44) Sūrat Ad-Dukhān | Printed format | 44) سُورَة الدُّخَان |
| Ĥā-Mīm | 1. H'a Mim | حَا-مِيم |
| Wa Al-Kitābi Al-Mubīni | 2. Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha, | وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ |
| 'Innā 'Anzalnāhu Fī Laylatin Mubārakatin 'Innā Kunnā Mundhirīna | 3. Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji. | إِنَّا أَنزَلْنَاه ُُ فِي لَيْلَة ٍ مُبَارَكَة ٍ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ |
| Fīhā Yufraqu Kullu 'Amrin Ĥakīmin | 4. Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima, | فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيم ٍ |
| 'Amrāan Min `Indinā 'Innā Kunnā Mursilīna | 5. Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma. | أَمْرا ً مِنْ عِنْدِنَا إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ |
| Raĥmatan Min Rabbika 'Innahu Huwa As-Samī`u Al-`Alīmu | 6. Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua. | رَحْمَة ً مِنْ رَبِّكَ إِنَّه ُُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ |
| Rabbi As-Samāwāti Wa Al-'Arđi Wa Mā Baynahumā 'In Kuntum Mūqinīna | 7. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini. | رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا إِنْ كُنْتُمْ مُوقِنِينَ |
| Lā 'Ilāha 'Illā Huwa Yuĥyī Wa Yumītu Rabbukum Wa Rabbu 'Ābā'ikumu Al-'Awwalīna | 8. Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo. | لاَ إِلَهَ~َ إِلاَّ هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الأَوَّلِينَ |
| Bal Hum Fī Shakkin Yal`abūna | 9. Lakini wao wanacheza katika shaka. | بَلْ هُمْ فِي شَكّ ٍ يَلْعَبُونَ |
| Fārtaqib Yawma Ta'tī As-Samā'u Bidukhānin Mubīnin | 10. Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri, | فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَان ٍ مُبِين ٍ |
| Yaghshá An-Nāsa Hādhā `Adhābun 'Alīmun | 11. Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu! | يَغْشَى النَّاسَ هَذَا عَذَابٌ أَلِيم ٌ |
| Rabbanā Akshif `Annā Al-`Adhāba 'Innā Mu'uminūna | 12. Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini. | رَبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ |
| 'Anná Lahumu Adh-Dhikrá Wa Qad Jā'ahum Rasūlun Mubīnun | 13. Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha. | أَنَّى لَهُمُ الذِّكْرَى وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُول ٌ مُبِين ٌ |
| Thumma Tawallaw `Anhu Wa Qālū Mu`allamun Majnūnun | 14. Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu. | ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّم ٌ مَجْنُون ٌ |
| 'Innā Kāshifū Al-`Adhābi Qalīlāan 'Innakum `Ā'idūna | 15. Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile! | إِنَّا كَاشِفُوا الْعَذَابِ قَلِيلا ً إِنَّكُمْ عَائِدُونَ |
| Yawma Nabţishu Al-Baţshata Al-Kubrá 'Innā Muntaqimūna | 16. Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa. | يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَى إِنَّا مُنتَقِمُونَ |
| Wa Laqad Fatannā Qablahum Qawma Fir`awna Wa Jā'ahum Rasūlun Karīmun | 17. Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu. | وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُول ٌ كَرِيم ٌ |
| 'An 'Addū 'Ilayya `Ibāda Allāhi 'Innī Lakum Rasūlun 'Amīnun | 18. Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu. | أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللَّهِ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِين ٌ |
| Wa 'An Lā Ta`lū `Alá Allāhi 'Innī 'Ātīkum Bisulţānin Mubīnin | 19. Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi. | وَأَنْ لاَ تَعْلُوا عَلَى اللَّهِ إِنِّي آتِيكُمْ بِسُلْطَان ٍ مُبِين ٍ |
