43) Sūrat Az-Zukhruf | Printed format | 43) سُورَة الزُّخرُف |
| Ĥā-Mīm | 1. H'a Mim | حَا-مِيم |
| Wa Al-Kitābi Al-Mubīni | 2. Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha. | وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ |
| 'Innā Ja`alnāhu Qur'ānāan `Arabīyāan La`allakum Ta`qilūna | 3. Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu. | إِنَّا جَعَلْنَاه ُُ قُرْآناً عَرَبِيّا ً لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ |
| Wa 'Innahu Fī 'Ummi Al-Kitābi Ladaynā La`alīyun Ĥakīmun | 4. Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima. | وَإِنَّه ُُ فِي أُمِّ الْكِتَابِ لَدَيْنَا لَعَلِيٌّ حَكِيم ٌ |
| 'Afanađribu `Ankumu Adh-Dhikra Şafĥāan 'An Kuntum Qawmāan Musrifīna | 5. Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri? | أَفَنَضْرِبُ عَنكُمُ الذِّكْرَ صَفْحاً أَنْ كُنتُمْ قَوْما ً مُسْرِفِينَ |
| Wa Kam 'Arsalnā Min Nabīyin Fī Al-'Awwalīna | 6. Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani! | وَكَمْ أَرْسَلْنَا مِنْ نَبِيّ ٍ فِي الأَوَّلِينَ |
| Wa Mā Ya'tīhim Min Nabīyin 'Illā Kānū Bihi Yastahzi'ūn | 7. Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli. | وَمَا يَأْتِيهِمْ مِنْ نَبِيّ ٍ إِلاَّ كَانُوا بِه ِِ يَسْتَهْزِئُون |
| Fa'ahlaknā 'Ashadda Minhum Baţshāan Wa Mađá Mathalu Al-'Awwalīna | 8. Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita. | فَأَهْلَكْنَا أَشَدَّ مِنْهُمْ بَطْشا ً وَمَضَى مَثَلُ الأَوَّلِينَ |
| Wa La'in Sa'altahum Man Khalaqa As-Samāwāti Wa Al-'Arđa Layaqūlunna Khalaqahunna Al-`Azīzu Al-`Alīmu | 9. Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi, | وَلَئِنْ سَأَلْتَهُمْ مَنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ لَيَقُولُنَّ خَلَقَهُنَّ الْعَزِيزُ الْعَلِيمُ |
| Al-Ladhī Ja`ala Lakumu Al-'Arđa Mahdāan Wa Ja`ala Lakum Fīhā Subulāan La`allakum Tahtadūna | 10. Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka. | الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الأَرْضَ مَهْدا ً وَجَعَلَ لَكُمْ فِيهَا سُبُلا ً لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ |
| Wa Al-Ladhī Nazzala Mina As-Samā'i Mā'an Biqadarin Fa'ansharnā Bihi Baldatan Maytāan Kadhālika Tukhrajūna | 11. Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa. | وَالَّذِي نَزَّلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاء ً بِقَدَر ٍ فَأَنشَرْنَا بِه ِِ بَلْدَة ً مَيْتا ً كَذَلِكَ تُخْرَجُونَ |
| Wa Al-Ladhī Khalaqa Al-'Azwāja Kullahā Wa Ja`ala Lakum Mina Al-Fulki Wa Al-'An`ām Mā Tarkabūna | 12. Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda. | وَالَّذِي خَلَقَ الأَزْوَاجَ كُلَّهَا وَجَعَلَ لَكُمْ مِنَ الْفُلْكِ وَالأَنعَام مَا تَرْكَبُونَ |
| Litastawū `Alá Žuhūrihi Thumma Tadhkurū Ni`mata Rabbikum 'Idhā Astawaytum `Alayhi Wa Taqūlū Subĥāna Al-Ladhī Sakhkhara Lanā Hādhā Wa Mā Kunnā Lahu Muqrinīna | 13. Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe. | لِتَسْتَوُوا عَلَى ظُهُورِه ِِ ثُمَّ تَذْكُرُوا نِعْمَةَ رَبِّكُمْ إِذَا اسْتَوَيْتُمْ عَلَيْهِ وَتَقُولُوا سُبْحانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَه ُُ مُقْرِنِينَ |
| Wa 'Innā 'Ilá Rabbinā Lamunqalibūna | 14. Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi. | وَإِنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ |
| Wa Ja`alū Lahu Min `Ibādihi Juz'āan 'Inna Al-'Insāna Lakafūrun Mubīnun | 15. Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri. | وَجَعَلُوا لَه ُُ مِنْ عِبَادِه ِِ جُزْءا ً إِنَّ الإِنسَانَ لَكَفُور ٌ مُبِين ٌ |
| 'Am Attakhadha Mimmā Yakhluqu Banātin Wa 'Aşfākum Bil-Banīna | 16. Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume? | أَمْ اتَّخَذَ مِمَّا يَخْلُقُ بَنَات ٍ وَأَصْفَاكُمْ بِالْبَنِينَ |
| Wa 'Idhā Bushshira 'Aĥaduhum Bimā Đaraba Lilrraĥmani Mathalāan Žalla Wajhuhu Muswaddāan Wa Huwa Kažīmun | 17. Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira. | وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُمْ بِمَا ضَرَبَ لِلرَّحْمَنِ مَثَلا ً ظَلَّ وَجْهُه ُُ مُسْوَدّا ً وَهُوَ كَظِيم ٌ |
| 'Awaman Yunashsha'u Fī Al-Ĥilyati Wa Huwa Fī Al-Khişāmi Ghayru Mubīnin | 18. Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...? | أَوَمَنْ يُنَشَّأُ فِي الْحِلْيَةِ وَهُوَ فِي الْخِصَامِ غَيْرُ مُبِين ٍ |
| Wa Ja`alū Al-Malā'ikata Al-Ladhīna Hum `Ibādu Ar-Raĥmāni 'Ināthāan 'Ashahidū Khalqahum Satuktabu Shahādatuhum Wa Yus'alūna | 19. Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa! | وَجَعَلُوا الْمَلاَئِكَةَ الَّذِينَ هُمْ عِبَادُ الرَّحْمَنِ إِنَاثاً أَشَهِدُوا خَلْقَهُمْ سَتُكْتَبُ شَهَادَتُهُمْ وَيُسْأَلُونَ |
| Wa Qālū Law Shā'a Ar-Raĥmānu Mā `Abadnāhum Mā Lahum Bidhālika Min `Ilmin 'In Hum 'Illā Yakhruşūna | 20. Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu! | وَقَالُوا لَوْ شَاءَ الرَّحْمَنُ مَا عَبَدْنَاهُمْ مَا لَهُمْ بِذَلِكَ مِنْ عِلْم ٍ إِنْ هُمْ إِلاَّ يَخْرُصُونَ |
| 'Am 'Ātaynāhum Kitābāan Min Qablihi Fahum Bihi Mustamsikūna | 21. Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho? | أَمْ آتَيْنَاهُمْ كِتَابا ً مِنْ قَبْلِه ِِ فَهُمْ بِه ِِ مُسْتَمْسِكُونَ |
| Bal Qālū 'Innā Wajadnā 'Ābā'anā `Alá 'Ummatin Wa 'Innā `Alá 'Āthārihim Muhtadūna | 22. Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao. | بَلْ قَالُوا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَى أُمَّة ٍ وَإِنَّا عَلَى آثَارِهِمْ مُهْتَدُونَ |
| Wa Kadhalika Mā 'Arsalnā Min Qablika Fī Qaryatin Min Nadhīrin 'Illā Qāla Mutrafūhā 'Innā Wajadnā 'Ābā'anā `Alá 'Ummatin Wa 'Innā `Alá 'Āthārihim Muqtadūna | 23. Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao. | وَكَذَلِكَ مَا أَرْسَلْنَا مِنْ قَبْلِكَ فِي قَرْيَة ٍ مِنْ نَذِير ٍ إِلاَّ قَالَ مُتْرَفُوهَا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَى أُمَّة ٍ وَإِنَّا عَلَى آثَارِهِمْ مُقْتَدُونَ |
| Qāla 'Awalaw Ji'tukum Bi'ahdá Mimmā Wajadtum `Alayhi 'Ābā'akum Qālū 'Innā Bimā 'Ursiltum Bihi Kāfirūna | 24. Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa. | قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكُمْ بِأَهْدَى مِمَّا وَجَدْتُمْ عَلَيْهِ آبَاءَكُمْ قَالُوا إِنَّا بِمَا أُرْسِلْتُمْ بِه ِِ كَافِرُونَ |
| Fāntaqamnā Minhum Fānžur Kayfa Kāna `Āqibatu Al-Mukadhdhibīna | 25. Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha! | فَانتَقَمْنَا مِنْهُمْ فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُكَذِّبِينَ |
| Wa 'Idh Qāla 'Ibrāhīmu Li'abīhi Wa Qawmihi 'Innanī Barā'un Mimmā Ta`budūna | 26. Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu, | وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيه ِِ وَقَوْمِهِ~ِ إِنَّنِي بَرَاء ٌ مِمَّا تَعْبُدُونَ |
| 'Illā Al-Ladhī Faţaranī Fa'innahu Sayahdīni | 27. Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa. | إِلاَّ الَّذِي فَطَرَنِي فَإِنَّه ُُ سَيَهْدِينِ |
| Wa Ja`alahā Kalimatan Bāqiyatan Fī `Aqibihi La`allahum Yarji`ūna | 28. Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee. | وَجَعَلَهَا كَلِمَة ً بَاقِيَة ً فِي عَقِبِه ِِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ |
| Bal Matta`tu Hā'uulā' Wa 'Ābā'ahum Ĥattá Jā'ahumu Al-Ĥaqqu Wa Rasūlun Mubīnun | 29. Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha. | بَلْ مَتَّعْتُ هَاؤُلاَء وَآبَاءَهُمْ حَتَّى جَاءَهُمُ الْحَقُّ وَرَسُول ٌ مُبِين ٌ |
| Wa Lammā Jā'ahumu Al-Ĥaqqu Qālū Hādhā Siĥrun Wa 'Innā Bihi Kāfirūna | 30. Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa. | وَلَمَّا جَاءَهُمُ الْحَقُّ قَالُوا هَذَا سِحْر ٌ وَإِنَّا بِه ِِ كَافِرُونَ |
| Wa Qālū Lawlā Nuzzila Hādhā Al-Qur'ānu `Alá Rajulin Mina Al-Qaryatayni `Ažīmin | 31. Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii? | وَقَالُوا لَوْلاَ نُزِّلَ هَذَا الْقُرْآنُ عَلَى رَجُل ٍ مِنَ الْقَرْيَتَيْنِ عَظِيم ٍ |
| 'Ahum Yaqsimūna Raĥmata Rabbika Naĥnu Qasamnā Baynahum Ma`īshatahum Fī Al-Ĥayāati Ad-Dunyā Wa Rafa`nā Ba`đahum Fawqa Ba`đin Darajātin Liyattakhidha Ba`đuhum Ba`đāan Sukhrīyāan Wa Raĥmatu Rabbika Khayrun Mimmā Yajma`ūna | 32. Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya. | أَهُمْ يَقْسِمُونَ رَحْمَةَ رَبِّكَ نَحْنُ قَسَمْنَا بَيْنَهُمْ مَعِيشَتَهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَرَفَعْنَا بَعْضَهُمْ فَوْقَ بَعْض ٍ دَرَجَات ٍ لِيَتَّخِذَ بَعْضُهُمْ بَعْضا ً سُخْرِيّا ً وَرَحْمَةُ رَبِّكَ خَيْر ٌ مِمَّا يَجْمَعُونَ |
| Wa Lawlā 'An Yakūna An-Nāsu 'Ummatan Wāĥidatan Laja`alnā Liman Yakfuru Bir-Raĥmani Libuyūtihim Suqufāan Min Fađđatin Wa Ma`ārija `Alayhā Yažharūna | 33. Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia, | وَلَوْلاَ أَنْ يَكُونَ النَّاسُ أُمَّة ً وَاحِدَة ً لَجَعَلْنَا لِمَنْ يَكْفُرُ بِالرَّحْمَنِ لِبُيُوتِهِمْ سُقُفا ً مِنْ فَضَّة ٍ وَمَعَارِجَ عَلَيْهَا يَظْهَرُونَ |
| Wa Libuyūtihim 'Abwābāan Wa Sururāan `Alayhā Yattaki'ūna | 34. Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake, | وَلِبُيُوتِهِمْ أَبْوَابا ً وَسُرُراً عَلَيْهَا يَتَّكِئُونَ |
| Wa Zukhrufāan Wa 'In Kullu Dhālika Lammā Matā`u Al-Ĥayāati Ad-Dunyā Wa Al-'Ākhiratu `Inda Rabbika Lilmuttaqīna | 35. Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu. | وَزُخْرُفا ً وَإِنْ كُلُّ ذَلِكَ لَمَّا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَالآخِرَةُ عِنْدَ رَبِّكَ لِلْمُتَّقِينَ |
| Wa Man Ya`shu `An Dhikri Ar-Raĥmāni Nuqayyiđ Lahu Shayţānāan Fahuwa Lahu Qarīnun | 36. Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake. | وَمَنْ يَعْشُ عَنْ ذِكْرِ الرَّحْمَنِ نُقَيِّضْ لَه ُُ شَيْطَانا ً فَهُوَ لَه ُُ قَرِين ٌ |
| Wa 'Innahum Layaşuddūnahum `Ani As-Sabīli Wa Yaĥsabūna 'Annahum Muhtadūna | 37. Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka. | وَإِنَّهُمْ لَيَصُدُّونَهُمْ عَنِ السَّبِيلِ وَيَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ مُهْتَدُونَ |
| Ĥattá 'Idhā Jā'anā Qāla Yā Layta Baynī Wa Baynaka Bu`da Al-Mashriqayni Fabi'sa Al-Qarīnu | 38. Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe! | حَتَّى إِذَا جَاءَنَا قَالَ يَالَيْتَ بَيْنِي وَبَيْنَكَ بُعْدَ الْمَشْرِقَيْنِ فَبِئْسَ الْقَرِينُ |
| Wa Lan Yanfa`akumu Al-Yawma 'Idh Žalamtum 'Annakum Fī Al-`Adhābi Mushtarikūna | 39. Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu. | وَلَنْ يَنفَعَكُمُ الْيَوْمَ إِذْ ظَلَمْتُمْ أَنَّكُمْ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ |
| 'Afa'anta Tusmi`u Aş-Şumma 'Aw Tahdī Al-`Umya Wa Man Kāna Fī Đalālin Mubīnin | 40. Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi? | أَفَأَنْتَ تُسْمِعُ الصُّمَّ أَوْ تَهْدِي الْعُمْيَ وَمَنْ كَانَ فِي ضَلاَل ٍ مُبِين ٍ |
| Fa'immā Nadh/habanna Bika Fa'innā Minhum Muntaqimūna | 41. Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao. | فَإِمَّا نَذْهَبَنَّ بِكَ فَإِنَّا مِنْهُمْ مُنْتَقِمُونَ |
| 'Aw Nuriyannaka Al-Ladhī Wa`adnāhum Fa'innā `Alayhim Muqtadirūna | 42. Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao. | أَوْ نُرِيَنَّكَ الَّذِي وَعَدْنَاهُمْ فَإِنَّا عَلَيْهِمْ مُقْتَدِرُونَ |
| Fāstamsik Bial-Ladhī 'Ūĥiya 'Ilayka 'Innaka `Alá Şirāţin Mustaqīmin | 43. Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka. | فَاسْتَمْسِكْ بِالَّذِي أُوحِيَ إِلَيْكَ إِنَّكَ عَلَى صِرَاط ٍ مُسْتَقِيم ٍ |
| Wa 'Innahu Ladhikrun Laka Wa Liqawmika Wa Sawfa Tus'alūna | 44. Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa. | وَإِنَّه ُُ لَذِكْر ٌ لَكَ وَلِقَوْمِكَ وَسَوْفَ تُسْأَلُونَ |
| Wa As'al Man 'Arsalnā Min Qablika Min Rusulinā 'Aja`alnā Min Dūni Ar-Raĥmāni 'Ālihatan Yu`badūna | 45. Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani? | وَاسْأَلْ مَنْ أَرْسَلْنَا مِنْ قَبْلِكَ مِنْ رُسُلِنَا أَجَعَلْنَا مِنْ دُونِ الرَّحْمَنِ آلِهَة ً يُعْبَدُونَ |
| Wa Laqad 'Arsalnā Mūsá Bi'āyātinā 'Ilá Fir`awna Wa Mala'ihi Faqāla 'Innī Rasūlu Rabbi Al-`Ālamīna | 46, Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote! | وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مُوسَى بِآيَاتِنَا إِلَى فِرْعَوْنَ وَمَلَئِه ِِ فَقَالَ إِنِّي رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ |
| Falammā Jā'ahum Bi'āyātinā 'Idhā Hum Minhā Yađĥakūna | 47. Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka. | فَلَمَّا جَاءَهُمْ بِآيَاتِنَا إِذَا هُمْ مِنْهَا يَضْحَكُونَ |
| Wa Mā Nurīhim Min 'Āyatin 'Illā Hiya 'Akbaru Min 'Ukhtihā Wa 'Akhadhnāhum Bil-`Adhābi La`allahum Yarji`ūna | 48. Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee. | وَمَا نُرِيهِمْ مِنْ آيَة ٍ إِلاَّ هِيَ أَكْبَرُ مِنْ أُخْتِهَا وَأَخَذْنَاهُمْ بِالْعَذَابِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ |
| Wa Qālū Yā 'Ayyuhā As-Sāĥiru Ad`u Lanā Rabbaka Bimā `Ahida `Indaka 'Innanā Lamuhtadūn | 49. Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka. | وَقَالُوا يَاأَيُّهَا السَّاحِرُ ادْعُ لَنَا رَبَّكَ بِمَا عَهِدَ عِنْدَكَ إِنَّنَا لَمُهْتَدُون |
| Falammā Kashafnā `Anhumu Al-`Adhāba 'Idhā Hum Yankuthūna | 50. Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi. | فَلَمَّا كَشَفْنَا عَنْهُمُ الْعَذَابَ إِذَا هُمْ يَنكُثُونَ |
| Wa Nādá Fir`awnu Fī Qawmihi Qāla Yā Qawmi 'Alaysa Lī Mulku Mişra Wa Hadhihi Al-'Anhāru Tajrī Min Taĥtī 'Afalā Tubşirūna | 51. Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni? | وَنَادَى فِرْعَوْنُ فِي قَوْمِه ِِ قَالَ يَاقَوْمِ أَلَيْسَ لِي مُلْكُ مِصْرَ وَهَذِهِ الأَنْهَارُ تَجْرِي مِنْ تَحْتِي أَفَلاَ تُبْصِرُونَ |
| 'Am 'Anā Khayrun Min Hādhā Al-Ladhī Huwa Mahīnun Wa Lā Yakādu Yubīnu | 52. Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi? | أَمْ أَنَا خَيْر ٌ مِنْ هَذَا الَّذِي هُوَ مَهِين ٌ وَلاَ يَكَادُ يُبِينُ |
| Falawlā 'Ulqiya `Alayhi 'Aswiratun Min Dhahabin 'Aw Jā'a Ma`ahu Al-Malā'ikatu Muqtarinīna | 53. Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama? | فَلَوْلاَ أُلْقِيَ عَلَيْهِ أَسْوِرَة ٌ مِنْ ذَهَبٍ أَوْ جَاءَ مَعَهُ الْمَلاَئِكَةُ مُقْتَرِنِينَ |
| Fāstakhaffa Qawmahu Fa'aţā`ūhu 'Innahum Kānū Qawmāan Fāsiqīna | 54. Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu. | فَاسْتَخَفَّ قَوْمَه ُُ فَأَطَاعُوهُ~ُ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْما ً فَاسِقِينَ |
| Falammā 'Āsafūnā Antaqamnā Minhum Fa'aghraqnāhum 'Ajma`īna | 55. Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote! | فَلَمَّا آسَفُونَا انتَقَمْنَا مِنْهُمْ فَأَغْرَقْنَاهُمْ أَجْمَعِينَ |
| Faja`alnāhum Salafāan Wa Mathalāan Lil'ākhirīna | 56. Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye. | فَجَعَلْنَاهُمْ سَلَفا ً وَمَثَلا ً لِلآخِرِينَ |
| Wa Lammā Đuriba Abnu Maryama Mathalāan 'Idhā Qawmuka Minhu Yaşiddūna | 57. Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele. | وَلَمَّا ضُرِبَ ابْنُ مَرْيَمَ مَثَلا ً إِذَا قَوْمُكَ مِنْهُ يَصِدُّونَ |
| Wa Qālū 'A'ālihatunā Khayrun 'Am Huwa Mā Đarabūhu Laka 'Illā Jadalāan Bal Hum Qawmun Khaşimūna | 58. Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi! | وَقَالُوا أَآلِهَتُنَا خَيْرٌ أَمْ هُوَ مَا ضَرَبُوه ُُ لَكَ إِلاَّ جَدَلا ً بَلْ هُمْ قَوْمٌ خَصِمُونَ |
| 'In Huwa 'Illā `Abdun 'An`amnā `Alayhi Wa Ja`alnāhu Mathalāan Libanī 'Isrā'īla | 59. Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili. | إِنْ هُوَ إِلاَّ عَبْدٌ أَنْعَمْنَا عَلَيْهِ وَجَعَلْنَاه ُُ مَثَلا ً لِبَنِي إِسْرَائِيلَ |
| Wa Law Nashā'u Laja`alnā Minkum Malā'ikatan Fī Al-'Arđi Yakhlufūna | 60. Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana. | وَلَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَا مِنْكُمْ مَلاَئِكَة ً فِي الأَرْضِ يَخْلُفُونَ |
| Wa 'Innahu La`ilmun Lilssā`ati Falā Tamtarunna Bihā Wa Attabi`ūnī Hādhā Şirāţun Mustaqīmun | 61. Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka. | وَإِنَّه ُُ لَعِلْم ٌ لِلسَّاعَةِ فَلاَ تَمْتَرُنَّ بِهَا وَاتَّبِعُونِي هَذَا صِرَاط ٌ مُسْتَقِيم ٌ |
| Wa Lā Yaşuddannakumu Ash-Shayţānu 'Innahu Lakum `Adūwun Mubīnun | 62. Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri. | وَلاَ يَصُدَّنَّكُمُ الشَّيْطَانُ إِنَّه ُُ لَكُمْ عَدُوّ ٌ مُبِين ٌ |
| Wa Lammā Jā'a `Īsá Bil-Bayyināti Qāla Qad Ji'tukum Bil-Ĥikmati Wa Li'abayyina Lakum Ba`đa Al-Ladhī Takhtalifūna Fīhi Fa Attaqū Allāha Wa 'Aţī`ūni | 63. Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi. | وَلَمَّا جَاءَ عِيسَى بِالْبَيِّنَاتِ قَالَ قَدْ جِئْتُكُمْ بِالْحِكْمَةِ وَلِأَبَيِّنَ لَكُمْ بَعْضَ الَّذِي تَخْتَلِفُونَ فِيه ِِ فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ |
| 'Inna Allāha Huwa Rabbī Wa Rabbukum Fā`budūhu Hādhā Şirāţun Mustaqīmun | 64. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka. | إِنَّ اللَّهَ هُوَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوه ُُ هَذَا صِرَاط ٌ مُسْتَقِيم ٌ |
| Fākhtalafa Al-'Aĥzābu Min Baynihim Fawaylun Lilladhīna Žalamū Min `Adhābi Yawmin 'Alīmin | 65. Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu. | فَاخْتَلَفَ الأَحْزَابُ مِنْ بَيْنِهِمْ فَوَيْل ٌ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْ عَذَابِ يَوْمٍ أَلِيم ٍ |
| Hal Yanžurūna 'Illā As-Sā`ata 'An Ta'tiyahum Baghtatan Wa Hum Lā Yash`urūna | 66. Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui? | هَلْ يَنظُرُونَ إِلاَّ السَّاعَةَ أَنْ تَأْتِيَهُمْ بَغْتَة ً وَهُمْ لاَ يَشْعُرُونَ |
| Al-'Akhillā'u Yawma'idhin Ba`đuhum Liba`đin `Adūwun 'Illā Al-Muttaqīna | 67. Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu. | الأَخِلاَّءُ يَوْمَئِذ ٍ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ عَدُوّ ٌ إِلاَّ الْمُتَّقِينَ |
| Yā `Ibādi Lā Khawfun `Alaykumu Al-Yawma Wa Lā 'Antum Taĥzanūna | 68. Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika. | يَاعِبَادِ لاَ خَوْفٌ عَلَيْكُمُ الْيَوْمَ وَلاَ أَنْتُمْ تَحْزَنُونَ |
| Al-Ladhīna 'Āmanū Bi'āyātinā Wa Kānū Muslimīna | 69. Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu. | الَّذِينَ آمَنُوا بِآيَاتِنَا وَكَانُوا مُسْلِمِينَ |
| Adkhulū Al-Jannata 'Antum Wa 'Azwājukum Tuĥbarūna | 70. Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo. | ادْخُلُوا الْجَنَّةَ أَنْتُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ تُحْبَرُونَ |
| Yuţāfu `Alayhim Bişiĥāfin Min Dhahabin Wa 'Akwābin Wa Fīhā Mā Tashtahīhi Al-'Anfusu Wa Taladhdhu Al-'A`yunu Wa 'Antum Fīhā Khālidūna | 71. Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele. | يُطَافُ عَلَيْهِمْ بِصِحَاف ٍ مِنْ ذَهَب ٍ وَأَكْوَاب ٍ وَفِيهَا مَا تَشْتَهِيهِ الأَنفُسُ وَتَلَذُّ الأَعْيُنُ وَأَنْتُمْ فِيهَا خَالِدُونَ |
| Wa Tilka Al-Jannatu Allatī 'Ūrithtumūhā Bimā Kuntum Ta`malūna | 72. Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya. | وَتِلْكَ الْجَنَّةُ الَّتِي أُورِثْتُمُوهَا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ |
| Lakum Fīhā Fākihatun Kathīratun Minhā Ta'kulūna | 73. Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala. | لَكُمْ فِيهَا فَاكِهَة ٌ كَثِيرَة ٌ مِنْهَا تَأْكُلُونَ |
| 'Inna Al-Mujrimīna Fī `Adhābi Jahannama Khālidūn | 74. Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu. | إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي عَذَابِ جَهَنَّمَ خَالِدُون |
| Lā Yufattaru `Anhum Wa Hum Fīhi Mublisūna | 75. Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa. | لاَ يُفَتَّرُ عَنْهُمْ وَهُمْ فِيه ِِ مُبْلِسُونَ |
| Wa Mā Žalamnāhum Wa Lakin Kānū Humu Až-Žālimīna | 76. Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu. | وَمَا ظَلَمْنَاهُمْ وَلَكِنْ كَانُوا هُمُ الظَّالِمِينَ |
| Wa Nādaw Yā Māliku Liyaqđi `Alaynā Rabbuka Qāla 'Innakum Mākithūna | 77. Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo! | وَنَادَوْا يَامَالِكُ لِيَقْضِ عَلَيْنَا رَبُّكَ قَالَ إِنَّكُمْ مَاكِثُونَ |
| Laqad Ji'nākum Bil-Ĥaqqi Wa Lakinna 'Aktharakum Lilĥaqqi Kārihūna | 78. Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki. | لَقَدْ جِئْنَاكُمْ بِالْحَقِّ وَلَكِنَّ أَكْثَرَكُمْ لِلْحَقِّ كَارِهُونَ |
| 'Am 'Abramū 'Amrāan Fa'innā Mubrimūna | 79. Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha. | أَمْ أَبْرَمُوا أَمْرا ً فَإِنَّا مُبْرِمُونَ |
| 'Am Yaĥsabūna 'Annā Lā Nasma`u Sirrahum Wa Najwāhum Balá Wa Rusulunā Ladayhim Yaktubūna | 80. Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika. | أَمْ يَحْسَبُونَ أَنَّا لاَ نَسْمَعُ سِرَّهُمْ وَنَجْوَاهُمْ بَلَى وَرُسُلُنَا لَدَيْهِمْ يَكْتُبُونَ |
| Qul 'In Kāna Lilrraĥmani Waladun Fa'anā 'Awwalu Al-`Ābidīna | 81. Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu. | قُلْ إِنْ كَانَ لِلرَّحْمَنِ وَلَد ٌ فَأَنَا أَوَّلُ الْعَابِدِينَ |
| Subĥāna Rabbi As-Samāwāti Wa Al-'Arđi Rabbi Al-`Arshi `Ammā Yaşifūna | 82. Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia. | سُبْحَانَ رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ رَبِّ الْعَرْشِ عَمَّا يَصِفُونَ |
| Fadharhum Yakhūđū Wa Yal`abū Ĥattá Yulāqū Yawmahumu Al-Ladhī Yū`adūna | 83. Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa. | فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّى يُلاَقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ |
| Wa Huwa Al-Ladhī Fī As-Samā'i 'Ilahun Wa Fī Al-'Arđi 'Ilahun Wa Huwa Al-Ĥakīmu Al-`Alīmu | 84. Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi. | وَهُوَ الَّذِي فِي السَّمَاءِ إِلَه ٌ ٌ وَفِي الأَرْضِ إِلَه ٌ ٌ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ |
| Wa Tabāraka Al-Ladhī Lahu Mulku As-Samāwāti Wa Al-'Arđi Wa Mā Baynahumā Wa `Indahu `Ilmu As-Sā`ati Wa 'Ilayhi Turja`ūna | 85. Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa. | وَتَبَارَكَ الَّذِي لَه ُُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَعِنْدَه ُُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ |
| Wa Lā Yamliku Al-Ladhīna Yad`ūna Min Dūnihi Ash-Shafā`ata 'Illā Man Shahida Bil-Ĥaqqi Wa Hum Ya`lamūna | 86. Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua. | وَلاَ يَمْلِكُ الَّذِينَ يَدْعُونَ مِنْ دُونِهِ الشَّفَاعَةَ إِلاَّ مَنْ شَهِدَ بِالْحَقِّ وَهُمْ يَعْلَمُونَ |
| Wa La'in Sa'altahum Man Khalaqahum Layaqūlunna Allāhu Fa'anná Yu'ufakūna | 87. Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa? | وَلَئِنْ سَأَلْتَهُمْ مَنْ خَلَقَهُمْ لَيَقُولُنَّ اللَّهُ فَأَنَّى يُؤْفَكُونَ |
| Wa Qīlihi Yā Rabbi 'Inna Hā'uulā' Qawmun Lā Yu'uminūna | 88. Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini. | وَقِيلِه ِِ يَارَبِّ إِنَّ هَاؤُلاَء قَوْم ٌ لاَ يُؤْمِنُونَ |
| Fāşfaĥ `Anhum Wa Qul Salāmun Fasawfa Ya`lamūna | 89. Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua. * | فَاصْفَحْ عَنْهُمْ وَقُلْ سَلاَم ٌ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ |