |
| Bal Yurīdu Al-'Insānu Liyafjura 'Amāmahu | 5. Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake. | بَلْ يُرِيدُ الإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ |
| Yas'alu 'Ayyāna Yawmu Al-Qiyāmahi | 6. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? | يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ |
| Fa'idhā Bariqa Al-Başaru | 7. Basi jicho litapo dawaa, | فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ |
| Wa Khasafa Al-Qamaru | 8. Na mwezi utapo patwa, | وَخَسَفَ الْقَمَرُ |
| Wa Jumi`a Ash-Shamsu Wa Al-Qamaru | 9. Na likakusanywa jua na mwezi, | وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ |
| Yaqūlu Al-'Insānu Yawma'idhin 'Ayna Al-Mafarru | 10. Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio? | يَقُولُ الإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ |
| Kallā Lā Wazara | 11. La! Hapana pa kukimbilia! | كَلاَّ لاَ وَزَرَ |
| 'Ilá Rabbika Yawma'idhin Al-Mustaqarru | 12. Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu. | إِلَى رَبِّكَ يَوْمَئِذ ٍ الْمُسْتَقَرُّ |
| Yunabba'u Al-'Insānu Yawma'idhin Bimā Qaddama Wa 'Akhkhara | 13. Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha. | يُنَبَّأُ الإِنسَانُ يَوْمَئِذ ٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ |
| Bali Al-'Insānu `Alá Nafsihi Başīrahun | 14. Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake. | بَلِ الإِنسَانُ عَلَى نَفْسِه ِِ بَصِيرَة ٌ |
| Wa Law 'Alqá Ma`ādhīrahu | 15. Na ingawa atatoa chungu ya udhuru. | وَلَوْ أَلْقَى مَعَاذِيرَهُ |
| Lā Tuĥarrik Bihi Lisānaka Lita`jala Bihi | 16. Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka. | لاَ تُحَرِّكْ بِه ِِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ |
| 'Inna `Alaynā Jam`ahu Wa Qur'ānahu | 17. Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha. | إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَه ُُ وَقُرْآنَهُ |
| Fa'idhā Qara'nāhu Fa Attabi` Qur'ānahu | 18. Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake. | فَإِذَا قَرَأْنَاه ُُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ |
| Thumma 'Inna `Alaynā Bayānahu | 19. Kisha ni juu yetu kuubainisha. | ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ |
| Kallā Bal Tuĥibbūna Al-`Ājilaha | 20. Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani, | كَلاَّ بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ |
| Wa Tadharūna Al-'Ākhiraha | 21. Na mnaacha maisha ya Akhera. | وَتَذَرُونَ الآخِرَةَ |
| Wujūhun Yawma'idhin Nāđirahun | 22. Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara, | وُجُوه ٌ ٌ يَوْمَئِذ ٍ نَاضِرَة ٌ |
| 'Ilá Rabbihā Nāžirahun | 23. Zinamwangallia Mola wao Mlezi. | إِلَى رَبِّهَا نَاظِرَة ٌ |
| Wa Wujūhun Yawma'idhin Bāsirahun | 24. Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana. | وَوُجُوه ٌ ٌ يَوْمَئِذ ٍ بَاسِرَة ٌ |
| Tažunnu 'An Yuf`ala Bihā Fāqirahun | 25. Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo. | تَظُنُّ أَنْ يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَة ٌ |
| Kallā 'Idhā Balaghati At-Tarāqī | 26. La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo, | كَلاَّ إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِي |
| Wa Qīla Man Rāqin | 27. Na pakasemwa: Nani wa kumganga? | وَقِيلَ مَنْ رَاق ٍ |
| Wa Žanna 'Annahu Al-Firāqu | 28. Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki; | وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ |
| Wa At-Taffati As-Sāqu Bis-Sāqi | 29. Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi, | وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ |
| 'Ilá Rabbika Yawma'idhin Al-Masāqu | 30. Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi! | إِلَى رَبِّكَ يَوْمَئِذ ٍ الْمَسَاقُ |
| Falā Şaddaqa Wa Lā Şallá | 31. Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali. | فَلاَ صَدَّقَ وَلاَ صَلَّى |
| Wa Lakin Kadhdhaba Wa Tawallá | 32. Bali alikanusha, na akageuka. | وَلَكِنْ كَذَّبَ وَتَوَلَّى |
| Thumma Dhahaba 'Ilá 'Ahlihi Yatamaţţá | 33. Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao. | ثُمَّ ذَهَبَ إِلَى أَهْلِه ِِ يَتَمَطَّى |
| 'Awlá Laka Fa'awlá | 34. Ole wako, ole wako! | أَوْلَى لَكَ فَأَوْلَى |
| Thumma 'Awlá Laka Fa'awlá | 35. Kisha Ole wako, ole wako! | ثُمَّ أَوْلَى لَكَ فَأَوْلَى |
| 'Ayaĥsabu Al-'Insānu 'An Yutraka Sudáan | 36. Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure? | أَيَحْسَبُ الإِنسَانُ أَنْ يُتْرَكَ سُدى ً |
| 'Alam Yaku Nuţfatan Min Manīyin Yumná | 37. Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa? | أَلَمْ يَكُ نُطْفَة ً مِنْ مَنِيّ ٍ يُمْنَى |
| Thumma Kāna `Alaqatan Fakhalaqa Fasawwá | 38. Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo. | ثُمَّ كَانَ عَلَقَة ً فَخَلَقَ فَسَوَّى |
| Faja`ala Minhu Az-Zawjayni Adh-Dhakara Wa Al-'Unthá | 39. Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke. | فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالأُنثَى |
| 'Alaysa Dhālika Biqādirin `Alá 'An Yuĥyiya Al-Mawtá | 40. Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu? * | أَلَيْسَ ذَلِكَ بِقَادِرٍ عَلَى أَنْ يُحْيِيَ الْمَوْتَى |