51) Sūrat Adh-Dhāriyāt | Printed format | 51) سُورَة الذَّارِيَات |
| Wa Adh-Dhāriyāti Dharwan | 1. Naapa kwa pepo zinazo tawanya, | وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوا ً |
| Fālĥāmilāti Wiqrāan | 2. Na zinazo beba mizigo, | فَالْحَامِلاَتِ وِقْرا ً |
| Fāljāriyāti Yusrāan | 3. Na zinazo kwenda kwa wepesi. | فَالْجَارِيَاتِ يُسْرا ً |
| Fālmuqassimāti 'Amrāan | 4. Na zinazo gawanya kwa amri, | فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرا ً |
| 'Innamā Tū`adūna Laşādiqun | 5. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli, | إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِق ٌ |
| Wa 'Inna Ad-Dīna Lawāqi`un | 6. Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea. | وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِع ٌ |
| Wa As-Samā'i Dhāti Al-Ĥubuki | 7. Naapa kwa mbingu zenye njia, | وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ |
| 'Innakum Lafī Qawlin Mukhtalifin | 8. Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana. | إِنَّكُمْ لَفِي قَوْل ٍ مُخْتَلِف ٍ |
| Yu'ufaku `Anhu Man 'Ufika | 9. Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa. | يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ |
| Qutila Al-Kharrāşūna | 10. Wazushi wameangamizwa. | قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ |
| Al-Ladhīna Hum Fī Ghamratin Sāhūna | 11. Ambao wameghafilika katika ujinga. | الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَة ٍ سَاهُونَ |
| Yas'alūna 'Ayyāna Yawmu Ad-Dīni | 12. Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo? | يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ |
| Yawma Hum `Alá An-Nāri Yuftanūna | 13. Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni. | يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ |
| Dhūqū Fitnatakum Hādhā Al-Ladhī Kuntum Bihi Tasta`jilūna | 14. Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza. | ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَذَا الَّذِي كُنتُمْ بِه ِِ تَسْتَعْجِلُونَ |
| 'Inna Al-Muttaqīna Fī Jannātin Wa `Uyūnin | 15. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. | إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّات ٍ وَعُيُون ٍ |
| 'Ākhidhīna Mā 'Ātāhum Rabbuhum 'Innahum Kānū Qabla Dhālika Muĥsinīna | 16. Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. | آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُحْسِنِينَ |
| Kānū Qalīlāan Mina Al-Layli Mā Yahja`ūna | 17. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. | كَانُوا قَلِيلا ً مِنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ |
| Wa Bil-'Asĥāri Hum Yastaghfirūna | 18. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira. | وَبِالأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ |
| Wa Fī 'Amwālihim Ĥaqqun Lilssā'ili Wa Al-Maĥrūmi | 19. Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba. | وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقّ ٌ لِلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ |
| Wa Fī Al-'Arđi 'Āyātun Lilmūqinīna | 20. Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini. | وَفِي الأَرْضِ آيَات ٌ لِلْمُوقِنِينَ |
| Wa Fī 'Anfusikum 'Afalā Tubşirūna | 21. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni? | وَفِي أَنفُسِكُمْ أَفَلاَ تُبْصِرُونَ |
| Wa Fī As-Samā'i Rizqukum Wa Mā Tū`adūna | 22. Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa. | وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ |
| Fawarabbi As-Samā'i Wa Al-'Arđi 'Innahu Laĥaqqun Mithla Mā 'Annakum Tanţiqūna | 23. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema. | فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالأَرْضِ إِنَّه ُُ لَحَقّ ٌ مِثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ |
| Hal 'Atāka Ĥadīthu Đayfi 'Ibrāhīma Al-Mukramīna | 24. Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa? | هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ |
| 'Idh Dakhalū `Alayhi Faqālū Salāmāan Qāla Salāmun Qawmun Munkarūna | 25. Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni. | إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلاَما ً قَالَ سَلاَم ٌ قَوْم ٌ مُنكَرُونَ |
| Farāgha 'Ilá 'Ahlihi Fajā'a Bi`ijlin Samīnin | 26. Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona. | فَرَاغَ إِلَى أَهْلِه ِِ فَجَاءَ بِعِجْل ٍ سَمِين ٍ |
| Faqarrabahu 'Ilayhim Qāla 'Alā Ta'kulūna | 27. Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli? | فَقَرَّبَهُ~ُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلاَ تَأْكُلُونَ |
| Fa'awjasa Minhum Khīfatan Qālū Lā Takhaf Wa Bashsharūhu Bighulāmin `Alīmin | 28. Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu. | فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَة ً قَالُوا لاَ تَخَفْ وَبَشَّرُوه ُُ بِغُلاَمٍ عَلِيم ٍ |
| Fa'aqbalati Amra'atuhu Fī Şarratin Faşakkat Wajhahā Wa Qālat `Ajūzun `Aqīmun | 29. Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa! | فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُه ُُ فِي صَرَّة ٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيم ٌ |
| Qālū Kadhāliki Qāla Rabbuki 'Innahu Huwa Al-Ĥakīmu Al-`Alīmu | 30. Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua. | قَالُوا كَذَلِكِ قَالَ رَبُّكِ إِنَّه ُُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ |
| Qāla Famā Khaţbukum 'Ayyuhā Al-Mursalūna | 31. AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa? | قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ |
| Qālū 'Innā 'Ursilnā 'Ilá Qawmin Mujrimīna | 32. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu, | قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَى قَوْم ٍ مُجْرِمِينَ |
| Linursila `Alayhim Ĥijāratan Min Ţīnin | 33. Tuwatupie mawe ya udongo, | لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَة ً مِنْ طِين ٍ |
| Musawwamatan `Inda Rabbika Lilmusrifīna | 34. Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka. | مُسَوَّمَةً عِنْدَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ |
| Fa'akhrajnā Man Kāna Fīhā Mina Al-Mu'uminīna | 35. Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini. | فَأَخْرَجْنَا مَنْ كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ |
| Famā Wajadnā Fīhā Ghayra Baytin Mina Al-Muslimīna | 36. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu! | فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْت ٍ مِنَ الْمُسْلِمِينَ |
| Wa Taraknā Fīhā 'Āyatan Lilladhīna Yakhāfūna Al-`Adhāba Al-'Alīma | 37. Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu. | وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَة ً لِلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الأَلِيمَ |
| Wa Fī Mūsá 'Idh 'Arsalnāhu 'Ilá Fir`awna Bisulţānin Mubīnin | 38. Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi. | وَفِي مُوسَى إِذْ أَرْسَلْنَاهُ~ُ إِلَى فِرْعَوْنَ بِسُلْطَان ٍ مُبِين ٍ |
| Fatawallá Biruknihi Wa Qāla Sāĥirun 'Aw Majnūnun | 39. Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu! | فَتَوَلَّى بِرُكْنِه ِِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُون ٌ |
| Fa'akhadhnāhu Wa Junūdahu Fanabadhnāhum Fī Al-Yammi Wa Huwa Mulīmun | 40. Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa. | فَأَخَذْنَاه ُُ وَجُنُودَه ُُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيم ٌ |
| Wa Fī `Ādin 'Idh 'Arsalnā `Alayhimu Ar-Rīĥa Al-`Aqīma | 41. Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi. | وَفِي عَاد ٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ |
| Mā Tadharu Min Shay'in 'Atat `Alayhi 'Illā Ja`alat/hu Kālrramīmi | 42. Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka. | مَا تَذَرُ مِنْ شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلاَّ جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ |
| Wa Fī Thamūda 'Idh Qīla Lahum Tamatta`ū Ĥattá Ĥīnin | 43. Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu. | وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّى حِين ٍ |
| Fa`ataw `An 'Amri Rabbihim Fa'akhadhat/humu Aş-Şā`iqatu Wa Hum Yanžurūna | 44. Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona. | فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ |
| Famā Astaţā`ū Min Qiyāmin Wa Mā Kānū Muntaşirīna | 45. Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea. | فَمَا اسْتَطَاعُوا مِنْ قِيَام ٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ |
| Wa Qawma Nūĥin Min Qablu 'Innahum Kānū Qawmāan Fāsiqīna | 46. Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu. | وَقَوْمَ نُوح ٍ مِنْ قَبْلُ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْما ً فَاسِقِينَ |
| Wa As-Samā'a Banaynāhā Bi'ayydin Wa 'Innā Lamūsi`ūna | 47. Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua. | وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْيد ٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ |
| Wa Al-'Arđa Farashnāhā Fani`ma Al-Māhidūna | 48. Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi! | وَالأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ |
| Wa Min Kulli Shay'in Khalaqnā Zawjayni La`allakum Tadhakkarūna | 49. Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie. | وَمِنْ كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ |
| Fafirrū 'Ilá Allāhi 'Innī Lakum Minhu Nadhīrun Mubīnun | 50. Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. | فَفِرُّوا إِلَى اللَّهِ إِنِّي لَكُمْ مِنْهُ نَذِير ٌ مُبِين ٌ |
| Wa Lā Taj`alū Ma`a Allāhi 'Ilahāan 'Ākhara 'Innī Lakum Minhu Nadhīrun Mubīnun | 51. Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. | وَلاَ تَجْعَلُوا مَعَ اللَّهِ إِلَها ً آخَرَ إِنِّي لَكُمْ مِنْهُ نَذِير ٌ مُبِين ٌ |
| Kadhālika Mā 'Atá Al-Ladhīna Min Qablihim Min Rasūlin 'Illā Qālū Sāĥirun 'Aw Majnūnun | 52. Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu. | كَذَلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِنْ قَبْلِهِمْ مِنْ رَسُول ٍ إِلاَّ قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُون ٌ |
| 'Atawāşaw Bihi Bal Hum Qawmun Ţāghūna | 53. Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi. | أَتَوَاصَوْا بِه ِِ بَلْ هُمْ قَوْم ٌ طَاغُونَ |
| Fatawalla `Anhum Famā 'Anta Bimalūmin | 54. Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi. | فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنْتَ بِمَلُوم ٍ |
| Wa Dhakkir Fa'inna Adh-Dhikrá Tanfa`u Al-Mu'uminīna | 55. Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini. | وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَى تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ |
| Wa Mā Khalaqtu Al-Jinna Wa Al-'Insa 'Illā Liya`budūni | 56. Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi. | وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالإِنسَ إِلاَّ لِيَعْبُدُونِ |
| Mā 'Urīdu Minhum Min Rizqin Wa Mā 'Urīdu 'An Yuţ`imūni | 57. Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe. | مَا أُرِيدُ مِنْهُمْ مِنْ رِزْق ٍ وَمَا أُرِيدُ أَنْ يُطْعِمُونِ |
| 'Inna Allāha Huwa Ar-Razzāqu Dhū Al-Qūwati Al-Matīnu | 58. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti. | إِنَّ اللَّهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ |
| Fa'inna Lilladhīna Žalamū Dhanūbāan Mithla Dhanūbi 'Aşĥābihim Falā Yasta`jilūni | 59. Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize. | فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبا ً مِثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلاَ يَسْتَعْجِلُونِ |
| Fawaylun Lilladhīna Kafarū Min Yawmihimu Al-Ladhī Yū`adūna | 60. Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa. * | فَوَيْل ٌ لِلَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ |