52) Sūrat Aţ-Ţūr | Printed format | 52) سُورَة الطُّور |
| Wa Aţ-Ţūri | 1. Naapa kwa mlima wa T'ur, | وَالطُّورِ |
| Wa Kitābin Masţūrin | 2. Na Kitabu kilicho andikwa | وَكِتَاب ٍ مَسْطُور ٍ |
| Fī Raqqin Manshūrin | 3. Katika ngozi iliyo kunjuliwa, | فِي رَقّ ٍ مَنْشُور ٍ |
| Wa Al-Bayti Al-Ma`mūri | 4. Na kwa Nyumba iliyo jengwa, | وَالْبَيْتِ الْمَعْمُورِ |
| Wa As-Saqfi Al-Marfū`i | 5. Na kwa dari iliyo nyanyuliwa, | وَالسَّقْفِ الْمَرْفُوعِ |
| Wa Al-Baĥri Al-Masjūri | 6. Na kwa bahari iliyo jazwa, | وَالْبَحْرِ الْمَسْجُورِ |
| 'Inna `Adhāba Rabbika Lawāqi`un | 7. Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea. | إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَاقِع ٌ |
| Mā Lahu Min Dāfi`in | 8. Hapana wa kuizuia. | مَا لَه ُُ مِنْ دَافِع ٍ |
| Yawma Tamūru As-Samā'u Mawrāan | 9. Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso, | يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرا ً |
| Wa Tasīru Al-Jibālu Sayrāan | 10. Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa. | وَتَسِيرُ الْجِبَالُ سَيْرا ً |
| Fawaylun Yawma'idhin Lilmukadhdhibīna | 11. Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha, | فَوَيْل ٌ يَوْمَئِذ ٍ لِلْمُكَذِّبِينَ |
| Al-Ladhīna Hum Fī Khawđin Yal`abūna | 12. Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi. | الَّذِينَ هُمْ فِي خَوْض ٍ يَلْعَبُونَ |
| Yawma Yuda``ūna 'Ilá Nāri Jahannama Da``āan | 13. Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu, | يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَى نَارِ جَهَنَّمَ دَعّا ً |
| Hadhihi An-Nāru Allatī Kuntum Bihā Tukadhdhibūna | 14. (Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha! | هَذِهِ النَّارُ الَّتِي كُنتُمْ بِهَا تُكَذِّبُونَ |
| 'Afasiĥrun Hādhā 'Am 'Antum Lā Tubşirūna | 15. Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu? | أَفَسِحْرٌ هَذَا أَمْ أَنْتُمْ لاَ تُبْصِرُونَ |
| Aşlawhā Fāşbirū 'Aw Lā Taşbirū Sawā'un `Alaykum 'Innamā Tujzawna Mā Kuntum Ta`malūna | 16. Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda. | اصْلَوْهَا فَاصْبِرُوا أَوْ لاَ تَصْبِرُوا سَوَاءٌ عَلَيْكُمْ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ |
| 'Inna Al-Muttaqīna Fī Jannātin Wa Na`īmin | 17. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema, | إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّات ٍ وَنَعِيم ٍ |
| Fākihīna Bimā 'Ātāhum Rabbuhum Wa Waqāhum Rabbuhum `Adhāba Al-Jaĥīmi | 18. Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni. | فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ |
| Kulū Wa Ashrabū Hanī'āan Bimā Kuntum Ta`malūna | 19. Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda. | كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئا ً بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ |
| Muttaki'īna `Alá Sururin Maşfūfatin Wa Zawwajnāhum Biĥūrin `Īnin | 20. Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini. | مُتَّكِئِينَ عَلَى سُرُر ٍ مَصْفُوفَة ٍ وَزَوَّجْنَاهُمْ بِحُورٍ عِين ٍ |
| Wa Al-Ladhīna 'Āmanū Wa Attaba`at/hum Dhurrīyatuhum Bi'īmānin 'Alĥaqnā Bihim Dhurrīyatahum Wa Mā 'Alatnāhum Min `Amalihim Min Shay'in Kullu Amri'in Bimā Kasaba Rahīnun | 21. Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma. | وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُمْ بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُمْ مِنْ عَمَلِهِمْ مِنْ شَيْء ٍ كُلُّ امْرِئ ٍ بِمَا كَسَبَ رَهِين ٌ |
| Wa 'Amdadnāhum Bifākihatin Wa Laĥmin Mimmā Yashtahūna | 22. Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda. | وَأَمْدَدْنَاهُمْ بِفَاكِهَة ٍ وَلَحْم ٍ مِمَّا يَشْتَهُونَ |
| Yatanāza`ūna Fīhā Ka'sāan Lā Laghwun Fīhā Wa Lā Ta'thīmun | 23. Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi. | يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسا ً لاَ لَغْو ٌ فِيهَا وَلاَ تَأْثِيم ٌ |
| Wa Yaţūfu `Alayhim Ghilmānun Lahum Ka'annahum Lu'ulu'uun Maknūnun | 24. Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza. | وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَان ٌ لَهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤ ٌ مَكْنُون ٌ |
| Wa 'Aqbala Ba`đuhum `Alá Ba`đin Yatasā'alūna | 25. Wataelekeana wakiulizana. | وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَى بَعْض ٍ يَتَسَاءَلُونَ |
| Qālū 'Innā Kunnā Qablu Fī 'Ahlinā Mushfiqīna | 26. Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa; | قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ |
| Famanna Allāhu `Alaynā Wa Waqānā `Adhāba As-Samūmi | 27. Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto. | فَمَنَّ اللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ |
| 'Innā Kunnā Min Qablu Nad`ūhu 'Innahu Huwa Al-Barru Ar-Raĥīmu | 28. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu. | إِنَّا كُنَّا مِنْ قَبْلُ نَدْعُوهُ~ُ إِنَّه ُُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ |
| Fadhakkir Famā 'Anta Bini`mati Rabbika Bikāhinin Wa Lā Majnūnin | 29. Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu. | فَذَكِّرْ فَمَا أَنْتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِكَاهِن ٍ وَلاَ مَجْنُون ٍ |
| 'Am Yaqūlūna Shā`irun Natarabbaşu Bihi Rayba Al-Manūni | 30. Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari. | أَمْ يَقُولُونَ شَاعِر ٌ نَتَرَبَّصُ بِه ِِ رَيْبَ الْمَنُونِ |
| Qul Tarabbaşū Fa'innī Ma`akum Mina Al-Mutarabbişīna | 31. Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia. | قُلْ تَرَبَّصُوا فَإِنِّي مَعَكُمْ مِنَ الْمُتَرَبِّصِينَ |
| 'Am Ta'muruhum 'Aĥlāmuhum Bihadhā 'Am Hum Qawmun Ţāghūna | 32. Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu? | أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلاَمُهُمْ بِهَذَا أَمْ هُمْ قَوْم ٌ طَاغُونَ |
| 'Am Yaqūlūna Taqawwalahu Bal Lā Yu'uminūna | 33. Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini! | أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَه ُُ بَل لاَ يُؤْمِنُونَ |
| Falya'tū Biĥadīthin Mithlihi 'In Kānū Şādiqīna | 34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli. | فَلْيَأْتُوا بِحَدِيث ٍ مِثْلِهِ~ِ إِنْ كَانُوا صَادِقِينَ |
| 'Am Khuliqū Min Ghayri Shay'in 'Am Humu Al-Khāliqūna | 35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji? | أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ |
| 'Am Khalaqū As-Samāwāti Wa Al-'Arđa Bal Lā Yūqinūna | 36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini. | أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ بَل لاَ يُوقِنُونَ |
| 'Am `Indahum Khazā'inu Rabbika 'Am Humu Al-Musayţirūna | 37. Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka? | أَمْ عِنْدَهُمْ خَزَائِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ الْمُسَيْطِرُونَ |
| 'Am Lahum Sullamun Yastami`ūna Fīhi Falya'ti Mustami`uhum Bisulţānin Mubīnin | 38. Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi! | أَمْ لَهُمْ سُلَّم ٌ يَسْتَمِعُونَ فِيه ِِ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُمْ بِسُلْطَان ٍ مُبِين ٍ |
| 'Am Lahu Al-Banātu Wa Lakumu Al-Banūna | 39. Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana? | أَمْ لَهُ الْبَنَاتُ وَلَكُمُ الْبَنُونَ |
| 'Am Tas'aluhum 'Ajrāan Fahum Min Maghramin Muthqalūna | 40. Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama? | أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرا ً فَهُمْ مِنْ مَغْرَم ٍ مُثْقَلُونَ |
| 'Am `Indahumu Al-Ghaybu Fahum Yaktubūna | 41. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika? | أَمْ عِنْدَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ |
| 'Am Yurīdūna Kaydāan Fa-Al-Ladhīna Kafarū Humu Al-Makīdūna | 42. Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka. | أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدا ً فَالَّذِينَ كَفَرُوا هُمُ الْمَكِيدُونَ |
| 'Am Lahum 'Ilahun Ghayru Allāhi Subĥāna Allāhi `Ammā Yushrikūna | 43. Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye. | أَمْ لَهُمْ إِلَه ٌٌ غَيْرُ اللَّهِ سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ |
| Wa 'In Yaraw Kisfāan Mina As-Samā'i Sāqiţāan Yaqūlū Saĥābun Markūmun | 44. Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana. | وَإِنْ يَرَوْا كِسْفا ً مِنَ السَّمَاءِ سَاقِطا ً يَقُولُوا سَحَاب ٌ مَرْكُوم ٌ |
| Fadharhum Ĥattá Yulāqū Yawmahumu Al-Ladhī Fīhi Yuş`aqūna | 45. Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa. | فَذَرْهُمْ حَتَّى يُلاَقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي فِيه ِِ يُصْعَقُونَ |
| Yawma Lā Yughnī `Anhum Kayduhum Shay'āan Wa Lā Hum Yunşarūna | 46. Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa. | يَوْمَ لاَ يُغْنِي عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئا ً وَلاَ هُمْ يُنصَرُونَ |
| Wa 'Inna Lilladhīna Žalamū `Adhābāan Dūna Dhālika Wa Lakinna 'Aktharahum Lā Ya`lamūna | 47. Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui. | وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا عَذَابا ً دُونَ ذَلِكَ وَلَكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ |
| Wa Aşbir Liĥukmi Rabbika Fa'innaka Bi'a`yuninā Wa Sabbiĥ Biĥamdi Rabbika Ĥīna Taqūmu | 48. Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama, | وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ |
| Wa Mina Al-Layli Fasabbiĥhu Wa 'Idbāra An-Nujūmi | 49. Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota. * | وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَارَ النُّجُومِ |