54) Sūrat Al-Qamar | Printed format | 54) سُورَة القَمَر |
| Aqtarabati As-Sā`atu Wa Anshaqqa Al-Qamaru | 1. Saa imekaribia, na mwezi umepasuka! | اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانْشَقَّ الْقَمَرُ |
| Wa 'In Yaraw 'Āyatan Yu`riđū Wa Yaqūlū Siĥrun Mustamirrun | 2. Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea. | وَإِنْ يَرَوْا آيَة ً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْر ٌ مُسْتَمِرّ ٌ |
| Wa Kadhdhabū Wa Attaba`ū 'Ahwā'ahum Wa Kullu 'Amrin Mustaqirrun | 3. Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti. | وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ وَكُلُّ أَمْر ٍ مُسْتَقِرّ ٌ |
| Wa Laqad Jā'ahum Mina Al-'Anbā'i Mā Fīhi Muzdajarun | 4. Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio. | وَلَقَدْ جَاءَهُمْ مِنَ الأَنْبَاءِ مَا فِيه ِِ مُزْدَجَر ٌ |
| Ĥikmatun Bālighatun Famā Tughni An-Nudhuru | 5. Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu! | حِكْمَة ٌ بَالِغَة ٌ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ |
| Fatawalla `Anhum Yawma Yad`u Ad-Dā`i 'Ilá Shay'in Nukurin | 6. Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha; | فَتَوَلَّ عَنْهُمْ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَى شَيْء ٍ نُكُر ٍ |
| Khushsha`āan 'Abşāruhum Yakhrujūna Mina Al-'Ajdāthi Ka'annahum Jarādun Muntashirun | 7. Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika, | خُشَّعاً أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَاد ٌ مُنتَشِر ٌ |
| Muhţi`īna 'Ilá Ad-Dā`i Yaqūlu Al-Kāfirūna Hādhā Yawmun `Asirun | 8. Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu. | مُهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَذَا يَوْمٌ عَسِر ٌ |
| Kadhdhabat Qablahum Qawmu Nūĥin Fakadhdhabū `Abdanā Wa Qālū Majnūnun Wa Azdujira | 9. Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa. | كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوح ٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُون ٌ وَازْدُجِرَ |
| Fada`ā Rabbahu 'Annī Maghlūbun Fāntaşir | 10. Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru! | فَدَعَا رَبَّهُ~ُ أَنِّي مَغْلُوب ٌ فَانْتَصِرْ |
| Fafataĥnā 'Abwāba As-Samā'i Bimā'in Munhamirin | 11. Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika. | فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاء ٍ مُنْهَمِر ٍ |
| Wa Fajjarnā Al-'Arđa `Uyūnāan Fāltaqá Al-Mā'u `Alá 'Amrin Qad Qudira | 12. Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa. | وَفَجَّرْنَا الأَرْضَ عُيُونا ً فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَى أَمْر ٍ قَدْ قُدِرَ |
| Wa Ĥamalnāhu `Alá Dhāti 'Alwāĥin Wa Dusurin | 13. Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba. | وَحَمَلْنَاه ُُ عَلَى ذَاتِ أَلْوَاح ٍ وَدُسُر ٍ |
| Tajrī Bi'a`yuninā Jazā'an Liman Kāna Kufira | 14.Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa. | تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاء ً لِمَنْ كَانَ كُفِرَ |
| Wa Laqad Taraknāhā 'Āyatan Fahal Min Muddakirin | 15. Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka? | وَلَقَدْ تَرَكْنَاهَا آيَة ً فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Fakayfa Kāna `Adhābī Wa Nudhuri | 16. Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu. | فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ |
| Wa Laqad Yassarnā Al-Qur'āna Lildhdhikri Fahal Min Muddakirin | 17. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka? | وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Kadhdhabat `Ādun Fakayfa Kāna `Adhābī Wa Nudhuri | 18. Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu? | كَذَّبَتْ عَاد ٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ |
| 'Innā 'Arsalnā `Alayhim Rīĥāan Şarşarāan Fī Yawmi Naĥsin Mustamirrin | 19. Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo, | إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحا ً صَرْصَرا ً فِي يَوْمِ نَحْس ٍ مُسْتَمِرّ ٍ |
| Tanzi`u An-Nāsa Ka'annahum 'A`jāzu Nakhlin Munqa`irin | 20. Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa. | تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْل ٍ مُنْقَعِر ٍ |
| Fakayfa Kāna `Adhābī Wa Nudhuri | 21. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu? | فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ |
| Wa Laqad Yassarnā Al-Qur'āna Lildhdhikri Fahal Min Muddakirin | 22. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka? | وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Kadhdhabat Thamūdu Bin-Nudhuri | 23. Thamudi waliwakanusha Waonyaji. | كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ |
| Faqālū 'Abasharāan Minnā Wāĥidāan Nattabi`uhu 'Innā 'Idhāan Lafī Đalālin Wa Su`urin | 24. Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa! | فَقَالُوا أَبَشَرا ً مِنَّا وَاحِدا ً نَتَّبِعُهُ~ُ إِنَّا إِذا ً لَفِي ضَلاَل ٍ وَسُعُر ٍ |
| 'A'uulqiya Adh-Dhikru `Alayhi Min Bayninā Bal Huwa Kadhdhābun 'Ashirun | 25. Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi! | أَؤُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنْ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِر ٌ |
| Saya`lamūna Ghadāan Mani Al-Kadhdhābu Al-'Ashiru | 26. Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi. | سَيَعْلَمُونَ غَدا ً مَنِ الْكَذَّابُ الأَشِرُ |
| 'Innā Mursilū An-Nāqati Fitnatan Lahum Fārtaqibhum Wa Aşţabir | 27. Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili. | إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَة ً لَهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ |
| Wa Nabbi'hum 'Anna Al-Mā'a Qismatun Baynahum Kullu Shirbin Muĥtađarun | 28. Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika. | وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَة ٌ بَيْنَهُمْ كُلُّ شِرْب ٍ مُحْتَضَر ٌ |
| Fanādaw Şāĥibahum Fata`āţá Fa`aqara | 29. Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja. | فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَى فَعَقَرَ |
| Fakayfa Kāna `Adhābī Wa Nudhuri | 30. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu! | فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ |
| 'Innā 'Arsalnā `Alayhim Şayĥatan Wāĥidatan Fakānū Kahashīmi Al-Muĥtažiri | 31. Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa. | إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَة ً وَاحِدَة ً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ |
| Wa Laqad Yassarnā Al-Qur'āna Lildhdhikri Fahal Min Muddakirin | 32. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye? | وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Kadhdhabat Qawmu Lūţin Bin-Nudhuri | 33. Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji. | كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوط ٍ بِالنُّذُرِ |
| 'Innā 'Arsalnā `Alayhim Ĥāşibāan 'Illā 'Āla Lūţin Najjaynāhum Bisaĥarin | 34. Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri. | إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبا ً إِلاَّ آلَ لُوط ٍ نَجَّيْنَاهُمْ بِسَحَر ٍ |
| Ni`matan Min `Indinā Kadhālika Najzī Man Shakara | 35. Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru. | نِعْمَة ً مِنْ عِنْدِنَا كَذَلِكَ نَجْزِي مَنْ شَكَرَ |
| Wa Laqad 'Andharahum Baţshatanā Fatamāraw Bin-Nudhuri | 36. Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo. | وَلَقَدْ أَنذَرَهُمْ بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ |
| Wa Laqad Rāwadūhu `An Đayfihi Faţamasnā 'A`yunahum Fadhūqū `Adhābī Wa Nudhuri | 37. Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu! | وَلَقَدْ رَاوَدُوه ُُ عَنْ ضَيْفِه ِِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ |
| Wa Laqad Şabbaĥahum Bukratan `Adhābun Mustaqirrun | 38. Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea. | وَلَقَدْ صَبَّحَهُمْ بُكْرَةً عَذَاب ٌ مُسْتَقِرّ ٌ |
| Fadhūqū `Adhābī Wa Nudhuri | 39. Basi onjeni adhabu na maonyo yangu! | فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ |
| Wa Laqad Yassarnā Al-Qur'āna Lildhdhikri Fahal Min Muddakirin | 40. Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka? | وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Wa Laqad Jā'a 'Āla Fir`awna An-Nudhuru | 41. Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni. | وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ |
| Kadhdhabū Bi'āyātinā Kullihā Fa'akhadhnāhum 'Akhdha `Azīzin Muqtadirin | 42. Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza. | كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيز ٍ مُقْتَدِر ٍ |
| 'Akuffārukum Khayrun Min 'Ūla'ikum 'Am Lakum Barā'atun Fī Az-Zuburi | 43. Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani? | أَكُفَّارُكُمْ خَيْر ٌ مِنْ أُوْلَئِكُمْ أَمْ لَكُمْ بَرَاءَة ٌ فِي الزُّبُرِ |
| 'Am Yaqūlūna Naĥnu Jamī`un Muntaşirun | 44. Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu. | أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيع ٌ مُنْتَصِر ٌ |
| Sayuhzamu Al-Jam`u Wa Yuwallūna Ad-Dubura | 45. Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma. | سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ |
| Bali As-Sā`atu Maw`iduhum Wa As-Sā`atu 'Ad/há Wa 'Amarru | 46. Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi. | بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَى وَأَمَرُّ |
| 'Inna Al-Mujrimīna Fī Đalālin Wa Su`urin | 47. Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu. | إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلاَل ٍ وَسُعُر ٍ |
| Yawma Yusĥabūna Fī An-Nāri `Alá Wujūhihim Dhūqū Massa Saqara | 48. Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu! | يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَى وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ |
| 'Innā Kulla Shay'in Khalaqnāhu Biqadarin | 49. Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo. | إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاه ُُ بِقَدَر ٍ |
| Wa Mā 'Amrunā 'Illā Wāĥidatun Kalamĥin Bil-Başari | 50. Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho. | وَمَا أَمْرُنَا إِلاَّ وَاحِدَة ٌ كَلَمْح ٍ بِالْبَصَرِ |
| Wa Laqad 'Ahlaknā 'Ashyā`akum Fahal Min Muddakirin | 51. Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka? | وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِنْ مُدَّكِر ٍ |
| Wa Kullu Shay'in Fa`alūhu Fī Az-Zuburi | 52. Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni. | وَكُلُّ شَيْء ٍ فَعَلُوه ُُ فِي الزُّبُرِ |
| Wa Kullu Şaghīrin Wa Kabīrin Mustaţarun | 53. Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa. | وَكُلُّ صَغِير ٍ وَكَبِير ٍ مُسْتَطَر ٌ |
| 'Inna Al-Muttaqīna Fī Jannātin Wa Naharin | 54. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito. | إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّات ٍ وَنَهَر ٍ |
| Fī Maq`adi Şidqin `Inda Malīkin Muqtadirin | 55. Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza. * | فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِنْدَ مَلِيك ٍ مُقْتَدِر ٍ |