Wa Aş-Şāffāti Şaffāan  | 1. Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. | وَالصَّافَّاتِ صَفّا ً |
Fālzzājirāti Zajrāan  | 2. Na kwa wenye kukataza mabaya. | فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرا ً |
Fālttāliyāti Dhikrāan  | 3. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. | فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرا ً |
'Inna 'Ilahakum Lawāĥidun  | 4. Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. | إِنَّ إِلَهَكُمْ لَوَاحِد ٌ |
Rabbu As-Samāwāti Wa Al-'Arđi Wa Mā Baynahumā Wa Rabbu Al-Mashāriqi  | 5. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo
kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote. | رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ |
'Innā Zayyannā As-Samā'a Ad-Dunyā Bizīnatin Al-Kawākib  | 6. Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa
pambo la nyota. | إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَة ٍ الْكَوَاكِب |
Wa Ĥifžāan Min Kulli Shayţānin Māridin  | 7. Na kulinda na kila shet'ani a'si. | وَحِفْظا ً مِنْ كُلِّ شَيْطَان ٍ مَارِد ٍ |
Lā Yassamma`ūna 'Ilá Al-Mala'i Al-'A`lá Wa Yuqdhafūna Min Kulli Jānibin  | 8. Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa
huko kila upande. | لاَ يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الأَعْلَى وَيُقْذَفُونَ مِنْ كُلِّ جَانِب ٍ |
Duĥūrāan Wa Lahum `Adhābun Wa Aşibun  | 9. Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. | دُحُورا ً وَلَهُمْ عَذَاب ٌ وَاصِب ٌ |
'Illā Man Khaţifa Al-Khaţfata Fa'atba`ahu Shihābun Thāqibāun  | 10. Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara
humfwatia kimondo kinacho ng'ara. | إِلاَّ مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَه ُُ شِهَاب ٌ ثَاقِبا ٌ |
Fāstaftihim 'Ahum 'Ashaddu Khalqāan 'Am Man Khalaqnā 'Innā Khalaqnāhum Min Ţīnin Lāzibin  | 11. Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu
zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo
unao nata. | فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقاً أَمْ مَنْ خَلَقْنَا إِنَّا خَلَقْنَاهُمْ مِنْ طِين ٍ لاَزِب ٍ |
Bal `Ajibta Wa Yaskharūna  | 12. Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. | بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ |
Wa 'Idhā Dhukkirū Lā Yadhkurūna  | 13. Na wanapo kumbushwa hawakumbuki. | وَإِذَا ذُكِّرُوا لاَ يَذْكُرُونَ |
Wa 'Idhā Ra'aw 'Āyatan Yastaskhirūna  | 14. Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara. | وَإِذَا رَأَوْا آيَة ً يَسْتَسْخِرُونَ |
Wa Qālū 'In Hādhā 'Illā Siĥrun Mubīnun  | 15. Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi
tu ulio dhaahiri. | وَقَالُوا إِنْ هَذَا إِلاَّ سِحْر ٌ مُبِين ٌ |
'A'idhā Mitnā Wa Kunnā Turābāan Wa `Ižāmāan 'A'innā Lamab`ūthūna  | 16. Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa
ndio kweli tutafufuliwa? | أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابا ً وَعِظَاماً أَئِنَّا لَمَبْعُوثُونَ |
'Awa'ābā'uunā Al-'Awwalūna  | 17. Hata baba zetu wa zamani? | أَوَآبَاؤُنَا الأَوَّلُونَ |
Qul Na`am Wa 'Antum Dākhirūna  | 18. Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili. | قُلْ نَعَمْ وَأَنْتُمْ دَاخِرُونَ |
Fa'innamā Hiya Zajratun Wāĥidatun Fa'idhā Hum Yanžurūna  | 19. Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio
wataona! | فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَة ٌ وَاحِدَة ٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ |
Wa Qālū Yā Waylanā Hādhā Yawmu Ad-Dīni  | 20. Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. | وَقَالُوا يَاوَيْلَنَا هَذَا يَوْمُ الدِّينِ |
Hādhā Yawmu Al-Faşli Al-Ladhī Kuntum Bihi Tukadhdhibūna  | 21. Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha. | هَذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُمْ بِه ِِ تُكَذِّبُونَ |
Aĥshurū Al-Ladhīna Žalamū Wa 'Azwājahum Wa Mā Kānū Ya`budūna  | 22. Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na
hao walio kuwa wakiwaabudu - | احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ |
Min Dūni Allāhi Fāhdūhum 'Ilá Şirāţi Al-Jaĥīmi  | 23. Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia
ya Jahannamu! | مِنْ دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَى صِرَاطِ الْجَحِيمِ |
Wa Qifūhum 'Innahum Mas'ūlūna  | 24. Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: | وَقِفُوهُمْ إِنَّهُمْ مَسْئُولُونَ |
Mā Lakum Lā Tanāşarūna  | 25. Mna nini? Mbona hamsaidiani? | مَا لَكُمْ لاَ تَنَاصَرُونَ |
Bal Humu Al-Yawma Mustaslimūna  | 26. Bali hii leo, watasalimu amri. | بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ |
Wa 'Aqbala Ba`đuhum `Alá Ba`đin Yatasā'alūna  | 27. Watakabiliana wao kwa wao kuulizana. | وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَى بَعْض ٍ يَتَسَاءَلُونَ |
Qālū 'Innakum Kuntum Ta'tūnanā `Ani Al-Yamīni  | 28. Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia
upande wa kulia. | قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ |
Qālū Bal Lam Takūnū Mu'uminīna  | 29. Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa
Waumini. | قَالُوا بَلْ لَمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ |
Wa Mā Kāna Lanā `Alaykum Min Sulţānin Bal Kuntum Qawmāan Ţāghīna  | 30. Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi
wenyewe mlikuwa wapotovu. | وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُمْ مِنْ سُلْطَان ٍ بَلْ كُنتُمْ قَوْما ً طَاغِينَ |
Faĥaqqa `Alaynā Qawlu Rabbinā 'Innā Ladhā'iqūna  | 31. Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha
tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. | فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا إِنَّا لَذَائِقُونَ |
Fa'aghwaynākum 'Innā Kunnā Ghāwīna  | 32. Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa
wapotovu. | فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ |
Fa'innahum Yawma'idhin Fī Al-`Adhābi Mushtarikūna  | 33. Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana
katika adhabu pamoja. | فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذ ٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ |
'Innā Kadhālika Naf`alu Bil-Mujrimīna  | 34. Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu. | إِنَّا كَذَلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ |
'Innahum Kānū 'Idhā Qīla Lahum Lā 'Ilāha 'Illā Allāhu Yastakbirūna  | 35. Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa
'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna. | إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لاَ إِلَهَ~َ إِلاَّ اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ |
Wa Yaqūlūna 'A'innā Latārikū 'Ālihatinā Lishā`irin Majnūnin  | 36. Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu
kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? | وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوا آلِهَتِنَا لِشَاعِر ٍ مَجْنُون ٍ |
Bal Jā'a Bil-Ĥaqqi Wa Şaddaqa Al-Mursalīna  | 37. Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha
Mitume. | بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ |
'Innakum Ladhā'iqū Al-`Adhābi Al-'Alīmi  | 38. Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu
chungu. | إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الأَلِيمِ |
Wa Mā Tujzawna 'Illā Mā Kuntum Ta`malūna  | 39. Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya. | وَمَا تُجْزَوْنَ إِلاَّ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ |
'Illā `Ibāda Allāhi Al-Mukhlaşīna  | 40. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. | إِلاَّ عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ |
'Ūlā'ika Lahum Rizqun Ma`lūmun  | 41. Hao ndio watakao pata riziki maalumu, | أُوْلَائِكَ لَهُمْ رِزْق ٌ مَعْلُوم ٌ |
Fawākihu Wa Hum Mukramūna  | 42. Matunda, nao watahishimiwa. | فَوَاكِه ُُ وَهُمْ مُكْرَمُونَ |
Fī Jannāti An-Na`īmi  | 43. Katika Bustani za neema. | فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ |
`Alá Sururin Mutaqābilīna  | 44. Wako juu ya viti wamekabiliana. | عَلَى سُرُر ٍ مُتَقَابِلِينَ |
Yuţāfu `Alayhim Bika'sin Min Ma`īnin  | 45. Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha
chemchem | يُطَافُ عَلَيْهِمْ بِكَأْس ٍ مِنْ مَعِين ٍ |
Bayđā'a Ladhdhatin Lilshshāribīna  | 46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao. | بَيْضَاءَ لَذَّة ٍ لِلشَّارِبِينَ |
Lā Fīhā Ghawlun Wa Lā Hum `Anhā Yunzafūna  | 47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi. | لاَ فِيهَا غَوْل ٌ وَلاَ هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ |
Wa `Indahum Qāşirātu Aţ-Ţarfi `Īnun  | 48. Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha
mazuri. | وَعِنْدَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِين ٌ |
Ka'annahunna Bayđun Maknūnun  | 49. Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. | كَأَنَّهُنَّ بَيْض ٌ مَكْنُون ٌ |
Fa'aqbala Ba`đuhum `Alá Ba`đin Yatasā'alūna  | 50. Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe. | فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَى بَعْض ٍ يَتَسَاءَلُونَ |
Qāla Qā'ilun Minhum 'Innī Kāna Lī Qarīnun  | 51. Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika
mimi nalikuwa na rafiki | قَالَ قَائِل ٌ مِنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِين ٌ |
Yaqūlu 'A'innaka Lamina Al-Muşaddiqīna  | 52. Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika
wanao sadiki | يَقُولُ أَئِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ |
'A'idhā Mitnā Wa Kunnā Turābāan Wa `Ižāmāan 'A'innā Lamadīnūna  | 53. Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa,
ndio tutalipwa na kuhisabiwa? | أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابا ً وَعِظَاماً أَئِنَّا لَمَدِينُونَ |
Qāla Hal 'Antum Muţţali`ūna  | 54. Atasema: Je! Nyie mnawaona? | قَالَ هَلْ أَنْتُمْ مُطَّلِعُونَ |
Fāţţala`a Fara'āhu Fī Sawā'i Al-Jaĥīmi  | 55. Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu. | فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ |
Qāla Ta-Allāhi 'In Kidta Laturdīni  | 56. Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza. | قَالَ تَاللَّهِ إِنْ كِدْتَ لَتُرْدِينِ |
Wa Lawlā Ni`matu Rabbī Lakuntu Mina Al-Muĥđarīna  | 57. Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi
bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. | وَلَوْلاَ نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ |
'Afamā Naĥnu Bimayyitīna  | 58. Je! Sisi hatutakufa, | أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ |
'Illā Mawtatanā Al-'Ūlá Wa Mā Naĥnu Bimu`adhdhabīna  | 59. Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi
hatutaadhibiwa. | إِلاَّ مَوْتَتَنَا الأُولَى وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ |
'Inna Hādhā Lahuwa Al-Fawzu Al-`Ažīmu  | 60. Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa. | إِنَّ هَذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ |
Limithli Hādhā Falya`mali Al-`Āmilūna  | 61. Kwa mfano wa haya nawatende watendao. | لِمِثْلِ هَذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ |
'Adhalika Khayrun Nuzulāan 'Am Shajaratu Az-Zaqqūmi  | 62. Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti
wa Zaqqum? | أَذَلِكَ خَيْر ٌ نُزُلاً أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ |
'Innā Ja`alnāhā Fitnatan Lilžžālimīna  | 63. Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso
kwa walio dhulumu. | إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَة ً لِلظَّالِمِينَ |
'Innahā Shajaratun Takhruju Fī 'Aşli Al-Jaĥīmi  | 64. Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu. | إِنَّهَا شَجَرَة ٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ |
Ţal`uhā Ka'annahu Ru'ūsu Ash-Shayāţīni  | 65. Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa
vya mashet'ani. | طَلْعُهَا كَأَنَّه ُُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ |
Fa'innahum La'ākilūna Minhā Famāli'ūna Minhā Al-Buţūna  | 66. Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo,
na wajaze matumbo. | فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ |
Thumma 'Inna Lahum `Alayhā Lashawbāan Min Ĥamīmin  | 67. Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji
yamoto yaliyo chemka. | ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبا ً مِنْ حَمِيم ٍ |
Thumma 'Inna Marji`ahum La'ilá Al-Jaĥīmi  | 68. Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa
kwenye Jahannamu. | ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ |
'Innahum 'Alfaw 'Ābā'ahum Đāllīna  | 69. Hakika waliwakuta baba zao wamepotea. | إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ |
Fahum `Alá 'Āthārihim Yuhra`ūna  | 70. Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. | فَهُمْ عَلَى آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ |
Wa Laqad Đalla Qablahum 'Aktharu Al-'Awwalīna  | 71. Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao
wengi wa watu wa zamani. | وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الأَوَّلِينَ |
Wa Laqad 'Arsalnā Fīhim Mundhirīna  | 72. Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. | وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِمْ مُنذِرِينَ |
Fānžur Kayfa Kāna `Āqibatu Al-Mundharīna  | 73. Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio
onywa. | فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ |
'Illā `Ibāda Allāhi Al-Mukhlaşīna  | 74. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. | إِلاَّ عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ |
Wa Laqad Nādānā Nūĥun Falani`ma Al-Mujībūna  | 75. Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora
wa waitikiaji. | وَلَقَدْ نَادَانَا نُوح ٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ |
Wa Najjaynāhu Wa 'Ahlahu Mina Al-Karbi Al-`Ažīmi  | 76. Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana
na msiba mkubwa. | وَنَجَّيْنَاه ُُ وَأَهْلَه ُُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ |
Wa Ja`alnā Dhurrīyatahu Humu Al-Bāqīna  | 77. Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia. | وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَه ُُ هُمُ الْبَاقِينَ |
Wa Taraknā `Alayhi Fī Al-'Ākhirīna  | 78. Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja
baadaye. | وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الآخِرِينَ |
Salāmun `Alá Nūĥin Fī Al-`Ālamīna  | 79. Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote! | سَلاَمٌ عَلَى نُوح ٍ فِي الْعَالَمِينَ |
'Innā Kadhālika Najzī Al-Muĥsinīna  | 80. Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao
fanya mema. | إِنَّا كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
'Innahu Min `Ibādinā Al-Mu'uminīna  | 81. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | إِنَّه ُُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ |
Thumma 'Aghraqnā Al-'Ākharīna  | 82. Kisha tukawazamisha wale wengine. | ثُمَّ أَغْرَقْنَا الآخَرِينَ |
Wa 'Inna Min Shī`atihi La'ibrāhīma  | 83. Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake, | وَإِنَّ مِنْ شِيعَتِه ِِ لَإِبْرَاهِيمَ |
'Idh Jā'a Rabbahu Biqalbin Salīmin  | 84. Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima. | إِذْ جَاءَ رَبَّه ُُ بِقَلْب ٍ سَلِيم ٍ |
'Idh Qāla Li'abīhi Wa Qawmihi Mādhā Ta`budūna  | 85. Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu
nini? | إِذْ قَالَ لِأَبِيه ِِ وَقَوْمِه ِِ مَاذَا تَعْبُدُونَ |
'A'ifkāan 'Ālihatan Dūna Allāhi Turīdūna  | 86. Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala
ya Mwenyezi Mungu? | أَئِفْكا ً آلِهَة ً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ |
Famā Žannukum Birabbi Al-`Ālamīna  | 87. Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu
wote? | فَمَا ظَنُّكُمْ بِرَبِّ الْعَالَمِينَ |
Fanažara Nažratan Fī An-Nujūmi  | 88. Kisha akapiga jicho kutazama nyota. | فَنَظَرَ نَظْرَة ً فِي النُّجُومِ |
Faqāla 'Innī Saqīmun  | 89. Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! | فَقَالَ إِنِّي سَقِيم ٌ |
Fatawallaw `Anhu Mudbirīna  | 90. Nao wakamwacha, wakampa kisogo. | فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ |
Farāgha 'Ilá 'Ālihatihim Faqāla 'Alā Ta'kulūna  | 91. Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia:
Mbona hamli? | فَرَاغَ إِلَى آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلاَ تَأْكُلُونَ |
Mā Lakum Lā Tanţiqūna  | 92. Mna nini hata hamsemi? | مَا لَكُمْ لاَ تَنطِقُونَ |
Farāgha `Alayhim Đarbāan Bil-Yamīni  | 93. Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia. | فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبا ً بِالْيَمِينِ |
Fa'aqbalū 'Ilayhi Yaziffūna  | 94. Basi wakamjia upesi upesi. | فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ |
Qāla 'Ata`budūna Mā Tanĥitūna  | 95. Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga
wenyewe? | قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ |
Wa Allāhu Khalaqakum Wa Mā Ta`malūna  | 96. Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni
nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! | وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ |
Qālū Abnū Lahu Bunyānāan Fa'alqūhu Fī Al-Jaĥīmi  | 97. Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni
motoni humo! | قَالُوا ابْنُوا لَه ُُ بُنْيَانا ً فَأَلْقُوه ُُ فِي الْجَحِيمِ |
Fa'arādū Bihi Kaydāan Faja`alnāhumu Al-'Asfalīna  | 98. Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya
wao ndio wa chini. | فَأَرَادُوا بِه ِِ كَيْدا ً فَجَعَلْنَاهُمُ الأَسْفَلِينَ |
Wa Qāla 'Innī Dhāhibun 'Ilá Rabbī Sayahdīni  | 99. Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda
kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. | وَقَالَ إِنِّي ذَاهِب ٌ إِلَى رَبِّي سَيَهْدِينِ |
Rabbi Hab Lī Mina Aş-Şāliĥīna  | 100. Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni
mwa watenda mema. | رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ |
Fabashsharnāhu Bighulāmin Ĥalīmin  | 101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole. | فَبَشَّرْنَاه ُُ بِغُلاَمٍ حَلِيم ٍ |
Falammā Balagha Ma`ahu As-Sa`ya Qāla Yā Bunayya 'Innī 'Ará Fī Al-Manāmi 'Annī 'Adhbaĥuka Fānžur Mādhā Tará Qāla Yā 'Abati Af`al Mā Tu'umaru Satajidunī 'In Shā'a Allāhu Mina Aş-Şābirīna  | 102. Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi
pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa
ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda
unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri. | فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَابُنَيَّ إِنِّي أَرَى فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَى قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ سَتَجِدُنِي إِنْ شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ |
Falammā 'Aslamā Wa Tallahu Liljabīni  | 103. Basi wote wawili walipo jisalimisha, na
akamlaza juu ya kipaji. | فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّه ُُ لِلْجَبِينِ |
Wa Nādaynāhu 'An Yā 'Ibrāhīmu  | 104. Tulimwita: Ewe Ibrahim! | وَنَادَيْنَاهُ~ُ أَنْ يَا إِبْرَاهِيمُ |
Qad Şaddaqta Ar-Ru'uyā 'Innā Kadhālika Najzī Al-Muĥsinīna  | 105. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi
ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema. | قَد صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا إِنَّا كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
'Inna Hādhā Lahuwa Al-Balā'u Al-Mubīnu  | 106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri. | إِنَّ هَذَا لَهُوَ الْبَلاَءُ الْمُبِينُ |
Wa Fadaynāhu Bidhibĥin `Ažīmin  | 107. Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. | وَفَدَيْنَاه ُُ بِذِبْحٍ عَظِيم ٍ |
Wa Taraknā `Alayhi Fī Al-'Ākhirīna  | 108. Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio
kuja baadaye. | وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الآخِرِينَ |
Salāmun `Alá 'Ibrāhīma  | 109. Iwe salama kwa Ibrahim! | سَلاَمٌ عَلَى إِبْرَاهِيمَ |
Kadhālika Najzī Al-Muĥsinīna  | 110. Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya
mema. | كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
'Innahu Min `Ibādinā Al-Mu'uminīna  | 111. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | إِنَّه ُُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ |
Wa Bashsharnāhu Bi'isĥāqa Nabīyāan Mina Aş-Şāliĥīna  | 112. Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye
ni Nabii miongoni mwa watu wema. | وَبَشَّرْنَاه ُُ بِإِسْحَاقَ نَبِيّا ً مِنَ الصَّالِحِينَ |
Wa Bāraknā `Alayhi Wa `Alá 'Isĥāqa Wa Min Dhurrīyatihimā Muĥsinun Wa Žālimun Linafsihi Mubīnun  | 113. Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni
mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. | وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَى إِسْحَاقَ وَمِنْ ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِن ٌ وَظَالِم ٌ لِنَفْسِه ِِ مُبِين ٌ |
Wa Laqad Manannā `Alá Mūsá Wa Hārūna  | 114. Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa
na Haruni. | وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَى مُوسَى وَهَارُونَ |
Wa Najjaynāhumā Wa Qawmahumā Mina Al-Karbi Al-`Ažīmi  | 115. Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana
na dhiki kubwa. | وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ |
Wa Naşarnāhum Fakānū Humu Al-Ghālibīna  | 116. Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye
kushinda. | وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ |
Wa 'Ātaynāhumā Al-Kitāba Al-Mustabīna  | 117. Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha. | وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ |
Wa Hadaynāhumā Aş-Şirāţa Al-Mustaqīma  | 118. Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. | وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ |
Wa Taraknā `Alayhimā Fī Al-'Ākhirīna  | 119. Na tukawaachia (sifa njema) katika watu
walio kuja baadaye. | وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الآخِرِينَ |
Salāmun `Alá Mūsá Wa Hārūna  | 120. Iwe salama kwa Musa na Haruni! | سَلاَمٌ عَلَى مُوسَى وَهَارُونَ |
'Innā Kadhālika Najzī Al-Muĥsinīna  | 121. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio
wema. | إِنَّا كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
'Innahumā Min `Ibādinā Al-Mu'uminīna  | 122. Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio
amini. | إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna 'Ilyāsa Lamina Al-Mursalīna  | 123. Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni
mwa Mitume. | وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ |
'Idh Qāla Liqawmihi 'Alā Tattaqūna  | 124. Alipo waambia watu wake: Hamwogopi? | إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ~ِ أَلاَ تَتَّقُونَ |
'Atad`ūna Ba`lāan Wa Tadharūna 'Aĥsana Al-Khāliqīna  | 125. Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa
waumbaji, | أَتَدْعُونَ بَعْلا ً وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ |
Allāha Rabbakum Wa Rabba 'Ābā'ikumu Al-'Awwalīna  | 126. Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola
Mlezi wa baba zenu wa zamani? | اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الأَوَّلِينَ |
Fakadhdhabūhu Fa'innahum Lamuĥđarūna  | 127. Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa; | فَكَذَّبُوه ُُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ |
'Illā `Ibāda Allāhi Al-Mukhlaşīna  | 128. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio
safishwa. | إِلاَّ عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ |
Wa Taraknā `Alayhi Fī Al-'Ākhirīna  | 129. Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja
baadaye. | وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الآخِرِينَ |
Salāmun `Alá 'Il Yā -Sīn  | 130. Iwe salama kwa Ilyas. | سَلاَمٌ عَلَى إِلْ يَا-سِين |
'Innā Kadhālika Najzī Al-Muĥsinīna  | 131. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio
wema. | إِنَّا كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ |
'Innahu Min `Ibādinā Al-Mu'uminīna  | 132. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | إِنَّه ُُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna Lūţāan Lamina Al-Mursalīna  | 133. Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni
mwa Mitume. | وَإِنَّ لُوطا ً لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ |
'Idh Najjaynāhu Wa 'Ahlahu 'Ajma`īna  | 134. Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote, | إِذْ نَجَّيْنَاه ُُ وَأَهْلَهُ~ُ أَجْمَعِينَ |
'Illā `Ajūzāan Fī Al-Ghābirīna  | 135. Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale
walio bakia nyuma. | إِلاَّ عَجُوزا ً فِي الْغَابِرِينَ |
Thumma Dammarnā Al-'Ākharīna  | 136. Kisha tukawaangamiza wale wengineo. | ثُمَّ دَمَّرْنَا الآخَرِينَ |
Wa 'Innakum Latamurrūna `Alayhim Muşbiĥīna  | 137. Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi, | وَإِنَّكُمْ لَتَمُرّ |