56) Sūrat Al-Wāqi`ah | Printed format | 56) سُورَة الوَاقِعَه |
| 'Idhā Waqa`ati Al-Wāqi`ahu | 1. Litakapo tukia hilo Tukio | إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ |
| Laysa Liwaq`atihā Kādhibahun | 2. Hapana cha kukanusha kutukia kwake. | لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَة ٌ |
| Khāfiđatun Rāfi`ahun | 3. Literemshalo linyanyualo, | خَافِضَة ٌ رَافِعَة ٌ |
| 'Idhā Rujjati Al-'Arđu Rajjāan | 4. Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso, | إِذَا رُجَّتِ الأَرْضُ رَجّا ً |
| Wa Bussati Al-Jibālu Bassāan | 5. Na milima itapo sagwasagwa, | وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسّا ً |
| Fakānat Habā'an Munbaththāan | 6. Iwe mavumbi yanayo peperushwa, | فَكَانَتْ هَبَاء ً مُنْبَثّا ً |
| Wa Kuntum 'Azwājāan Thalāthahan | 7. Na nyinyi mtakuwa namna tatu:- | وَكُنتُمْ أَزْوَاجا ً ثَلاَثَة ً |
| Fa'aşĥābu Al-Maymanati Mā 'Aşĥābu Al-Maymanahi | 8. Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani? | فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ |
| Wa 'Aşĥābu Al-Mash'amati Mā 'Aşĥābu Al-Mash'amahi | 9. Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni? | وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ |
| Wa As-Sābiqūna As-Sābiqūna | 10. Na wa mbele watakuwa mbele. | وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ |
| 'Ūlā'ika Al-Muqarrabūna | 11. Hao ndio watakao karibishwa | أُوْلَائِكَ الْمُقَرَّبُونَ |
| Fī Jannāti An-Na`īmi | 12. Katika Bustani zenye neema. | فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ |
| Thullatun Mina Al-'Awwalīna | 13. Fungu kubwa katika wa mwanzo, | ثُلَّة ٌ مِنَ الأَوَّلِينَ |
| Wa Qalīlun Mina Al-'Ākhirīna | 14. Na wachache katika wa mwisho. | وَقَلِيل ٌ مِنَ الآخِرِينَ |
| `Alá Sururin Mawđūnahin | 15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa. | عَلَى سُرُر ٍ مَوْضُونَة ٍ |
| Muttaki'īna `Alayhā Mutaqābilīna | 16. Wakiviegemea wakielekeana. | مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ |
| Yaţūfu `Alayhim Wildānun Mukhalladūna | 17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele, | يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَان ٌ مُخَلَّدُونَ |
| Bi'akwābin Wa 'Abārīqa Wa Ka'sin Min Ma`īnin | 18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. | بِأَكْوَاب ٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْس ٍ مِنْ مَعِين ٍ |
| Lā Yuşadda`ūna `Anhā Wa Lā Yunzifūna | 19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. | لاَ يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلاَ يُنزِفُونَ |
| Wa Fākihatin Mimmā Yatakhayyarūna | 20. Na matunda wayapendayo, | وَفَاكِهَة ٍ مِمَّا يَتَخَيَّرُونَ |
| Wa Laĥmi Ţayrin Mimmā Yashtahūna | 21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani. | وَلَحْمِ طَيْر ٍ مِمَّا يَشْتَهُونَ |
| Wa Ĥūrun `Īnun | 22. Na Mahurulaini, | وَحُورٌ عِين ٌ |
| Ka'amthāli Al-Lu'ulu'ui Al-Maknūni | 23. Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa. | كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ |
| Jazā'an Bimā Kānū Ya`malūna | 24. Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda. | جَزَاء ً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ |
| Lā Yasma`ūna Fīhā Laghwan Wa Lā Ta'thīmāan | 25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi, | لاَ يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوا ً وَلاَ تَأْثِيما ً |
| 'Illā Qīlāan Salāmāan Salāmāan | 26. Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama. | إِلاَّ قِيلا ً سَلاَما ً سَلاَما ً |
| Wa 'Aşĥābu Al-Yamīni Mā 'Aşĥābu Al-Yamīni | 27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani? | وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ |
| Fī Sidrin Makhđūdin | 28. Katika mikunazi isiyo na miba, | فِي سِدْر ٍ مَخْضُود ٍ |
| Wa Ţalĥin Manđūdin | 29. Na migomba iliyo pangiliwa, | وَطَلْح ٍ مَنْضُود ٍ |
| Wa Žillin Mamdūdin | 30. Na kivuli kilicho tanda, | وَظِلّ ٍ مَمْدُود ٍ |
| Wa Mā'in Maskūbin | 31. Na maji yanayo miminika, | وَمَاء ٍ مَسْكُوب ٍ |
| Wa Fākihatin Kathīrahin | 32. Na matunda mengi, | وَفَاكِهَة ٍ كَثِيرَة ٍ |
| Lā Maqţū`atin Wa Lā Mamnū`ahin | 33. Hayatindikii wala hayakatazwi, | لاَ مَقْطُوعَة ٍ وَلاَ مَمْنُوعَة ٍ |
| Wa Furushin Marfū`ahin | 34. Na matandiko yaliyo nyanyuliwa. | وَفُرُش ٍ مَرْفُوعَة ٍ |
| 'Innā 'Ansha'nāhunna 'Inshā'an | 35. Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya, | إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاء ً |
| Faja`alnāhunna 'Abkārāan | 36. Na tutawafanya vijana, | فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارا ً |
| `Urubāan 'Atrābāan | 37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja. | عُرُباً أَتْرَابا ً |
| Li'aşĥābi Al-Yamīni | 38. Kwa ajili ya watu wa kuliani. | لِأَصْحَابِ الْيَمِينِ |
| Thullatun Mina Al-'Awwalīna | 39. Fungu kubwa katika wa mwanzo, | ثُلَّة ٌ مِنَ الأَوَّلِينَ |
| Wa Thullatun Mina Al-'Ākhirīna | 40. Na fungu kubwa katika wa mwisho. | وَثُلَّة ٌ مِنَ الآخِرِينَ |
| Wa 'Aşĥābu Ash-Shimāli Mā 'Aşĥābu Ash-Shimāli | 41. Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni? | وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ |
| Fī Samūmin Wa Ĥamīmin | 42. Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka, | فِي سَمُوم ٍ وَحَمِيم ٍ |
| Wa Žillin Min Yaĥmūmin | 43. Na kivuli cha moshi mweusi, | وَظِلّ ٍ مِنْ يَحْمُوم ٍ |
| Lā Bāridin Wa Lā Karīmin | 44. Si cha kuburudisha wala kustarehesha. | لاَ بَارِد ٍ وَلاَ كَرِيم ٍ |
| 'Innahum Kānū Qabla Dhālika Mutrafīna | 45. Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa. | إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُتْرَفِينَ |
| Wa Kānū Yuşirrūna `Alá Al-Ĥinthi Al-`Ažīmi | 46. Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa, | وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ |
| Wa Kānū Yaqūlūna 'A'idhā Mitnā Wa Kunnā Turābāan Wa `Ižāmāan 'A'innā Lamab`ūthūna | 47. Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa? | وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابا ً وَعِظَاماً أَئِنَّا لَمَبْعُوثُونَ |
| 'Awa 'Ābā'uunā Al-'Awwalūna | 48. Au baba zetu wa zamani? | أَوَ آبَاؤُنَا الأَوَّلُونَ |
| Qul 'Inna Al-'Awwalīna Wa Al-'Ākhirīna | 49. Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho | قُلْ إِنَّ الأَوَّلِينَ وَالآخِرِينَ |
| Lamajmū`ūna 'Ilá Mīqāti Yawmin Ma`lūmin | 50. Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu. | لَمَجْمُوعُونَ إِلَى مِيقَاتِ يَوْم ٍ مَعْلُوم ٍ |
| Thumma 'Innakum 'Ayyuhā Ađ-Đāllūna Al-Mukadhdhibūna | 51. Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha, | ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ |
| La'ākilūna Min Shajarin Min Zaqqūmin | 52. Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu. | لَآكِلُونَ مِنْ شَجَر ٍ مِنْ زَقُّوم ٍ |
| Famāli'ūna Minhā Al-Buţūna | 53. Na kwa mti huo mtajaza matumbo. | فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ |
| Fashāribūna `Alayhi Mina Al-Ĥamīmi | 54. Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka. | فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ |
| Fashāribūna Shurba Al-Hīmi | 55. Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu. | فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ |
| Hādhā Nuzuluhum Yawma Ad-Dīni | 56. Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo. | هَذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ |
| Naĥnu Khalaqnākum Falawlā Tuşaddiqūna | 57. Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki? | نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلاَ تُصَدِّقُونَ |
| 'Afara'aytum Mā Tumnūna | 58. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza? | أَفَرَأَيْتُمْ مَا تُمْنُونَ |
| 'A'antum Takhluqūnahu 'Am Naĥnu Al-Khāliqūna | 59. Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji? | أَأَنْتُمْ تَخْلُقُونَهُ~ُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ |
| Naĥnu Qaddarnā Baynakumu Al-Mawta Wa Mā Naĥnu Bimasbūqīna | 60. Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi | نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ |
| `Alá 'An Nubaddila 'Amthālakum Wa Nunshi'akum Fī Mā Lā Ta`lamūna | 61. Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua. | عَلَى أَنْ نُبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنْشِئَكُمْ فِي مَا لاَ تَعْلَمُونَ |
| Wa Laqad `Alimtumu An-Nash'ata Al-'Ūlá Falawlā Tadhkkarūna | 62. Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki? | وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الأُولَى فَلَوْلاَ تَذكَّرُونَ |
| 'Afara'aytum Mā Taĥruthūna | 63. Je! Mnaona makulima mnayo yapanda? | أَفَرَأَيْتُمْ مَا تَحْرُثُونَ |
| 'A'antum Tazra`ūnahu 'Am Naĥnu Az-Zāri`ūna | 64. Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha? | أَأَنْتُمْ تَزْرَعُونَهُ~ُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ |
| Law Nashā'u Laja`alnāhu Ĥuţāmāan Fažalaltum Tafakkahūna | 65. Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu, | لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاه ُُ حُطَاما ً فَظَلَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ |
| 'Innā Lamughramūna | 66. Mkisema: Hakika sisi tumegharimika; | إِنَّا لَمُغْرَمُونَ |
| Bal Naĥnu Maĥrūmūna | 67. Bali sisi tumenyimwa. | بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ |
| 'Afara'aytumu Al-Mā'a Al-Ladhī Tashrabūna | 68. Je! Mnayaona maji mnayo yanywa? | أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ |
| 'A'antum 'Anzaltumūhu Mina Al-Muzni 'Am Naĥnu Al-Munzilūna | 69. Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha? | أَأَنْتُمْ أَنزَلْتُمُوه ُُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ |
| Law Nashā'u Ja`alnāhu 'Ujājāan Falawlā Tashkurūna | 70. Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru? | لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ~ُ أُجَاجا ً فَلَوْلاَ تَشْكُرُونَ |
| 'Afara'aytumu An-Nāra Allatī Tūrūna | 71. Je! Mnauona moto mnao uwasha? | أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ |
| 'A'antum 'Ansha'tum Shajaratahā 'Am Naĥnu Al-Munshi'ūna | 72. Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji? | أَأَنْتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ |
| Naĥnu Ja`alnāhā Tadhkiratan Wa Matā`āan Lilmuqwīna | 73. Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani. | نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَة ً وَمَتَاعا ً لِلْمُقْوِينَ |
| Fasabbiĥ Biāsmi Rabbika Al-`Ažīmi | 74. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu. | فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ |
| Falā 'Uqsimu Bimawāqi`i An-Nujūmi | 75. Basi naapa kwa maanguko ya nyota, | فَلاَ أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ |
| Wa 'Innahu Laqasamun Law Ta`lamūna `Ažīmun | 76. Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua! | وَإِنَّه ُُ لَقَسَم ٌ لَوْ تَعْلَمُونَ عَظِيم ٌ |
| 'Innahu Laqur'ānun Karīmun | 77. Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, | إِنَّه ُُ لَقُرْآن ٌ كَرِيم ٌ |
| Fī Kitābin Maknūnin | 78. Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. | فِي كِتَاب ٍ مَكْنُون ٍ |
| Lā Yamassuhu 'Illā Al-Muţahharūna | 79. Hapana akigusaye ila walio takaswa. | لاَ يَمَسُّهُ~ُ إِلاَّ الْمُطَهَّرُونَ |
| Tanzīlun Min Rabbi Al-`Ālamīna | 80. Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. | تَنزِيل ٌ مِنْ رَبِّ الْعَالَمِينَ |
| 'Afabihadhā Al-Ĥadīthi 'Antum Mud/hinūna | 81. Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza? | أَفَبِهَذَا الْحَدِيثِ أَنْتُمْ مُدْهِنُونَ |
| Wa Taj`alūna Rizqakum 'Annakum Tukadhdhibūna | 82. Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? | وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ |
| Falawlā 'Idhā Balaghati Al-Ĥulqūma | 83. Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo, | فَلَوْلاَ إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ |
| Wa 'Antum Ĥīna'idhin Tanžurūna | 84. Na nyinyi wakati huo mnatazama! | وَأَنْتُمْ حِينَئِذ ٍ تَنظُرُونَ |
| Wa Naĥnu 'Aqrabu 'Ilayhi Minkum Wa Lakin Lā Tubşirūna | 85. Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi. | وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْكُمْ وَلَكِنْ لاَ تُبْصِرُونَ |
| Falawlā 'In Kuntum Ghayra Madīnīna | 86. Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu, | فَلَوْلاَ إِنْ كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ |
| Tarji`ūnahā 'In Kuntum Şādiqīna | 87. Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? | تَرْجِعُونَهَا إِنْ كُنتُمْ صَادِقِينَ |
| Fa'ammā 'In Kāna Mina Al-Muqarrabīna | 88. Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, | فَأَمَّا إِنْ كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ |
| Farawĥun Wa Rayĥānun Wa Jannatu Na`īmin | 89. Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. | فَرَوْح ٌ وَرَيْحَان ٌ وَجَنَّةُ نَعِيم ٍ |
| Wa 'Ammā 'In Kāna Min 'Aşĥābi Al-Yamīni | 90. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia, | وَأَمَّا إِنْ كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ |
| Fasalāmun Laka Min 'Aşĥābi Al-Yamīni | 91. Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. | فَسَلاَم ٌ لَكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ |
| Wa 'Ammā 'In Kāna Mina Al-Mukadhdhibīna Ađ-Đāllīna | 92. Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, | وَأَمَّا إِنْ كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ |
| Fanuzulun Min Ĥamīmin | 93. Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, | فَنُزُل ٌ مِنْ حَمِيم ٍ |
| Wa Taşliyatu Jaĥīmin | 94. Na kutiwa Motoni. | وَتَصْلِيَةُ جَحِيم ٍ |
| 'Inna Hādhā Lahuwa Ĥaqqu Al-Yaqīni | 95. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. | إِنَّ هَذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ |
| Fasabbiĥ Biāsmi Rabbika Al-`Ažīmi | 96. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. * | فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ |