70) Sūrat Al-Ma`ārij | Printed format | 70) سُورَة المَعَارِج |
| Sa'ala Sā'ilun Bi`adhābin Wāqi`in | 1. Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea, | سَأَلَ سَائِل ٌ بِعَذَاب ٍ وَاقِع ٍ |
| Lilkāfiryna Laysa Lahu Dāfi`un | 2. Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia - | لِلْكَافِرينَ لَيْسَ لَه ُُ دَافِع ٌ |
| Mina Allāhi Dhī Al-Ma`āriji | 3. Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja. | مِنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِ |
| Ta`ruju Al-Malā'ikatu Wa Ar-Rūĥu 'Ilayhi Fī Yawmin Kāna Miqdāruhu Khamsīna 'Alfa Sanahin | 4. Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu! | تَعْرُجُ الْمَلاَئِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْم ٍ كَانَ مِقْدَارُه ُُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَة ٍ |
| Fāşbir Şabrāan Jamīlāan | 5. Basi subiri kwa subira njema. | فَاصْبِرْ صَبْرا ً جَمِيلا ً |
| 'Innahum Yarawnahu Ba`īdāan | 6. Hakika wao wanaiona iko mbali, | إِنَّهُمْ يَرَوْنَه ُُ بَعِيدا ً |
| Wa Narāhu Qarībāan | 7. Na Sisi tunaiona iko karibu. | وَنَرَاه ُُ قَرِيبا ً |
| Yawma Takūnu As-Samā'u Kālmuhli | 8. Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa. | يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ |
| Wa Takūnu Al-Jibālu Kāl`ihni | 9. Na milima itakuwa kama sufi. | وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ |
| Wa Lā Yas'alu Ĥamīmun Ĥamīmāan | 10. Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake. | وَلاَ يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيما ً |
| Yubaşşarūnahum Yawaddu Al-Mujrimu Law Yaftadī Min `Adhābi Yawmi'idhin Bibanīhi | 11. Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe, | يُبَصَّرُونَهُمْ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذ ٍ بِبَنِيهِ |
| Wa Şāĥibatihi Wa 'Akhīhi | 12. Na mkewe, na nduguye, | وَصَاحِبَتِه ِِ وَأَخِيهِ |
| Wa Faşīlatihi Allatī Tu'uwyhi | 13. Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu, | وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْويهِ |
| Wa Man Fī Al-'Arđi Jamī`āan Thumma Yunjīhi | 14. Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye. | وَمَنْ فِي الأَرْضِ جَمِيعا ً ثُمَّ يُنجِيهِ |
| Kallā 'Innahā Lažá | 15. La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa, | كَلاَّ إِنَّهَا لَظَى |
| Nazzā`atan Lilshshawá | 16. Unao babua ngozi ya kichwa! | نَزَّاعَة ً لِلشَّوَى |
| Tad`ū Man 'Adbara Wa Tawallá | 17. Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka. | تَدْعُوا مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّى |
| Wa Jama`a Fa'aw`á | 18. Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi. | وَجَمَعَ فَأَوْعَى |
| 'Inna Al-'Insāna Khuliqa Halū`āan | 19. Hakika mtu ameumbwa na papara. | إِنَّ الإِنسَانَ خُلِقَ هَلُوعا ً |
| 'Idhā Massahu Ash-Sharru Jazū`āan | 20. Inapo mgusa shari hupapatika. | إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعا ً |
| Wa 'Idhā Massahu Al-Khayru Manū`āan | 21. Na inapo mgusa kheri huizuilia. | وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعا ً |
| 'Illā Al-Muşallīna | 22. Isipo kuwa wanao sali, | إِلاَّ الْمُصَلِّينَ |
| Al-Ladhīna Hum `Alá Şalātihim Dā'imūna | 23. Ambao wanadumisha Sala zao, | الَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلاَتِهِمْ دَائِمُونَ |
| Wa Al-Ladhīna Fī 'Amwālihim Ĥaqqun Ma`lūmun | 24. Na ambao katika mali yao iko haki maalumu | وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقّ ٌ مَعْلُوم ٌ |
| Lilssā'ili Wa Al-Maĥrūmi | 25. Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba; | لِلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ |
| Wa Al-Ladhīna Yuşaddiqūna Biyawmi Ad-Dīni | 26. Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo, | وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ |
| Wa Al-Ladhīna Hum Min `Adhābi Rabbihim Mushfiqūna | 27. Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi. | وَالَّذِينَ هُمْ مِنْ عَذَابِ رَبِّهِمْ مُشْفِقُونَ |
| 'Inna `Adhāba Rabbihim Ghayru Ma'mūnin | 28. Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo. | إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُون ٍ |
| Wa Al-Ladhīna Hum Lifurūjihim Ĥāfižūna | 29. Na ambao wanahifadhi tupu zao. | وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ |
| 'Illā `Alá 'Azwājihim 'Aw Mā Malakat 'Aymānuhum Fa'innahum Ghayru Malūmīna | 30. Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi - | إِلاَّ عَلَى أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ |
| Famani Abtaghá Warā'a Dhālika Fa'ūlā'ika Humu Al-`Ādūna | 31. Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka. | فَمَنِ ابْتَغَى وَرَاءَ ذَلِكَ فَأُوْلَائِكَ هُمُ الْعَادُونَ |
| Wa Al-Ladhīna Hum Li'mānātihim Wa `Ahdihim Rā`ūna | 32. Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao, | وَالَّذِينَ هُمْ لِأمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ |
| Wa Al-Ladhīna Hum Bishahādātihim Qā'imūna | 33. Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao, | وَالَّذِينَ هُمْ بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ |
| Wa Al-Ladhīna Hum `Alá Şalātihim Yuĥāfižūna | 34. Na ambao wanazihifadhi Sala zao. | وَالَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلاَتِهِمْ يُحَافِظُونَ |
| 'Ūlā'ika Fī Jannātin Mukramūna | 35. Hao ndio watakao hishimiwa Peponi. | أُوْلَائِكَ فِي جَنَّات ٍ مُكْرَمُونَ |
| Famāli Al-Ladhīna Kafarū Qibalaka Muhţi`īna | 36. Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu? | فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ |
| `Ani Al-Yamīni Wa `Ani Ash-Shimāli `Izīna | 37. Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto! | عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ |
| 'Ayaţma`u Kullu Amri'in Minhum 'An Yudkhala Jannata Na`īmin | 38. Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema? | أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئ ٍ مِنْهُمْ أَنْ يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيم ٍ |
| Kallā 'Innā Khalaqnāhum Mimmā Ya`lamūna | 39. La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua. | كَلاَّ إِنَّا خَلَقْنَاهُمْ مِمَّا يَعْلَمُونَ |
| Falā 'Uqsimu Birabbi Al-Mashāriqi Wa Al-Maghāribi 'Innā Laqādirūna | 40. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza | فَلاَ أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَ |
| `Alá 'An Nubaddila Khayrāan Minhum Wa Mā Naĥnu Bimasbūqīna | 41. Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi. | عَلَى أَنْ نُبَدِّلَ خَيْرا ً مِنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ |
| Fadharhum Yakhūđū Wa Yal`abū Ĥattá Yulāqū Yawmahumu Al-Ladhī Yū`adūna | 42. Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa, | فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّى يُلاَقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ |
| Yawma Yakhrujūna Mina Al-'Ajdāthi Sirā`āan Ka'annahum 'Ilá Nuşubin Yūfiđūna | 43. Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo, | يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الأَجْدَاثِ سِرَاعا ً كَأَنَّهُمْ إِلَى نُصُب ٍ يُوفِضُونَ |
| Khāshi`atan 'Abşāruhum Tarhaquhum Dhillatun Dhālika Al-Yawmu Al-Ladhī Kānū Yū`adūna | 44. Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa. * | خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّة ٌ ذَلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ |