69) Sūrat Al-Ĥāqqah | Printed format | 69) سُورَة الحَاقَّه |
| Al-Ĥāqqahu | 1. Tukio la haki. | الْحَاقَّةُ |
| Mā Al-Ĥāqqahu | 2. Nini hilo Tukio la haki? | مَا الْحَاقَّةُ |
| Wa Mā 'Adrāka Mā Al-Ĥāqqahu | 3. Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki? | وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحَاقَّةُ |
| Kadhdhabat Thamūdu Wa `Ādun Bil-Qāri`ahi | 4. Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha. | كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَاد ٌ بِالْقَارِعَةِ |
| Fa'ammā Thamūdu Fa'uhlikū Biţ-Ţāghiyahi | 5. Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno. | فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا بِالطَّاغِيَةِ |
| Wa 'Ammā `Ādun Fa'uhlikū Birīĥin Şarşarin `Ātiyahin | 6. Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika. | وَأَمَّا عَاد ٌ فَأُهْلِكُوا بِرِيح ٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَة ٍ |
| Sakhkharahā `Alayhim Sab`a Layālin Wa Thamāniyata 'Ayyāmin Ĥusūmāan Fatará Al-Qawma Fīhā Şar`á Ka'annahum 'A`jāzu Nakhlin Khāwiyahin | 7. Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani. | سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَال ٍ وَثَمَانِيَةَ أَيَّامٍ حُسُوما ً فَتَرَى الْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَى كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَة ٍ |
| Fahal Tará Lahum Min Bāqiyahin | 8. Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki? | فَهَلْ تَرَى لَهُمْ مِنْ بَاقِيَة ٍ |
| Wa Jā'a Fir`awnu Wa Man Qablahu Wa Al-Mu'utafikātu Bil-Khāţi'ahi | 9. Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia. | وَجَاءَ فِرْعَوْنُ وَمَنْ قَبْلَه ُُ وَالْمُؤْتَفِكَاتُ بِالْخَاطِئَةِ |
| Fa`aşaw Rasūla Rabbihim Fa'akhadhahum 'Akhdhatan Rābiyahan | 10. Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu. | فَعَصَوْا رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَة ً رَابِيَة ً |
| 'Innā Lammā Ţaghá Al-Mā'u Ĥamalnākum Fī Al-Jāriyahi | 11. Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina, | إِنَّا لَمَّا طَغَى الْمَاءُ حَمَلْنَاكُمْ فِي الْجَارِيَةِ |
| Linaj`alahā Lakum Tadhkiratan Wa Ta`iyahā 'Udhunun Wā`iyahun | 12. Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi. | لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَة ً وَتَعِيَهَا أُذُن ٌ وَاعِيَة ٌ |
| Fa'idhā Nufikha Fī Aş-Şūri Nafkhatun Wāĥidahun | 13. Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu, | فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ نَفْخَة ٌ وَاحِدَة ٌ |
| Wa Ĥumilati Al-'Arđu Wa Al-Jibālu Fadukkatā Dakkatan Wāĥidahan | 14. Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja, | وَحُمِلَتِ الأَرْضُ وَالْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّة ً وَاحِدَة ً |
| Fayawma'idhin Waqa`ati Al-Wāqi`ahu | 15. Siku hiyo ndio Tukio litatukia. | فَيَوْمَئِذ ٍ وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ |
| Wa Anshaqqati As-Samā'u Fahiya Yawma'idhin Wa Ahiyahun | 16. Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa. | وَانشَقَّتِ السَّمَاءُ فَهِيَ يَوْمَئِذ ٍ وَاهِيَة ٌ |
| Wa Al-Malaku `Alá 'Arjā'ihā Wa Yaĥmilu `Arsha Rabbika Fawqahum Yawma'idhin Thamāniyahun | 17. Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi. | وَالْمَلَكُ عَلَى أَرْجَائِهَا وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذ ٍ ثَمَانِيَة ٌ |
| Yawma'idhin Tu`rađūna Lā Takhfá Minkum Khāfiyahun | 18. Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu. | يَوْمَئِذ ٍ تُعْرَضُونَ لاَ تَخْفَى مِنْكُمْ خَافِيَة ٌ |
| Fa'ammā Man 'Ūtiya Kitābahu Biyamīnihi Fayaqūlu Hā'uum Aqra'ū Kitābī | 19. Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu! | فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَه ُُ بِيَمِينِه ِِ فَيَقُولُ هَاؤُمْ اقْرَءُوا كِتَابِي |
| 'Innī Žanantu 'Annī Mulāqin Ĥisābiyah | 20. Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu. | إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلاَقٍ حِسَابِيَه |
| Fahuwa Fī `Īshatin Rāđiyahin | 21. Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza, | فَهُوَ فِي عِيشَة ٍ رَاضِيَة ٍ |
| Fī Jannatin `Āliyahin | 22. Katika Bustani ya juu, | فِي جَنَّةٍ عَالِيَة ٍ |
| Quţūfuhā Dāniyahun | 23. Matunda yake yakaribu. | قُطُوفُهَا دَانِيَة ٌ |
| Kulū Wa Ashrabū Hanī'āan Bimā 'Aslaftum Fī Al-'Ayyāmi Al-Khāliyahi | 24. Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita. | كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئا ً بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الأَيَّامِ الْخَالِيَةِ |
| Wa 'Ammā Man 'Ūtiya Kitābahu Bishimālihi Fayaqūlu Yā Laytanī Lam 'Ūta Kitābīh | 25. Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu! | وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَه ُُ بِشِمَالِه ِِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيهْ |
| Wa Lam 'Adri Mā Ĥisābīh | 26. Wala nisingeli jua nini hisabu yangu. | وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيهْ |
| Yā Laytahā Kānati Al-Qāđiyaha | 27. Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa. | يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ |
| Mā 'Aghná `Annī Mālīh | 28. Mali yangu hayakunifaa kitu. | مَا أَغْنَى عَنِّي مَالِيهْ |
| Halaka `Annī Sulţānīh | 29. Madaraka yangu yamenipotea. | هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيهْ |
| Khudhūhu Faghullūhu | 30. (Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu! | خُذُوه ُُ فَغُلُّوهُ |
| Thumma Al-Jaĥīma Şallūhu | 31. Kisha mtupeni Motoni! | ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ |
| Thumma Fī Silsilatin Dhar`uhā Sab`ūna Dhirā`āan Fāslukūhu | 32. Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini! | ثُمَّ فِي سِلْسِلَة ٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعا ً فَاسْلُكُوهُ |
| 'Innahu Kāna Lā Yu'uminu Billāhi Al-`Ažīmi | 33. Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu, | إِنَّه ُُ كَانَ لاَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ |
| Wa Lā Yaĥuđđu `Alá Ţa`āmi Al-Miskīni | 34. Wala hahimizi kulisha masikini. | وَلاَ يَحُضُّ عَلَى طَعَامِ الْمِسْكِينِ |
| Falaysa Lahu Al-Yawma Hāhunā Ĥamīmun | 35. Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu, | فَلَيْسَ لَهُ الْيَوْمَ هَاهُنَا حَمِيم ٌ |
| Wa Lā Ţa`āmun 'Illā Min Ghislīnin | 36. Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni. | وَلاَ طَعَام ٌ إِلاَّ مِنْ غِسْلِين ٍ |
| Lā Ya'kuluhu 'Illā Al-Khāţi'ūna | 37. Chakula hicho hawakili ila wakosefu. | لاَ يَأْكُلُهُ~ُ إِلاَّ الْخَاطِئُونَ |
| Falā 'Uqsimu Bimā Tubşirūna | 38. Basi naapa kwa mnavyo viona, | فَلاَ أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ |
| Wa Mā Lā Tubşirūna | 39. Na msivyo viona, | وَمَا لاَ تُبْصِرُونَ |
| 'Innahu Laqawlu Rasūlin Karīmin | 40. Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima. | إِنَّه ُُ لَقَوْلُ رَسُول ٍ كَرِيم ٍ |
| Wa Mā Huwa Biqawli Shā`irin Qalīlāan Mā Tu'uminūna | 41. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini. | وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِر ٍ قَلِيلا ً مَا تُؤْمِنُونَ |
| Wa Lā Biqawli Kāhinin Qalīlāan Mā Tadhakkarūna | 42. Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka. | وَلاَ بِقَوْلِ كَاهِن ٍ قَلِيلا ً مَا تَذَكَّرُونَ |
| Tanzīlun Min Rabbi Al-`Ālamīna | 43. Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. | تَنزِيل ٌ مِنْ رَبِّ الْعَالَمِينَ |
| Wa Law Taqawwala `Alaynā Ba`đa Al-'Aqāwīli | 44. Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu, | وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ الأَقَاوِيلِ |
| La'akhadhnā Minhu Bil-Yamīni | 45. Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia, | لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِالْيَمِينِ |
| Thumma Laqaţa`nā Minhu Al-Watīna | 46. Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo! | ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ الْوَتِينَ |
| Famā Minkum Min 'Aĥadin `Anhu Ĥājizīna | 47. Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia. | فَمَا مِنْكُمْ مِنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَاجِزِينَ |
| Wa 'Innahu Latadhkiratun Lilmuttaqīna | 48. Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu. | وَإِنَّه ُُ لَتَذْكِرَة ٌ لِلْمُتَّقِينَ |
| Wa 'Innā Lana`lamu 'Anna Minkum Mukadhdhibīna | 49. Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha. | وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنْكُمْ مُكَذِّبِينَ |
| Wa 'Innahu Laĥasratun `Alá Al-Kāfirīna | 50. Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa. | وَإِنَّه ُُ لَحَسْرَةٌ عَلَى الْكَافِرِينَ |
| Wa 'Innahu Laĥaqqu Al-Yaqīni | 51. Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini. | وَإِنَّه ُُ لَحَقُّ الْيَقِينِ |
| Fasabbiĥ Biāsmi Rabbika Al-`Ažīmi | 52. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu. * | فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ |