Ţā-Sīn-Mīm  | 1. T'aa Siin Miim. (T'.S.M.) | طَا-سِين-مِيم |
Tilka 'Āyātu Al-Kitābi Al-Mubīni  | 2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha. | تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ |
La`allaka Bākhi`un Nafsaka 'Allā Yakūnū Mu'uminīna  | 3. Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa
hawawi Waumini. | لَعَلَّكَ بَاخِع ٌ نَفْسَكَ أَلاَّ يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ |
'In Nasha' Nunazzil `Alayhim Mina As-Samā'i 'Āyatan Fažallat 'A`nāquhum Lahā Khāđi`īna  | 4. Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni
Ishara zikanyenyekea shingo zao. | إِنْ نَشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِمْ مِنَ السَّمَاءِ آيَة ً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ لَهَا خَاضِعِينَ |
Wa Mā Ya'tīhim Min Dhikrin Mina Ar-Raĥmāni Muĥdathin 'Illā Kānū `Anhu Mu`riđīna  | 5. Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman
ila wao hujitenga nao. | وَمَا يَأْتِيهِمْ مِنْ ذِكْر ٍ مِنَ الرَّحْمَنِ مُحْدَث ٍ إِلاَّ كَانُوا عَنْهُ مُعْرِضِينَ |
Faqad Kadhdhabū Fasaya'tīhim 'Anbā'u Mā Kānū Bihi Yastahzi'ūn  | 6. Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja
wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha. | فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنْبَاءُ مَا كَانُوا بِه ِِ يَسْتَهْزِئُون |
'Awalam Yaraw 'Ilá Al-'Arđi Kam 'Anbatnā Fīhā Min Kulli Zawjin Karīmin  | 7. Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha
humo, ya kila namna nzuri? | أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الأَرْضِ كَمْ أَنْبَتْنَا فِيهَا مِنْ كُلِّ زَوْج ٍ كَرِيم ٍ |
'Inna Fī Dhālika La'āyatan Wa Mā Kāna 'Aktharuhum Mu'uminīna  | 8. Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi
wao hawakuwa wenye kuamini. | إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَة ً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُمْ مُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna Rabbaka Lahuwa Al-`Azīzu Ar-Raĥīmu  | 9. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye
nguvu Mwenye kurehemu. | وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ |
Wa 'Idh Nādá Rabbuka Mūsá 'Ani A'ti Al-Qawma Až-Žālimīna  | 10. Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia:
Fika kwa watu madhaalimu, | وَإِذْ نَادَى رَبُّكَ مُوسَى أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ |
Qawma Fir`awna 'Alā Yattaqūna  | 11. Watu wa Firauni. Hawaogopi? | قَوْمَ فِرْعَوْنَ أَلاَ يَتَّقُونَ |
Qāla Rabbi 'Innī 'Akhāfu 'An Yukadhdhibūni  | 12. Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe. | قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَنْ يُكَذِّبُونِ |
Wa Yađīqu Şadrī Wa Lā Yanţaliqu Lisānī Fa'arsil 'Ilá Hārūna  | 13. Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu
haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun. | وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلاَ يَنْطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَى هَارُونَ |
Wa Lahum `Alayya Dhanbun Fa'akhāfu 'An Yaqtulūni  | 14. Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa
wasije kuniuwa. | وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنْب ٌ فَأَخَافُ أَنْ يَقْتُلُونِ |
Qāla Kallā Fādh/habā Bi'āyātinā 'Innā Ma`akum Mustami`ūna  | 15. Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza
yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza. | قَالَ كَلاَّ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا إِنَّا مَعَكُمْ مُسْتَمِعُونَ |
Fa'tiyā Fir`awna Faqūlā 'Innā Rasūlu Rabbi Al-`Ālamīna  | 16. Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika
sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote. | فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولاَ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ |
'An 'Arsil Ma`anā Banī 'Isrā'īla  | 17. Waachilie Wana wa Israili wende nasi. | أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ |
Qāla 'Alam Nurabbika Fīnā Walīdāan Wa Labithta Fīnā Min `Umurika Sinīna  | 18. (Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe
utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi? | قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدا ً وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ |
Wa Fa`alta Fa`lataka Allatī Fa`alta Wa 'Anta Mina Al-Kāfirīna  | 19. Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe
ukawa miongoni mwa wasio na shukrani? | وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنْتَ مِنَ الْكَافِرِينَ |
Qāla Fa`altuhā 'Idhāan Wa 'Anā Mina Ađ-Đāllīn  | 20. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo
kuwa miongoni mwa wale walio potea. | قَالَ فَعَلْتُهَا إِذا ً وَأَنَا مِنَ الضَّالِّين |
Fafarartu Minkum Lammā Khiftukum Fawahaba Lī Rabbī Ĥukmāan Wa Ja`alanī Mina Al-Mursalīna  | 21. Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena
Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa
Mitume. | فَفَرَرْتُ مِنْكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْما ً وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُرْسَلِينَ |
Wa Tilka Ni`matun Tamunnuhā `Alayya 'An `Abbadta Banī 'Isrā'īla  | 22. Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe
umewatia utumwani Wana wa Israili? | وَتِلْكَ نِعْمَة ٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدْتَ بَنِي إِسْرَائِيلَ |
Qāla Fir`awnu Wa Mā Rabbu Al-`Ālamīna  | 23. Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi
wa walimwengu wote? | قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ |
Qāla Rabbu As-Samāwāti Wa Al-'Arđi Wa Mā Baynahumā 'In Kuntum Mūqinīna  | 24. Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi,
na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini. | قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا إنْ كُنتُمْ مُوقِنِينَ |
Qāla Liman Ĥawlahu 'Alā Tastami`ūna  | 25. (Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi? | قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ~ُ أَلاَ تَسْتَمِعُونَ |
Qāla Rabbukum Wa Rabbu 'Ābā'ikumu Al-'Awwalīna  | 26. (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na
Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza. | قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الأَوَّلِينَ |
Qāla 'Inna Rasūlakumu Al-Ladhī 'Ursila 'Ilaykum Lamajnūnun  | 27. (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu
aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu. | قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُون ٌ |
Qāla Rabbu Al-Mashriqi Wa Al-Maghribi Wa Mā Baynahumā 'In Kuntum Ta`qilūna  | 28. (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki
na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini. | قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا إِنْ كُنْتُمْ تَعْقِلُونَ |
Qāla La'ini Attakhadhta 'Ilahāan Ghayrī La'aj`alannaka Mina Al-Masjūnīna  | 29. (Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine
asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani. | قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَهَاً غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ |
Qāla 'Awalaw Ji'tuka Bishay'in Mubīnin  | 30. Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu
cha kubainisha wazi? | قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْء ٍ مُبِين ٍ |
Qāla Fa'ti Bihi 'In Kunta Mina Aş-Şādiqīna  | 31. Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika
wasemao kweli. | قَالَ فَأْتِ بِهِ~ِ إِنْ كُنْتَ مِنَ الصَّادِقِينَ |
Fa'alqá `Aşāhu Fa'idhā Hiya Thu`bānun Mubīnun  | 32. Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka
wa kuonekana dhaahiri. | فَأَلْقَى عَصَاه ُُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَان ٌ مُبِين ٌ |
Wa Naza`a Yadahu Fa'idhā Hiya Bayđā'u Lilnnāžirīna  | 33. Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe
kwa watazamao. | وَنَزَعَ يَدَه ُُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ |
Qāla Lilmala'i Ĥawlahu 'Inna Hādhā Lasāĥirun `Alīmun  | 34. (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka:
Hakika huyu ni mchawi mtaalamu. | قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ~ُ إِنَّ هَذَا لَسَاحِرٌ عَلِيم ٌ |
Yurīdu 'An Yukhrijakum Min 'Arđikum Bisiĥrihi Famādhā Ta'murūna  | 35. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi
wake. Basi mna shauri gani? | يُرِيدُ أَنْ يُخْرِجَكُمْ مِنْ أَرْضِكُمْ بِسِحْرِه ِِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ |
Qālū 'Arjihi Wa 'Akhāhu Wa Ab`ath Fī Al-Madā'ini Ĥāshirīna  | 36. Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume
mijini wapigao mbiu ya mgambo. | قَالُوا أَرْجِه ِِ وَأَخَاه ُُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ |
Ya'tūka Bikulli Saĥĥārin `Alīmin  | 37. Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu. | يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيم ٍ |
Fajumi`a As-Saĥaratu Limīqāti Yawmin Ma`lūmin  | 38. Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku
maalumu. | فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْم ٍ مَعْلُوم ٍ |
Wa Qīla Lilnnāsi Hal 'Antum Mujtami`ūna  | 39. Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika? | وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنْتُمْ مُجْتَمِعُونَ |
La`allanā Nattabi`u As-Saĥarata 'In Kānū Humu Al-Ghālibīna  | 40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio
watakao shinda. | لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِنْ كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ |
Falammā Jā'a As-Saĥaratu Qālū Lifir`awna 'A'inna Lanā La'ajrāan 'In Kunnā Naĥnu Al-Ghālibīna  | 41. Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni:
Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda? | فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرا ً إِنْ كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ |
Qāla Na`am Wa 'Innakum 'Idhāan Lamina Al-Muqarrabīna  | 42. Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele. | قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذا ً لَمِنَ الْمُقَرَّبِينَ |
Qāla Lahum Mūsá 'Alqū Mā 'Antum Mulqūna  | 43. Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa. | قَالَ لَهُمْ مُوسَى أَلْقُوا مَا أَنْتُمْ مُلْقُونَ |
Fa'alqaw Ĥibālahum Wa `Işīyahum Wa Qālū Bi`izzati Fir`awna 'Innā Lanaĥnu Al-Ghālibūna  | 44. Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na
wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda. | فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ |
Fa'alqá Mūsá `Aşāhu Fa'idhā Hiya Talqafu Mā Ya'fikūna  | 45. Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza
walivyo vizua. | فَأَلْقَى مُوسَى عَصَاه ُُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ |
Fa'ulqiya As-Saĥaratu Sājidīna  | 46. Hapo wachawi walipinduka wakasujudu. | فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ |
Qālū 'Āmannā Birabbi Al-`Ālamīna  | 47. Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu
wote. | قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ |
Rabbi Mūsá Wa Hārūna  | 48. Mola Mlezi wa Musa na Harun. | رَبِّ مُوسَى وَهَارُونَ |
Qāla 'Āmantum Lahu Qabla 'An 'Ādhana Lakum 'Innahu Lakabīrukumu Al-Ladhī `Allamakumu As-Siĥra Falasawfa Ta`lamūna La'uqaţţi`anna 'Aydiyakum Wa 'Arjulakum Min Khilāfin Wa La'uşallibannakum 'Ajma`īna  | 49. (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni?
Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi
mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni
misalabani nyote. | قَالَ آمَنْتُمْ لَه ُُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ إِنَّه ُُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ مِنْ خِلاَف ٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ |
Qālū Lā Đayra 'Innā 'Ilá Rabbinā Munqalibūna  | 50. Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea
kwa Mola wetu Mlezi. | قَالُوا لاَ ضَيْرَ إِنَّا إِلَى رَبِّنَا مُنْقَلِبُونَ |
'Innā Naţma`u 'An Yaghfira Lanā Rabbunā Khaţāyānā 'An Kunnā 'Awwala Al-Mu'uminīna  | 51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe
makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini. | إِنَّا نَطْمَعُ أَنْ يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَنْ كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ |
Wa 'Awĥaynā 'Ilá Mūsá 'An 'Asri Bi`ibādī 'Innakum Muttaba`ūna  | 52. Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na
waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa. | وَأَوْحَيْنَا إِلَى مُوسَى أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُمْ مُتَّبَعُونَ |
Fa'arsala Fir`awnu Fī Al-Madā'ini Ĥāshirīna  | 53. Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu
za mgambo. | فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ |
'Inna Hā'uulā' Lashirdhimatun Qalīlūna  | 54. (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo. | إِنَّ هَاؤُلاَء لَشِرْذِمَة ٌ قَلِيلُونَ |
Wa 'Innahum Lanā Laghā'ižūna  | 55. Nao wanatuudhi. | وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَائِظُونَ |
Wa 'Innā Lajamī`un Ĥādhirūna  | 56. Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari. | وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَاذِرُونَ |
Fa'akhrajnāhum Min Jannātin Wa `Uyūnin  | 57. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem, | فَأَخْرَجْنَاهُمْ مِنْ جَنَّات ٍ وَعُيُون ٍ |
Wa Kunūzin Wa Maqāmin Karīmin  | 58. Na makhazina, na vyeo vya hishima, | وَكُنُوز ٍ وَمَقَام ٍ كَرِيم ٍ |
Kadhālika Wa 'Awrathnāhā Banī 'Isrā'īla  | 59. Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa
Israili. | كَذَلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ |
Fa'atba`ūhum Mushriqīna  | 60. Basi wakawafuata lilipo chomoza jua. | فَأَتْبَعُوهُمْ مُشْرِقِينَ |
Falammā Tarā'á Al-Jam`āni Qāla 'Aşĥābu Mūsá 'Innā Lamudrakūna  | 61. Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu
wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana! | فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَى إِنَّا لَمُدْرَكُونَ |
Qāla Kallā 'Inna Ma`iya Rabbī Sayahdīni  | 62. (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami
Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa! | قَالَ كَلاَّ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ |
Fa'awĥaynā 'Ilá Mūsá 'Ani Ađrib Bi`aşāka Al-Baĥra Fānfalaqa Fakāna Kullu Firqin Kālţţawdi Al-`Ažīmi  | 63. Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari
kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa. | فَأَوْحَيْنَا إِلَى مُوسَى أَنِ اضْرِبْ بِعَصَاكَ الْبَحْرَ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْق ٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ |
Wa 'Azlafnā Thamma Al-'Ākharīna  | 64. Na tukawajongeza hapo wale wengine. | وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الآخَرِينَ |
Wa 'Anjaynā Mūsá Wa Man Ma`ahu 'Ajma`īna  | 65. Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye
wote. | وَأَنْجَيْنَا مُوسَى وَمَنْ مَعَهُ~ُ أَجْمَعِينَ |
Thumma 'Aghraqnā Al-'Ākharīna  | 66. Kisha tukawazamisha hao wengine. | ثُمَّ أَغْرَقْنَا الآخَرِينَ |
'Inna Fī Dhālika La'āyatan Wa Mā Kāna 'Aktharuhum Mu'uminīna  | 67. Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara;
lakini wengi wao si katika wenye kuamini. | إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَة ً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُمْ مُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna Rabbaka Lahuwa Al-`Azīzu Ar-Raĥīmu  | 68. Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye
nguvu Mwenye kurehemu. | وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ |
Wa Atlu `Alayhim Naba'a 'Ibrāhīma  | 69. Na wasomee khabari za Ibrahim. | وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَاهِيمَ |
'Idh Qāla Li'abīhi Wa Qawmihi Mā Ta`budūna  | 70. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu
nini? | إِذْ قَالَ لِأَبِيه ِِ وَقَوْمِه ِِ مَا تَعْبُدُونَ |
Qālū Na`budu 'Aşnāmāan Fanažallu Lahā `Ākifīna  | 71. Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea. | قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَاما ً فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ |
Qāla Hal Yasma`ūnakum 'Idh Tad`ūna  | 72. Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita? | قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ |
'Aw Yanfa`ūnakum 'Aw Yađurrūna  | 73. Au yanakufaeni, au yanakudhuruni? | أَوْ يَنْفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ |
Qālū Bal Wajadnā 'Ābā'anā Kadhālika Yaf`alūna  | 74. Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya
hivyo hivyo. | قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَلِكَ يَفْعَلُونَ |
Qāla 'Afara'aytum Mā Kuntum Ta`budūna  | 75. Je! Mmewaona hawa mnao waabudu- | قَالَ أَفَرَأَيْتُمْ مَا كُنْتُمْ تَعْبُدُونَ |
'Antum Wa 'Ābā'uukumu Al-'Aqdamūna  | 76. Nyinyi na baba zenu wa zamani? | أَنْتُمْ وَآبَاؤُكُمُ الأَقْدَمُونَ |
Fa'innahum `Adūwun Lī 'Illā Rabba Al-`Ālamīna  | 77. Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa
Mola Mlezi wa walimwengu wote. | فَإِنَّهُمْ عَدُوّ ٌ لِي إِلاَّ رَبَّ الْعَالَمِينَ |
Al-Ladhī Khalaqanī Fahuwa Yahdīni  | 78. Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye
ananiongoa, | الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ |
Wa Al-Ladhī Huwa Yuţ`imunī Wa Yasqīni  | 79. Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha. | وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ |
Wa 'Idhā Mariđtu Fahuwa Yashfīni  | 80. Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha. | وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ |
Wa Al-Ladhī Yumītunī Thumma Yuĥyīni  | 81. Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha. | وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ |
Wa Al-Ladhī 'Aţma`u 'An Yaghfira Lī Khaţī'atī Yawma Ad-Dīni  | 82. Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe
makosa yangu Siku ya Malipo. | وَالَّذِي أَطْمَعُ أَنْ يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ |
Rabbi Hab Lī Ĥukmāan Wa 'Alĥiqnī Biş-Şāliĥīna  | 83, Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe
na watendao mema. | رَبِّ هَبْ لِي حُكْما ً وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ |
Wa Aj`al Lī Lisāna Şidqin Fī Al-'Ākhirīna  | 84. Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao
kuja baadaye. | وَاجْعَلْ لِي لِسَانَ صِدْق ٍ فِي الآخِرِينَ |
Wa Aj`alnī Min Warathati Jannati An-Na`īmi  | 85. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za
neema. | وَاجْعَلْنِي مِنْ وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ |
Wa Aghfir Li'abī 'Innahu Kāna Mina Ađ-Đāllīna  | 86. Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa
miongoni mwa wapotovu. | وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّه ُُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ |
Wa Lā Tukhzinī Yawma Yub`athūna  | 87. Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa. | وَلاَ تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ |
Yawma Lā Yanfa`u Mālun Wa Lā Banūna  | 88. Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala
wana. | يَوْمَ لاَ يَنْفَعُ مَال ٌ وَلاَ بَنُونَ |
'Illā Man 'Atá Allāha Biqalbin Salīmin  | 89. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na
moyo safi. | إِلاَّ مَنْ أَتَى اللَّهَ بِقَلْب ٍ سَلِيم ٍ |
Wa 'Uzlifati Al-Jannatu Lilmuttaqīna  | 90. Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu. | وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ |
Wa Burrizati Al-Jaĥīmu Lilghāwīna  | 91. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu. | وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ |
Wa Qīla Lahum 'Ayna Mā Kuntum Ta`budūna  | 92. Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu | وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنْتُمْ تَعْبُدُونَ |
Min Dūni Allāhi Hal Yanşurūnakum 'Aw Yantaşirūna  | 93. Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni,
au wanajisaidia wenyewe? | مِنْ دُونِ اللَّهِ هَلْ يَنْصُرُونَكُمْ أَوْ يَنْتَصِرُونَ |
Fakubkibū Fīhā Hum Wa Al-Ghāwūna  | 94. Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu, | فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ |
Wa Junūdu 'Iblīsa 'Ajma`ūna  | 95. Na majeshi ya Ibilisi yote. | وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ |
Qālū Wa Hum Fīhā Yakhtaşimūna  | 96. Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo: | قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ |
Ta-Allāhi 'In Kunnā Lafī Đalālin Mubīnin  | 97. Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu
ulio dhaahiri, | تَاللَّهِ إِنْ كُنَّا لَفِي ضَلاَل ٍ مُبِين ٍ |
'Idh Nusawwīkum Birabbi Al-`Ālamīna  | 98. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa
walimwengu wote. | إِذْ نُسَوِّيكُمْ بِرَبِّ الْعَالَمِينَ |
Wa Mā 'Ađallanā 'Illā Al-Mujrimūna  | 99. Na hawakutupoteza ila wale wakosefu. | وَمَا أَضَلَّنَا إِلاَّ الْمُجْرِمُونَ |
Famā Lanā Min Shāfi`īna  | 100. Basi hatuna waombezi. | فَمَا لَنَا مِنْ شَافِعِينَ |
Wa Lā Şadīqin Ĥamīmin  | 101. Wala rafiki wa dhati. | وَلاَ صَدِيقٍ حَمِيم ٍ |
Falaw 'Anna Lanā Karratan Fanakūna Mina Al-Mu'uminīna  | 102. Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli
kuwa katika Waumini. | فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّة ً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ |
'Inna Fī Dhālika La'āyatan Wa Mā Kāna 'Aktharuhum Mu'uminīna  | 103. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi
wao hawakuwa wenye kuamini. | إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَة ً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُمْ مُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna Rabbaka Lahuwa Al-`Azīzu Ar-Raĥīmu  | 104. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye
nguvu Mwenye kurehemu. | وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ |
Kadhdhabat Qawmu Nūĥin Al-Mursalīna  | 105. Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume. | كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوح ٍ الْمُرْسَلِينَ |
'Idh Qāla Lahum 'Akhūhum Nūĥun 'Alā Tattaqūna  | 106. Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu? | إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلاَ تَتَّقُونَ |
'Innī Lakum Rasūlun 'Amīnun  | 107. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. | إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِين ٌ |
Fāttaqū Allāha Wa 'Aţī`ūni  | 108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini
mimi. | فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ |
Wa Mā 'As'alukum `Alayhi Min 'Ajrin 'In 'Ajrī 'Illā `Alá Rabbi Al-`Ālamīna  | 109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira
wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. | وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْر ٍ إِنْ أَجْرِي إِلاَّ عَلَى رَبِّ الْعَالَمِينَ |
Fāttaqū Allāha Wa 'Aţī`ūni  | 110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini
mimi. | فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ |
Qālū 'Anu'uminu Laka Wa Attaba`aka Al-'Ardhalūna  | 111. Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao
kufuata ni watu wa chini? | قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الأَرْذَلُونَ |
Qāla Wa Mā `Ilmī Bimā Kānū Ya`malūna  | 112. Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya? | قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ |
'In Ĥisābuhum 'Illā `Alá Rabbī Law Tash`urūna  | 113. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi,
laiti mngeli tambua! | إِنْ حِسَابُهُمْ إِلاَّ عَلَى رَبِّي لَوْ تَشْعُرُونَ |
Wa Mā 'Anā Biţāridi Al-Mu'uminīna  | 114. Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini. | وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ |
'In 'Anā 'Illā Nadhīrun Mubīnun  | 115. Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri
shaahiri. | إِنْ أَنَا إِلاَّ نَذِير ٌ مُبِين ٌ |
Qālū La'in Lam Tantahi Yā Nūĥu Latakūnanna Mina Al-Marjūmīna  | 116. Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila
ya shaka utapigwa mawe. | قَالُوا لَئِنْ لَمْ تَنْتَه ِِ يَانُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ |
Qāla Rabbi 'Inna Qawmī Kadhdhabūni  | 117. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu
wangu wamenikanusha. | قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ |
Fāftaĥ Baynī Wa Baynahum Fatĥāan Wa Najjinī Wa Man Ma`ī Mina Al-Mu'uminīna  | 118. Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu
yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini. | فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحا ً وَنَجِّنِي وَمَنْ مَعِي مِنَ الْمُؤْمِنِينَ |
Fa'anjaynāhu Wa Man Ma`ahu Fī Al-Fulki Al-Mashĥūni  | 119. Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa
pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni. | فَأَنجَيْنَاه ُُ وَمَنْ مَعَه ُُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ |
Thumma 'Aghraqnā Ba`du Al-Bāqīna  | 120. Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia. | ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ |
'Inna Fī Dhālika La'āyatan Wa Mā Kāna 'Aktharuhum Mu'uminīna  | 121. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si
wengi wao walio kuwa Waumini. | إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَة ً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُمْ مُؤْمِنِينَ |
Wa 'Inna Rabbaka Lahuwa Al-`Azīzu Ar-Raĥīmu  | 122. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye
nguvu Mwenye kurehemu. | وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ |
Kadhdhabat `Ādun Al-Mursalīna  | 123. Kina A'd waliwakanusha Mitume. | كَذَّبَتْ عَاد ٌ الْمُرْسَلِينَ |
'Idh Qāla Lahum 'Akhūhum Hūdun 'Alā Tattaqūna  | 124. Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu? | إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلاَ تَتَّقُونَ |
'Innī Lakum Rasūlun 'Amīnun  | 125. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu. | إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِين ٌ |
Fāttaqū Allāha Wa 'Aţī`ūni  | 126. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini
mimi. | فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ |
Wa Mā 'As'alukum `Alayhi Min 'Ajrin 'In 'Ajrī 'Illā `Alá Rabbi Al-`Ālamīna  | 127. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira
wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. | وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْر ٍ إِنْ أَجْرِي إِلاَّ عَلَى رَبِّ الْع |