Ţā-Sīn-Mīm  | 1. T'A SIN MIM, (T'.S.M.) | طَا-سِين-مِيم |
Tilka 'Āyātu Al-Kitābi Al-Mubīni  | 2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha. | تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ |
Natlū `Alayka Min Naba'i Mūsá Wa Fir`awna Bil-Ĥaqqi Liqawmin Yu'uminūna  | 3. Tunakusomea khabari za Musa na Firauni kwa
Haki kwa ajili ya watu wanao amini. | نَتْلُو عَلَيْكَ مِنْ نَبَإِ مُوسَى وَفِرْعَوْنَ بِالْحَقِّ لِقَوْم ٍ يُؤْمِنُونَ |
'Inna Fir`awna `Alā Fī Al-'Arđi Wa Ja`ala 'Ahlahā Shiya`āan Yastađ`ifu Ţā'ifatan Minhum Yudhabbiĥu 'Abnā'ahum Wa Yastaĥyī Nisā'ahum 'Innahu Kāna Mina Al-Mufsidīna  | 4. Hakika Firauni alitakabari katika nchi, na
akawagawa wananchi makundi mbali mbali. Akalidhoofisha taifa moja miongoni
mwao, akiwachinja watoto wao wanaume na akiwaacha watoto wao wanawake.
Hakika yeye alikuwa katika mafisadi. | إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلاَ فِي الأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعا ً يَسْتَضْعِفُ طَائِفَة ً مِنْهُمْ يُذَبِّحُ أَبْنَاءَهُمْ وَيَسْتَحْيِي نِسَاءَهُمْ إِنَّه ُُ كَانَ مِنَ الْمُفْسِدِينَ |
Wa Nurīdu 'An Namunna `Alá Al-Ladhīna Astuđ`ifū Fī Al-'Arđi Wa Naj`alahum 'A'immatan Wa Naj`alahumu Al-Wārithīna  | 5. Na tukataka kuwafadhili walio dhoofishwa katika
nchi hiyo na kuwafanya wawe waongozi na kuwafanya ni warithi. | وَنُرِيدُ أَنْ نَمُنَّ عَلَى الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا فِي الأَرْضِ وَنَجْعَلَهُمْ أَئِمَّة ً وَنَجْعَلَهُمُ الْوَارِثِينَ |
Wa Numakkina Lahum Fī Al-'Arđi Wa Nuriya Fir`awna Wa Hāmāna Wa Junūdahumā Minhum Mā Kānū Yaĥdharūna  | 6. Na kuwapa nguvu katika nchi, na kutokana na
wao kuwaonyesha kina Firauni na Hamana na majeshi yao mambo yale waliyo
kuwa wakiyaogopa. | وَنُمَكِّنَ لَهُمْ فِي الأَرْضِ وَنُرِيَ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا مِنْهُمْ مَا كَانُوا يَحْذَرُونَ |
Wa 'Awĥaynā 'Ilá 'Ummi Mūsá 'An 'Arđi`īhi Fa'idhā Khifti `Alayhi Fa'alqīhi Fī Al-Yammi Wa Lā Takhāfī Wa Lā Taĥzanī 'Innā Rāddūhu 'Ilayki Wa Jā`ilūhu Mina Al-Mursalīna  | 7. Tulimfunulia mama yake Musa kwa kumwambia:
Mnyonyeshe. Na utakapo mkhofia basi mtie mtoni, na usikhofu wala usihuzunike.
Hakika Sisi tutamrudisha kwako na tutamfanya miongoni mwa Mitume. | وَأَوْحَيْنَا إِلَى أُمِّ مُوسَى أَنْ أَرْضِعِيه ِِ فَإِذَا خِفْتِ عَلَيْهِ فَأَلْقِيه ِِ فِي الْيَمِّ وَلاَ تَخَافِي وَلاَ تَحْزَنِي إِنَّا رَادُّوهُ~ُ إِلَيْكِ وَجَاعِلُوه ُُ مِنَ الْمُرْسَلِينَ |
Fāltaqaţahu 'Ālu Fir`awna Liyakūna Lahum `Adūwāan Wa Ĥazanāan 'Inna Fir`awna Wa Hāmāna Wa Junūdahumā Kānū Khāţi'īna  | 8. Basi wakamwokota watu wa Firauni, aje kuwa
adui kwao na huzuni. Hakika Firauni na Hamana na majeshi yao walikuwa wenye
makosa. | فَالْتَقَطَهُ آلُ فِرْعَوْنَ لِيَكُونَ لَهُمْ عَدُوّا ً وَحَزَنا ً إِنَّ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا كَانُوا خَاطِئِينَ |
Wa Qālat Amra'atu Fir`awna Qurratu `Aynin Lī Wa Laka Lā Taqtulūhu `Asá 'An Yanfa`anā 'Aw Nattakhidhahu Waladāan Wa Hum Lā Yash`urūna  | 9. Na mkewe Firauni alisema: Atakuwa kiburudisho
cha macho kwangu na kwako. Msimuuwe! Huenda akatufaa, au tumpange kuwa
mwenetu. Wala wao hawakutambua. | وَقَالَتْ امْرَأَةُ فِرْعَوْنَ قُرَّةُ عَيْن ٍ لِي وَلَكَ لاَ تَقْتُلُوه ُُ عَسَى أَنْ يَنفَعَنَا أَوْ نَتَّخِذَه ُُ وَلَدا ً وَهُمْ لاَ يَشْعُرُونَ |
Wa 'Aşbaĥa Fu'uādu 'Ummi Mūsá Fārighāan 'In Kādat Latubdī Bihi Lawlā 'An Rabaţnā `Alá Qalbihā Litakūna Mina Al-Mu'uminīna  | 10. Na moyo wa mama yake Musa ukawa mtupu. Alikuwa
karibu kumdhihirisha, ingeli kuwa hatukumtia nguvu moyo wake ili awe miongoni
mwa Waumini. | وَأَصْبَحَ فُؤَادُ أُمِّ مُوسَى فَارِغا ً إِنْ كَادَتْ لَتُبْدِي بِه ِِ لَوْلاَ أَنْ رَبَطْنَا عَلَى قَلْبِهَا لِتَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ |
Wa Qālat Li'khtihi Quşşīhi Fabaşurat Bihi `An Junubin Wa Hum Lā Yash`urūna  | 11. Naye akamwambia dada yake Musa: Mfuatie.
Basi naye akawa anamuangalia kwa mbali bila ya wao kujua. | وَقَالَتْ لِأخْتِه ِِ قُصِّيه ِِ فَبَصُرَتْ بِه ِِ عَنْ جُنُب ٍ وَهُمْ لاَ يَشْعُرُونَ |
Wa Ĥarramnā `Alayhi Al-Marāđi`a Min Qablu Faqālat Hal 'Adullukum `Alá 'Ahli Baytin Yakfulūnahu Lakum Wa Hum Lahu Nāşiĥūna  | 12. Na tukamjaalia awakatae wanyonyeshaji wote
tangu mwanzo, mpaka dada yake akasema: Je! Nikuonyesheni watu wa nyumba
watakao mlea kwa ajili yenu, nao pia watakuwa wema kwake? | وَحَرَّمْنَا عَلَيْهِ الْمَرَاضِعَ مِنْ قَبْلُ فَقَالَتْ هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَى أَهْلِ بَيْت ٍ يَكْفُلُونَه ُُ لَكُمْ وَهُمْ لَه ُُ نَاصِحُونَ |
Faradadnāhu 'Ilá 'Ummihi Kay Taqarra `Aynuhā Wa Lā Taĥzana Wa Lita`lama 'Anna Wa`da Allāhi Ĥaqqun Wa Lakinna 'Aktharahum Lā Ya`lamūna  | 13. Basi tukamrudisha kwa mama yake ili macho
yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ajue ya kwamba ahadi ya Mwenyezi
Mungu ni ya kweli, lakini wengi wao hawajui. | فَرَدَدْنَاهُ~ُ إِلَى أُمِّه ِِ كَيْ تَقَرَّ عَيْنُهَا وَلاَ تَحْزَنَ وَلِتَعْلَمَ أَنَّ وَعْدَ اللَّهِ حَقّ ٌ وَلَكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ |
Wa Lammā Balagha 'Ashuddahu Wa Astawá 'Ātaynāhu Ĥukmāan Wa `Ilmāan Wa Kadhalika Najzī Al-Muĥsinīna  | 14. Na Musa alipo fika utu-uzima baraabara, tulimpa
akili na ilimu. Na hivi ndivyo tunavyo walipa walio wema. | وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّه ُُ وَاسْتَوَى آتَيْنَاه ُُ حُكْما ً وَعِلْما ً وَكَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
Wa Dakhala Al-Madīnata `Alá Ĥīni Ghaflatin Min 'Ahlihā Fawajada Fīhā Rajulayni Yaqtatilāni Hādhā Min Shī`atihi Wa Hadhā Min `Adūwihi Fāstaghāthahu Al-Ladhī Min Shī`atihi `Alá Al-Ladhī Min `Adūwihi Fawakazahu Mūsá Faqađá `Alayhi Qāla Hādhā Min `Amali Ash-Shayţāni 'Innahu `Adūwun Muđillun Mubīnun  | 15. Na akaingia mjini wakati wa kughafilika wenyeji
wake, na akakuta humo watu wawili wanapigana - mmoja ni katika wenzake,
na mwengine katika maadui zake. Yule mwenzake alimtaka msaada kumpiga adui
yake. Musa akampiga ngumi, akamuuwa. Akasema: Hiki ni kitendo cha Shet'ani;
hakika yeye ni adui, mpotezaji dhaahiri. | وَدَخَلَ الْمَدِينَةَ عَلَى حِينِ غَفْلَة ٍ مِنْ أَهْلِهَا فَوَجَدَ فِيهَا رَجُلَيْنِ يَقْتَتِلاَنِ هَذَا مِنْ شِيعَتِه ِِ وَهَذَا مِنْ عَدُوِّه ِِ فَاسْتَغَاثَهُ الَّذِي مِنْ شِيعَتِه ِِ عَلَى الَّذِي مِنْ عَدُوِّه ِِ فَوَكَزَه ُُ مُوسَى فَقَضَى عَلَيْهِ قَالَ هَذَا مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ إِنَّه ُُ عَدُوّ ٌ مُضِلّ ٌ مُبِين ٌ |
Qāla Rabbi 'Innī Žalamtu Nafsī Fāghfir Lī Faghafara Lahu 'Innahu Huwa Al-Ghafūru Ar-Raĥīmu  | 16. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimejidhulumu
nafsi yangu; basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwenye kusamehe
Mwenye kurehemu. | قَالَ رَبِّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي فَغَفَرَ لَهُ~ُ إِنَّه ُُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ |
Qāla Rabbi Bimā 'An`amta `Alayya Falan 'Akūna Žahīrāan Lilmujrimīna  | 17. Akasema: Mola wangu Mlezi! Kwa ulivyo nineemesha,
basi mimi sitakuwa kabisa msaidizi wa wakosefu. | قَالَ رَبِّ بِمَا أَنْعَمْتَ عَلَيَّ فَلَنْ أَكُونَ ظَهِيرا ً لِلْمُجْرِمِينَ |
Fa'aşbaĥa Fī Al-Madīnati Khā'ifāan Yataraqqabu Fa'idhā Al-Ladhī Astanşarahu Bil-'Amsi Yastaşrikhuhu Qāla Lahu Mūsá 'Innaka Laghawīyun Mubīnun  | 18. Akapambazukiwa mjini asubuhi naye ana khofu,
akiangalia huku na huku. Mara yule yule aliye mtaka msaada jana akawa anampigia
kelele amsaidie. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mgomvi kweli kweli. | فَأَصْبَحَ فِي الْمَدِينَةِ خَائِفا ً يَتَرَقَّبُ فَإِذَا الَّذِي اسْتَنصَرَه ُُ بِالأَمْسِ يَسْتَصْرِخُه ُُ قَالَ لَه ُُ مُوسَى إِنَّكَ لَغَوِيّ ٌ مُبِين ٌ |
Falammā 'An 'Arāda 'An Yabţisha Bial-Ladhī Huwa `Adūwun Lahumā Qāla Yā Mūsá 'Aturīdu 'An Taqtulanī Kamā Qatalta Nafsāan Bil-'Amsi 'In Turīdu 'Illā 'An Takūna Jabbārāan Fī Al-'Arđi Wa Mā Turīdu 'An Takūna Mina Al-Muşliĥīna  | 19. Basi alipo taka kumshika kwa nguvu yule aliye
adui wao wote wawili, akasema: Ewe Musa! Unataka kuniuwa kama ulivyo muuwa
mtu jana? Wewe hutaki ila kuwa jabari katika nchi, wala hutaki kuwa miongoni
mwa wenye maslaha.. | فَلَمَّا أَنْ أَرَادَ أَنْ يَبْطِشَ بِالَّذِي هُوَ عَدُوّ ٌ لَهُمَا قَالَ يَامُوسَى أَتُرِيدُ أَنْ تَقْتُلَنِي كَمَا قَتَلْتَ نَفْسا ً بِالأَمْسِ إِنْ تُرِيدُ إِلاَّ أَنْ تَكُونَ جَبَّارا ً فِي الأَرْضِ وَمَا تُرِيدُ أَنْ تَكُونَ مِنَ الْمُصْلِحِينَ |
Wa Jā'a Rajulun Min 'Aqşá Al-Madīnati Yas`á Qāla Yā Mūsá 'Inna Al-Mala'a Ya'tamirūna Bika Liyaqtulūka Fākhruj 'Innī Laka Mina An-Nāşiĥīna  | 20. Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akipiga
mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanashauriana kukuuwa. Basi toka! Hakika
mimi ni katika wanao kupa nasaha. | وَجَاءَ رَجُل ٌ مِنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ يَسْعَى قَالَ يَامُوسَى إِنَّ الْمَلَأَ يَأْتَمِرُونَ بِكَ لِيَقْتُلُوكَ فَاخْرُجْ إِنِّي لَكَ مِنَ النَّاصِحِينَ |
Fakharaja Minhā Khā'ifāan Yataraqqabu Qāla Rabbi Najjinī Mina Al-Qawmi Až-Žālimīna  | 21. Basi akatoka, naye ana khofu, akiangalia
huku na huku. Akasema: Mola wangu Mlezi! Niokoe na watu madhaalimu. | فَخَرَجَ مِنْهَا خَائِفا ً يَتَرَقَّبُ قَالَ رَبِّ نَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ |
Wa Lammā Tawajjaha Tilqā'a Madyana Qāla `Asá Rabbī 'An Yahdiyanī Sawā'a As-Sabīl  | 22. Na alipo elekea upande wa Madyana alisema:
Asaa Mola wangu Mlezi akaniongoa njia iliyo sawa. | وَلَمَّا تَوَجَّه ََ تِلْقَاءَ مَدْيَنَ قَالَ عَسَى رَبِّي أَنْ يَهْدِيَنِي سَوَاءَ السَّبِيل |
Wa Lammā Warada Mā'a Madyana Wajada `Alayhi 'Ummatan Mina An-Nāsi Yasqūna Wa Wajada Min Dūnihimu Amra'tayni Tadhūdāni Qāla Mā Khaţbukumā Qālatā Lā Nasqī Ĥattá Yuşdira Ar-Ri`ā'u Wa 'Abūnā Shaykhun Kabīrun  | 23. Na alipo yafikia maji ya Madyana alikuta
umati wa watu wananywesha (wanyama wao), na akakuta karibu yao wanawake
wawili wanawazuia wanyama wao. Akasema: Mna nini? Wakasema: Hatunyweshi
sisi mpaka wamalize hao wachunga. Na baba yetu ni mzee sana. | وَلَمَّا وَرَدَ مَاءَ مَدْيَنَ وَجَدَ عَلَيْهِ أُمَّة ً مِنَ النَّاسِ يَسْقُونَ وَوَجَدَ مِنْ دُونِهِمُ امْرَأتَيْنِ تَذُودَانِ قَالَ مَا خَطْبُكُمَا قَالَتَا لاَ نَسْقِي حَتَّى يُصْدِرَ الرِّعَاءُ وَأَبُونَا شَيْخ ٌ كَبِير ٌ |
Fasaqá Lahumā Thumma Tawallá 'Ilá Až-Žilli Faqāla Rabbi 'Innī Limā 'Anzalta 'Ilayya Min Khayrin Faqīrun  | 24. Basi Musa akawanyweshea; kisha akarudi kivulini,
na akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika mimi ni mhitaji wa kheri utakayo niteremshia. | فَسَقَى لَهُمَا ثُمَّ تَوَلَّى إِلَى الظِّلِّ فَقَالَ رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْر ٍ فَقِير ٌ |
Fajā'at/hu 'Iĥdāhumā Tamshī `Alá Astiĥyā'in Qālat 'Inna 'Abī Yad`ūka Liyajziyaka 'Ajra Mā Saqayta Lanā Falammā Jā'ahu Wa Qaşşa `Alayhi Al-Qaşaşa Qāla Lā Takhaf Najawta Mina Al-Qawmi Až-Žālimīna  | 25. Basi mmoja katika wale wanawake wawili akamjia,
naye anaona haya. Akasema: Baba yangu anakwita akulipe ujira wa kutunyweshea.
Basi alipo mjia na akamsimulia visa vyake, alisema: Usiogope; umekwisha
okoka kwenye watu madhaalimu. | فَجَاءَتْهُ إِحْدَاهُمَا تَمْشِي عَلَى اسْتِحْيَاء ٍ قَالَتْ إِنَّ أَبِي يَدْعُوكَ لِيَجْزِيَكَ أَجْرَ مَا سَقَيْتَ لَنَا فَلَمَّا جَاءَه ُُ وَقَصَّ عَلَيْهِ الْقَصَصَ قَالَ لاَ تَخَفْ نَجَوْتَ مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ |
Qālat 'Iĥdāhumā Yā 'Abati Asta'jirhu 'Inna Khayra Mani Asta'jarta Al-Qawīyu Al-'Amīnu  | 26. Akasema mmoja katika wale wanawake: Ewe baba
yetu! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumuajiri ni mwenye nguvu na muaminifu. | قَالَتْ إِحْدَاهُمَا يَاأَبَتِ اسْتَأْجِرْهُ إِنَّ خَيْرَ مَنِ اسْتَأْجَرْتَ الْقَوِيُّ الأَمِينُ |
Qāla 'Innī 'Urīdu 'An 'Unkiĥaka 'Iĥdá Abnatayya Hātayni `Alá 'An Ta'juranī Thamāniyata Ĥijajin Fa'in 'Atmamta `Ashrāan Famin `Indika Wa Mā 'Urīdu 'An 'Ashuqqa `Alayka Satajidunī 'In Shā'a Allāhu Mina Aş-Şāliĥīna  | 27. Akasema: Mimi nataka kukuoza mmojawapo katika
binti zangu hawa wawili kwa kunitumikia miaka minane. Ukitimiza kumi, khiari
yako; lakini mimi sitaki kukutaabisha. Inshallah utanikuta miongoni mwa
watu wema. | قَالَ إِنِّي أُرِيدُ أَنْ أُنكِحَكَ إِحْدَى ابْنَتَيَّ هَاتَيْنِ عَلَى أَنْ تَأْجُرَنِي ثَمَانِيَةَ حِجَج ٍ فَإِنْ أَتْمَمْتَ عَشْرا ً فَمِنْ عِنْدِكَ وَمَا أُرِيدُ أَنْ أَشُقَّ عَلَيْكَ سَتَجِدُنِي إِنْ شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّالِحِينَ |
Qāla Dhālika Baynī Wa Baynaka 'Ayyamā Al-'Ajalayni Qađaytu Falā `Udwāna `Alayya Wa Allāhu `Alá Mā Naqūlu Wa Kīlun  | 28. Musa akasema: Hayo yamekwisha kuwa baina
yangu na wewe. Muda mmojapo nikiumaliza sitiwi ubayani. Na Mwenyezi Mungu
ni Mlinzi juu ya haya tunayo yasema. | قَالَ ذَلِكَ بَيْنِي وَبَيْنَكَ أَيَّمَا الأَجَلَيْنِ قَضَيْتُ فَلاَ عُدْوَانَ عَلَيَّ وَاللَّهُ عَلَى مَا نَقُولُ وَكِيل ٌ |
Falammā Qađá Mūsá Al-'Ajala Wa Sāra Bi'ahlihi 'Ānasa Min Jānibi Aţ-Ţūri Nārāan Qāla Li'hlihi Amkuthū 'Innī 'Ānastu Nārāan La`allī 'Ātīkum Minhā Bikhabarin 'Aw Jadhwatin Mina An-Nāri La`allakum Taşţalūna  | 29. Basi alipo timiza muda wake na akasafiri
na ahali zake, aliona moto upande wa Mlima T'uri. Akawaambia ahali zake:
Ngojeni! Mimi nimeona moto, labda nitakuleteeni kutoka huko khabari au
kijinga cha moto ili mpate kuota moto. | فَلَمَّا قَضَى مُوسَى الأَجَلَ وَسَارَ بِأَهْلِهِ آنَسَ مِنْ جَانِبِ الطُّورِ نَارا ً قَالَ لِأهْلِهِ امْكُثُوا إِنِّي آنَسْتُ نَارا ً لَعَلِّي آتِيكُمْ مِنْهَا بِخَبَرٍ أَوْ جَذْوَة ٍ مِنَ النَّارِ لَعَلَّكُمْ تَصْطَلُونَ |
Falammā 'Atāhā Nūdī Min Shāţi'i Al-Wādī Al-'Aymani Fī Al-Buq`ati Al-Mubārakati Mina Ash-Shajarati 'An Yā Mūsá 'Innī 'Anā Allāhu Rabbu Al-`Ālamīna  | 30. Basi alipo ufikia aliitwa kutoka ng'ambo
ya bonde la kuliani katika eneo lilio barikiwa kutoka kwenye mti: Ewe Musa!
Hakika Mimi ni Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote. | فَلَمَّا أَتَاهَا نُودِي مِنْ شَاطِئِ الْوَادِي الأَيْمَنِ فِي الْبُقْعَةِ الْمُبَارَكَةِ مِنَ الشَّجَرَةِ أَنْ يَامُوسَى إِنِّي أَنَا اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ |
Wa 'An 'Alqi `Aşāka Falammā Ra'āhā Tahtazzu Ka'annahā Jānnun Wallá Mudbirāan Wa Lam Yu`aqqib Yā Mūsá 'Aqbil Wa Lā Takhaf 'Innaka Mina Al-'Āminīna  | 31. Na tupa chini fimbo yako. Basi alipo iona
ikitikisika kama nyoka, akarudi nyuma wala hakutazama. (Akaambiwa): Ewe
Musa! Njoo mbele wala usiogope. Hakika wewe ni miongoni mwa walio salimika. | وَأَنْ أَلْقِ عَصَاكَ فَلَمَّا رَآهَا تَهْتَزُّ كَأَنَّهَا جَانّ ٌ وَلَّى مُدْبِرا ً وَلَمْ يُعَقِّبْ يَامُوسَى أَقْبِلْ وَلاَ تَخَفْ إِنَّكَ مِنَ الآمِنِينَ |
Asluk Yadaka Fī Jaybika Takhruj Bayđā'a Min Ghayri Sū'in Wa Ađmum 'Ilayka Janāĥaka Mina Ar-Rahbi Fadhānika Burhānāni Min Rabbika 'Ilá Fir`awna Wa Mala'ihi 'Innahum Kānū Qawmāan Fāsiqīna  | 32. Ingiza mkono wako kwenye mfuko wako, utatoka
mweupe pasipo na ubaya. Na jiambatishe mkono wako ukihisi khofu. Basi hizi
ni dalili mbili zitokazo kwa Mola wako Mlezi kumpelekea Firauni na wakuu
wa umma wake. Hakika hao walikuwa watu mafaasiki. | اسْلُكْ يَدَكَ فِي جَيْبِكَ تَخْرُجْ بَيْضَاءَ مِنْ غَيْرِ سُوء ٍ وَاضْمُمْ إِلَيْكَ جَنَاحَكَ مِنَ الرَّهْبِ فَذَانِكَ بُرْهَانَانِ مِنْ رَبِّكَ إِلَى فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ~ِ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْما ً فَاسِقِينَ |
Qāla Rabbi 'Innī Qataltu Minhum Nafsāan Fa'akhāfu 'An Yaqtulūni  | 33. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nilimuuwa
mtu katika wao, kwa hivyo naogopa wataniuwa. | قَالَ رَبِّ إِنِّي قَتَلْتُ مِنْهُمْ نَفْسا ً فَأَخَافُ أَنْ يَقْتُلُونِ |
Wa 'Akhī Hārūnu Huwa 'Afşaĥu Minnī Lisānāan Fa'arsilhu Ma`iya Rid'āan Yuşaddiqunī 'Innī 'Akhāfu 'An Yukadhdhibūni  | 34. Na ndugu yangu Harun ni fasihi zaidi ulimi
wake kuliko mimi. Basi mtume ende nami kunisaidia, ili anisadikishe. Hakika
mimi nina khofu watanikadhibisha. | وَأَخِي هَارُونُ هُوَ أَفْصَحُ مِنِّي لِسَانا ً فَأَرْسِلْهُ مَعِيَ رِدْءا ً يُصَدِّقُنِي إِنِّي أَخَافُ أَنْ يُكَذِّبُونِ |
Qāla Sanashuddu `Ađudaka Bi'akhīka Wa Naj`alu Lakumā Sulţānāan Falā Yaşilūna 'Ilaykumā Bi'āyātinā 'Antumā Wa Mani Attaba`akumā Al-Ghālibūna  | 35. (Mwenyezi Mungu) akasema: Tutautia nguvu
mkono wako kwa nduguyo, na tutakupeni madaraka, hata wasikufikilieni. Kwa
sababu ya Ishara zetu nyinyi na watakao kufuateni mtashinda. | قَالَ سَنَشُدُّ عَضُدَكَ بِأَخِيكَ وَنَجْعَلُ لَكُمَا سُلْطَانا ً فَلاَ يَصِلُونَ إِلَيْكُمَا بِآيَاتِنَا أَنْتُمَا وَمَنِ اتَّبَعَكُمَا الْغَالِبُونَ |
Falammā Jā'ahum Mūsá Bi'āyātinā Bayyinātin Qālū Mā Hādhā 'Illā Siĥrun Muftaráan Wa Mā Sami`nā Bihadhā Fī 'Ābā'inā Al-'Awwalīna  | 36. Basi alipo wafikia Musa na Ishara zetu, walisema:
Haya si chochote ila ni uchawi ulio zuliwa. Na hatukuyasikia haya kwa baba
zetu wa zamani. | فَلَمَّا جَاءَهُمْ مُوسَى بِآيَاتِنَا بَيِّنَات ٍ قَالُوا مَا هَذَا إِلاَّ سِحْر ٌ مُفْتَرى ً وَمَا سَمِعْنَا بِهَذَا فِي آبَائِنَا الأَوَّلِينَ |
Wa Qāla Mūsá Rabbī 'A`lamu Biman Jā'a Bil-Hudá Min `Indihi Wa Man Takūnu Lahu `Āqibatu Ad-Dāri 'Innahu Lā Yufliĥu Až-Žālimūna  | 37. Na Musa akasema: Mola wangu Mlezi ni Mwenye
kujua kabisa nani anaye kuja na uwongofu unao toka kwake, na nani atakaye
kuwa na mwisho mwema wa makaazi. Hakika wenye kudhulumu hawatafanikiwa. | وَقَالَ مُوسَى رَبِّي أَعْلَمُ بِمَنْ جَاءَ بِالْهُدَى مِنْ عِنْدِه ِِ وَمَنْ تَكُونُ لَه ُُ عَاقِبَةُ الدَّارِ إِنَّهُ لاَ يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ |
Wa Qāla Fir`awnu Yā 'Ayyuhā Al-Mala'u Mā `Alimtu Lakum Min 'Ilahin Ghayrī Fa'awqid Lī Yā Hāmānu `Alá Aţ-Ţīni Fāj`al Lī Şarĥāan La`allī 'Aţţali`u 'Ilá 'Ilahi Mūsá Wa 'Innī La'ažunnuhu Mina Al-Kādhibīna  | 38. Na Firauni akasema: Enyi waheshimiwa! Sijui
kama mnaye mungu asiye kuwa mimi. Ewe Haman! Niwashie moto unichomee udongo,
unijengee mnara nipate kumchungulia mungu wa Musa. Na hakika mimi namwona
yeye ni katika waongo. | وَقَالَ فِرْعَوْنُ يَاأَيُّهَا الْمَلَأُ مَا عَلِمْتُ لَكُمْ مِنْ إِلَه ٍٍ غَيْرِي فَأَوْقِدْ لِي يَاهَامَانُ عَلَى الطِّينِ فَاجْعَل لِي صَرْحا ً لَعَلِّي أَطَّلِعُ إِلَى إِلَه ِِ مُوسَى وَإِنِّي لَأَظُنُّه ُُ مِنَ الْكَاذِبِينَ |
Wa Astakbara Huwa Wa Junūduhu Fī Al-'Arđi Bighayri Al-Ĥaqqi Wa Žannū 'Annahum 'Ilaynā Lā Yurja`ūna  | 39. Na alipanda kiburi yeye na majeshi yake katika
nchi bila ya haki, na wakadhania kuwa hawatarudishwa kwetu. | وَاسْتَكْبَرَ هُوَ وَجُنُودُه ُُ فِي الأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَظَنُّوا أَنَّهُمْ إِلَيْنَا لاَ يُرْجَعُونَ |
Fa'akhadhnāhu Wa Junūdahu Fanabadhnāhum Fī Al-Yammi Fānžur Kayfa Kāna `Āqibatu Až-Žālimīna  | 40. Basi tukamshika yeye na majeshi yake, na
tukawatupa baharini. Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa wenye kudhulumu? | فَأَخَذْنَاه ُُ وَجُنُودَه ُُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الظَّالِمِينَ |
Wa Ja`alnāhum 'A'immatan Yad`ūna 'Ilá An-Nāri Wa Yawma Al-Qiyāmati Lā Yunşarūna  | 41. Na tuliwafanya ni waongozi waitao kwenye
Moto. Na Siku ya Kiyama hawatanusuriwa. | وَجَعَلْنَاهُمْ أَئِمَّة ً يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ لاَ يُنصَرُونَ |
Wa 'Atba`nāhum Fī Hadhihi Ad-Dunyā La`natan Wa Yawma Al-Qiyāmati Hum Mina Al-Maqbūĥīna  | 42. Na tukawafuatishia laana katika dunia hii,
na Siku ya Kiyama watakuwa miongoni mwa wanao chusha. | وَأَتْبَعْنَاهُمْ فِي هَذِهِ الدُّنْيَا لَعْنَة ً وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ هُمْ مِنَ الْمَقْبُوحِينَ |
Wa Laqad 'Ātaynā Mūsá Al-Kitāba Min Ba`di Mā 'Ahlaknā Al-Qurūna Al-'Ūlá Başā'ira Lilnnāsi Wa Hudáan Wa Raĥmatan La`allahum Yatadhakkarūna  | 43. Na hakika bila ya shaka tulimpa Musa Kitabu
baada ya kwisha ziangamiza kaumu za mwanzo, ili kiwafumbue macho watu,
na kiwe uwongofu, na rehema, ili wapate kukumbuka. | وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ مِنْ بَعْدِ مَا أَهْلَكْنَا الْقُرُونَ الأُولَى بَصَائِرَ لِلنَّاسِ وَهُدى ً وَرَحْمَة ً لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ |
Wa Mā Kunta Bijānibi Al-Gharbīyi 'Idh Qađaynā 'Ilá Mūsá Al-'Amra Wa Mā Kunta Mina Ash-Shāhidīn  | 44. Wala wewe hukuwa upande wa magharibi tulipo
mpa Musa amri, wala hukuwa katika walio hudhuria. | وَمَا كُنتَ بِجَانِبِ الْغَرْبِيِّ إِذْ قَضَيْنَا إِلَى مُوسَى الأَمْرَ وَمَا كُنتَ مِنَ الشَّاهِدِين |
Wa Lakinnā 'Ansha'nā Qurūnāan Fataţāwala `Alayhimu Al-`Umuru Wa Mā Kunta Thāwīāan Fī 'Ahli Madyana Tatlū `Alayhim 'Āyātinā Wa Lakinnā Kunnā Mursilīna  | 45. Lakini Sisi tuliziumba kaumu, na ukawa mrefu
umri juu yao. Wala hukuwa mkaazi na watu wa Madyana ukiwasomea Aya zetu.
Lakini ni Sisi tulio kuwa tukiwatuma Mitume. | وَلَكِنَّا أَنشَأْنَا قُرُونا ً فَتَطَاوَلَ عَلَيْهِمُ الْعُمُرُ وَمَا كُنتَ ثَاوِيا ً فِي أَهْلِ مَدْيَنَ تَتْلُوا عَلَيْهِمْ آيَاتِنَا وَلَكِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ |
Wa Mā Kunta Bijānibi Aţ-Ţūri 'Idh Nādaynā Wa Lakin Raĥmatan Min Rabbika Litundhira Qawmāan Mā 'Atāhum Min Nadhīrin Min Qablika La`allahum Yatadhakkarūna  | 46. Wala hukuwa kando ya mlima tulipo nadi. Lakini
ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi ili uwaonye watu wasio pata kufikiwa
na mwonyaji kabla yako, huenda wakakumbuka. | وَمَا كُنتَ بِجَانِبِ الطُّورِ إِذْ نَادَيْنَا وَلَكِنْ رَحْمَة ً مِنْ رَبِّكَ لِتُنذِرَ قَوْما ً مَا أَتَاهُمْ مِنْ نَذِير ٍ مِنْ قَبْلِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ |
Wa Lawlā 'An Tuşībahum Muşībatun Bimā Qaddamat 'Aydīhim Fayaqūlū Rabbanā Lawlā 'Arsalta 'Ilaynā Rasūlāan Fanattabi`a 'Āyātika Wa Nakūna Mina Al-Mu'uminīna  | 47. Na usije kuwasibu msiba kwa iliyo yatanguliza
mikono yao, wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Mbona hukututumia Mtume nasi,
tukafuata Ishara zako, na tukawa miongoni mwa Waumini? | وَلَوْلاَ أَنْ تُصِيبَهُمْ مُصِيبَة ٌ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ فَيَقُولُوا رَبَّنَا لَوْلاَ أَرْسَلْتَ إِلَيْنَا رَسُولا ً فَنَتَّبِعَ آيَاتِكَ وَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ |
Falammā Jā'ahumu Al-Ĥaqqu Min `Indinā Qālū Lawlā 'Ūtiya Mithla Mā 'Ūtiya Mūsá 'Awalam Yakfurū Bimā 'Ūtiya Mūsá Min Qablu Qālū Siĥrāni Tažāharā Wa Qālū 'Innā Bikullin Kāfirūna  | 48. Ilipo wajia Haki kutoka kwetu walisema: Mbona
hakupewa kama aliyo pewa Musa? Je! Kwani wao hawakuyakataa aliyo pewa Musa
zamani? Walisema: Ni wachawi wawili wanasaidiana. Na wakasema: Hakika sisi
tunawakataa wote. | فَلَمَّا جَاءَهُمُ الْحَقُّ مِنْ عِنْدِنَا قَالُوا لَوْلاَ أُوتِيَ مِثْلَ مَا أُوتِيَ مُوسَى أَوَلَمْ يَكْفُرُوا بِمَا أُوتِيَ مُوسَى مِنْ قَبْلُ قَالُوا سِحْرَانِ تَظَاهَرَا وَقَالُوا إِنَّا بِكُلّ ٍ كَافِرُونَ |
Qul Fa'tū Bikitābin Min `Indi Allāhi Huwa 'Ahdá Minhumā 'Attabi`hu 'In Kuntum Şādiqīna  | 49. Sema: Basi leteni Kitabu kinacho toka kwa
Mwenyezi Mungu chenye kuongoka zaidi kuliko hivi viwili tukifuate, kama
nyinyi mnasema kweli. | قُلْ فَأْتُوا بِكِتَاب ٍ مِنْ عِنْدِ اللَّهِ هُوَ أَهْدَى مِنْهُمَا أَتَّبِعْهُ إِنْ كُنتُمْ صَادِقِينَ |
Fa'in Lam Yastajībū Laka Fā`lam 'Annamā Yattabi`ūna 'Ahwā'ahum Wa Man 'Ađallu Mimmani Attaba`a Hawāhu Bighayri Hudáan Mina Allāhi 'Inna Allāha Lā Yahdī Al-Qawma Až-Žālimīna  | 50. Na ikiwa hawakuitikii, basi jua kuwa wanafuata
pumbao lao tu. Na nani aliye potea zaidi kumshinda anaye fuata pumbao lake
bila ya uwongofu utokao kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi
watu wenye kudhulumu. | فَإِنْ لَمْ يَسْتَجِيبُوا لَكَ فَاعْلَمْ أَنَّمَا يَتَّبِعُونَ أَهْوَاءَهُمْ وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّنِ اتَّبَعَ هَوَاه ُُ بِغَيْرِ هُدى ً مِنَ اللَّهِ إِنَّ اللَّهَ لاَ يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ |
Wa Laqad Waşşalnā Lahumu Al-Qawla La`allahum Yatadhakkarūna  | 51. Na sasa kwa yakini tumewafikishia Neno ili
wapate kukumbuka. | وَلَقَدْ وَصَّلْنَا لَهُمُ الْقَوْلَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ |
Al-Ladhīna 'Ātaynāhumu Al-Kitāba Min Qablihi Hum Bihi Yu'uminūna  | 52. Wale tulio wapa Kitabu kabla yake wanakiamini
hiki. | الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ مِنْ قَبْلِه ِِ هُمْ بِه ِِ يُؤْمِنُونَ |
Wa 'Idhā Yutlá `Alayhim Qālū 'Āmannā Bihi 'Innahu Al-Ĥaqqu Min Rabbinā 'Innā Kunnā Min Qablihi Muslimīna  | 53. Na wanapo somewa wanasema: Tunaiamini. Hakika
hii ni Haki inayo toka kwa Mola wetu Mlezi. Hakika sisi kabla yake tulikuwa
ni Waislamu, tulio nyenyekea. | وَإِذَا يُتْلَى عَلَيْهِمْ قَالُوا آمَنَّا بِهِ~ِ إِنَّهُ الْحَقُّ مِنْ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا مِنْ قَبْلِه ِِ مُسْلِمِينَ |
'Ūlā'ika Yu'utawna 'Ajrahum Marratayni Bimā Şabarū Wa Yadra'ūna Bil-Ĥasanati As-Sayyi'ata Wa Mimmā Razaqnāhum Yunfiqūna  | 54. Basi hao watapewa ujira wao mara mbili kwa
walivyo vumilia, na wakaondoa ubaya kwa wema, na wakatoa katika tuliyo
waruzuku. | أُوْلَائِكَ يُؤْتَوْنَ أَجْرَهُمْ مَرَّتَيْنِ بِمَا صَبَرُوا وَيَدْرَءُونَ بِالْحَسَنَةِ السَّيِّئَةَ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ |
Wa 'Idhā Sami`ū Al-Laghwa 'A`rađū `Anhu Wa Qālū Lanā 'A`mālunā Wa Lakum 'A`mālukum Salāmun `Alaykum Lā Nabtaghī Al-Jāhilīna  | 55. Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema:
Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum,
Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga. | وَإِذَا سَمِعُوا اللَّغْوَ أَعْرَضُوا عَنْهُ وَقَالُوا لَنَا أَعْمَالُنَا وَلَكُمْ أَعْمَالُكُمْ سَلاَمٌ عَلَيْكُمْ لاَ نَبْتَغِي الْجَاهِلِينَ |
'Innaka Lā Tahdī Man 'Aĥbabta Wa Lakinna Allāha Yahdī Man Yashā'u Wa Huwa 'A`lamu Bil-Muhtadīna  | 56. Kwa hakika wewe humwongoi umpendaye, lakini
Mwenyezi Mungu humwongoa amtakaye. Na Yeye ndiye anawajua zaidi waongokao. | إِنَّكَ لاَ تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَكِنَّ اللَّهَ يَهْدِي مَنْ يَشَاءُ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ |
Wa Qālū 'In Nattabi`i Al-Hudá Ma`aka Nutakhaţţaf Min 'Arđinā 'Awalam Numakkin Lahum Ĥaramāan 'Āmināan Yujbá 'Ilayhi Thamarātu Kulli Shay'in Rizqāan Min Ladunnā Wa Lakinna 'Aktharahum Lā Ya`lamūna  | 57. Na wakasema: Tukiufuata uwongofu huu pamoja
nawe tutanyakuliwa kutoka nchi yetu. Je! Kwani Sisi hatukuwaweka imara
katika pahala patakatifu, penye amani, ambapo huletewa matunda ya kila
aina kuwa ni riziki itokayo kwetu? Lakini wengi wao hawajui. | وَقَالُوا إِنْ نَتَّبِعِ الْهُدَى مَعَكَ نُتَخَطَّفْ مِنْ أَرْضِنَا أَوَلَمْ نُمَكِّنْ لَهُمْ حَرَما ً آمِنا ً يُجْبَى إِلَيْهِ ثَمَرَاتُ كُلِّ شَيْء ٍ رِزْقا ً مِنْ لَدُنَّا وَلَكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ |
Wa Kam 'Ahlaknā Min Qaryatin Baţirat Ma`īshatahā Fatilka Masākinuhum Lam Tuskan Min Ba`dihim 'Illā Qalīlāan Wa Kunnā Naĥnu Al-Wārithīna  | 58. Na miji mingapi iliyo jifakharisha tumeiangamiza!
Na hayo maskani yao hayakukaliwa tena baada yao, ila kwa uchache tu. Na
Sisi ndio tumekuwa warithi wao. | وَكَمْ أَهْلَكْنَا مِنْ قَرْيَة ٍ بَطِرَتْ مَعِيشَتَهَا فَتِلْكَ مَسَاكِنُهُمْ لَمْ تُسْكَنْ مِنْ بَعْدِهِمْ إِلاَّ قَلِيلا ً وَكُنَّا نَحْنُ الْوَارِثِينَ |
Wa Mā Kāna Rabbuka Muhlika Al-Qurá Ĥattá Yab`atha Fī 'Ummihā Rasūlāan Yatlū `Alayhim 'Āyātinā Wa Mā Kunnā Muhlikī Al-Qurá 'Illā Wa 'Ahluhā Žālimūna  | 59. Na Mola wako Mlezi haangamizi miji mpaka
ampeleke Mtume katika miji yake mikuu awasomee Ishara zetu. Wala hatuiangamizi
miji mpaka watu wake wawe madhaalimu. | وَمَا كَانَ رَبُّكَ مُهْلِكَ الْقُرَى حَتَّى يَبْعَثَ فِي أُمِّهَا رَسُولا ً يَتْلُوا عَلَيْهِمْ آيَاتِنَا وَمَا كُنَّا مُهْلِكِي الْقُرَى إِلاَّ وَأَهْلُهَا ظَالِمُونَ |
Wa Mā 'Ūtītum Min Shay'in Famatā`u Al-Ĥayāati Ad-Dunyā Wa Zīnatuhā Wa Mā `Inda Allāhi Khayrun Wa 'Abqá 'Afalā Ta`qilūna  | 60. Na chochote mlicho pewa ni matumizi ya maisha
ya dunia na pambo lake. Na yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ndio bora na yatakayo
baki zaidi. Basi je, hamfahamu? | وَمَا أُوتِيتُمْ مِنْ شَيْء ٍ فَمَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَزِينَتُهَا وَمَا عِنْدَ اللَّهِ خَيْر ٌ وَأَبْقَى أَفَلاَ تَعْقِلُونَ |
'Afaman Wa`adnāhu Wa`dāan Ĥasanāan Fahuwa Lāqīhi Kaman Matta`nāhu Matā`a Al-Ĥayāati Ad-Dunyā Thumma Huwa Yawma Al-Qiyāmati Mina Al-Muĥđarīna  | 61. Je! Yule tuliye muahidi ahadi nzuri, tena
naye akayapata, ni kama tuliye mstarehesha kwa starehe za maisha ya duniani,
na kisha Siku ya Kiyama akawa miongoni mwa wanao hudhurishwa? | أَفَمَنْ وَعَدْنَاه ُُ وَعْداً حَسَنا ً فَهُوَ لاَقِيه ِِ كَمَنْ مَتَّعْنَاه ُُ مَتَاعَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ثُمَّ هُوَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ مِنَ الْمُحْضَرِينَ |
Wa Yawma Yunādīhim Fayaqūlu 'Ayna Shurakā'iya Al-Ladhīna Kuntum Taz`umūna  | 62. Na siku atakapo waita na akasema: Wako wapi
mlio kuwa mkidai kuwa ni washirika wangu? | وَيَوْمَ يُنَادِيهِمْ فَيَقُولُ أَيْنَ شُرَكَائِيَ الَّذِينَ كُنتُمْ تَزْعُمُونَ |
Qāla Al-Ladhīna Ĥaqqa `Alayhimu Al-Qawlu Rabbanā Hā'uulā' Al-Ladhīna 'Aghwaynā 'Aghwaynāhum Kamā Ghawaynā Tabarra'nā 'Ilayka Mā Kānū 'Īyānā Ya`budūna  | 63. Watasema wale iliyo thibiti juu yao kauli:
Mola wetu Mlezi! Hawa ndio tulio wapoteza. Tuliwapoteza kama tulivyo potea
sisi. Tunajitenga nao mbele yako. Hawakuwa wakituabudu sisi. | قَالَ الَّذِينَ حَقَّ عَلَيْهِمُ الْقَوْلُ رَبَّنَا هَاؤُلاَء الَّذِينَ أَغْوَيْنَا أَغْوَيْنَاهُمْ كَمَا غَوَيْنَا تَبَرَّأْنَا إِلَيْكَ مَا كَانُوا إِيَّانَا يَعْبُدُونَ |
Wa Qīla Ad`ū Shurakā'akum Fada`awhum Falam Yastajībū Lahum Wa Ra'aw Al-`Adhāba Law 'Annahum Kānū Yahtadūna  | 64. Na itasemwa: Waiteni hao miungu wa kishirikina
wenu! Basi watawaita, lakini hawatawaitikia, na wataiona adhabu; laiti
wangeli kuwa wameongoka! | وَقِيلَ ادْعُوا شُرَكَاءَكُمْ فَدَعَ |