| Wa 'Innī `Udhtu Birabbī Wa Rabbikum 'An Tarjumūni | 20. Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe. | وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَنْ تَرْجُمُونِ |
| Wa 'In Lam Tu'uminū Lī Fā`tazilūni | 21. Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami. | وَإِنْ لَمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ |
| Fada`ā Rabbahu 'Anna Hā'uulā' Qawmun Mujrimūna | 22. Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu. | فَدَعَا رَبَّهُ~ُ أَنَّ هَاؤُلاَء قَوْم ٌ مُجْرِمُونَ |
| Fa'asri Bi`ibādī Laylāan 'Innakum Muttaba`ūna | 23. Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa. | فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلا ً إِنَّكُمْ مُتَّبَعُونَ |
| Wa Atruki Al-Baĥra Rahwan 'Innahum Jundun Mughraqūna | 24. Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa. | وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوا ً إِنَّهُمْ جُند ٌ مُغْرَقُونَ |
| Kam Tarakū Min Jannātin Wa `Uyūnin | 25. Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha! | كَمْ تَرَكُوا مِنْ جَنَّات ٍ وَعُيُون ٍ |
| Wa Zurū`in Wa Maqāmin Karīmin | 26. Na mimea na vyeo vitukufu! | وَزُرُوع ٍ وَمَقَام ٍ كَرِيم ٍ |
| Wa Na`matin Kānū Fīhā Fākihīna | 27. Na neema walizo kuwa wakijistareheshea! | وَنَعْمَة ٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ |
| Kadhālika Wa 'Awrathnāhā Qawmāan 'Ākharīna | 28. Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe. | كَذَلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْما ً آخَرِينَ |
| Famā Bakat `Alayhimu As-Samā'u Wa Al-'Arđu Wa Mā Kānū Munžarīna | 29. La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula. | فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ |
| Wa Laqad Najjaynā Banī 'Isrā'īla Mina Al-`Adhābi Al-Muhīni | 30. Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha, | وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ |
| Min Fir`awna 'Innahu Kāna `Ālīāan Mina Al-Musrifīna | 31. Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka. | مِنْ فِرْعَوْنَ إِنَّه ُُ كَانَ عَالِيا ً مِنَ الْمُسْرِفِينَ |
| Wa Laqadi Akhtarnāhum `Alá `Ilmin `Alá Al-`Ālamīna | 32. Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe. | وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَى عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ |
| Wa 'Ātaynāhum Mina Al-'Āyāti Mā Fīhi Balā'un Mubīnun | 33. Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi. | وَآتَيْنَاهُمْ مِنَ الآيَاتِ مَا فِيه ِِ بَلاَء ٌ مُبِين ٌ |
| 'Inna Hā'uulā' Layaqūlūna | 34. Hakika hawa wanasema: | إِنَّ هَاؤُلاَء لَيَقُولُونَ |
| 'In Hiya 'Illā Mawtatunā Al-'Ūlá Wa Mā Naĥnu Bimunsharīna | 35. Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi. | إِنْ هِيَ إِلاَّ مَوْتَتُنَا الأُولَى وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ |
| Fa'tū Bi'ābā'inā 'In Kuntum Şādiqīna | 36. Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli. | فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِنْ كُنتُمْ صَادِقِينَ |
| 'Ahum Khayrun 'Am Qawmu Tubba`in Wa Al-Ladhīna Min Qablihim 'Ahlaknāhum 'Innahum Kānū Mujrimīna | 37. Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu. | أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّع ٍ وَالَّذِينَ مِنْ قَبْلِهِمْ أَهْلَكْنَاهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ |
| Wa Mā Khalaqnā As-Samāwāti Wa Al-'Arđa Wa Mā Baynahumā Lā`ibīna | 38. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo. | وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لاَعِبِينَ |
| Mā Khalaqnāhumā 'Illā Bil-Ĥaqqi Wa Lakinna 'Aktharahum Lā Ya`lamūna | 39. Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui. | مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلاَّ بِالْحَقِّ وَلَكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ |
| 'Inna Yawma Al-Faşli Mīqātuhum 'Ajma`īna | 40. Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote. | إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ |
| Yawma Lā Yughnī Mawláan `An Mawláan Shay'āan Wa Lā Hum Yunşarūna | 41. Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa. | يَوْمَ لاَ يُغْنِي مَوْلىً عَنْ مَوْلى ً شَيْئا ً وَلاَ هُمْ يُنصَرُونَ |
| 'Illā Man Raĥima Allāhu 'Innahu Huwa Al-`Azīzu Ar-Raĥīmu | 42. Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. | إِلاَّ مَنْ رَحِمَ اللَّهُ إِنَّه ُُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ |
| 'Inna Shajarata Az-Zaqqūmi | 43. Hakika Mti wa Zaqqum, | إِنَّ شَجَرَةَ الزَّقُّومِ |
| Ţa`āmu Al-'Athīmi | 44. Ni chakula cha mwenye dhambi. | طَعَامُ الأَثِيمِ |
| Kālmuhli Yaghlī Fī Al-Buţūni | 45. Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni | كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ |
| Kaghalyi Al-Ĥamīmi | 46. Kama kutokota kwa maji ya moto. | كَغَلْيِ الْحَمِيمِ |
| Khudhūhu Fā`tilūhu 'Ilá Sawā'i Al-Jaĥīmi | 47. (Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu! | خُذُوه ُُ فَاعْتِلُوهُ~ُ إِلَى سَوَاءِ الْجَحِيمِ |
| Thumma Şubbū Fawqa Ra'sihi Min `Adhābi Al-Ĥamīmi | 48. Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka. | ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِه ِِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ |
| Dhuq 'Innaka 'Anta Al-`Azīzu Al-Karīmu | 49. Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu! | ذُقْ إِنَّكَ أَنْتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ |
| 'Inna Hādhā Mā Kuntum Bihi Tamtarūna | 50. Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka. | إِنَّ هَذَا مَا كُنتُمْ بِه ِِ تَمْتَرُونَ |
| 'Inna Al-Muttaqīna Fī Maqāmin 'Amīnin | 51. Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani, | إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِين ٍ |
| Fī Jannātin Wa `Uyūnin | 52. Katika mabustani na chemchem, | فِي جَنَّات ٍ وَعُيُون ٍ |
| Yalbasūna Min Sundusin Wa 'Istabraqin Mutaqābilīna | 53. Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana, | يَلْبَسُونَ مِنْ سُندُس ٍ وَإِسْتَبْرَق ٍ مُتَقَابِلِينَ |
| Kadhālika Wa Zawwajnāhum Biĥūrin `Īnin | 54. Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini. | كَذَلِكَ وَزَوَّجْنَاهُمْ بِحُورٍ عِين ٍ |
| Yad`ūna Fīhā Bikulli Fākihatin 'Āminīna | 55. Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani. | يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَة ٍ آمِنِينَ |
| Lā Yadhūqūna Fīhā Al-Mawta 'Illā Al-Mawtata Al-'Ūlá Wa Waqāhum `Adhāba Al-Jaĥīmi | 56. Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu, | لاَ يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلاَّ الْمَوْتَةَ الأُولَى وَوَقَاهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ |
| Fađlāan Min Rabbika Dhālika Huwa Al-Fawzu Al-`Ažīmu | 57. Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa. | فَضْلا ً مِنْ رَبِّكَ ذَلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ |
| Fa'innamā Yassarnāhu Bilisānika La`allahum Yatadhakkarūna | 58. Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka. | فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاه ُُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ |
| Fārtaqib 'Innahum Murtaqibūna | 59. Ngoja tu, na wao wangoje pia. * | فَارْتَقِبْ إِنَّهُمْ مُرْتَقِبُونَ |