Barā'atun Mina Allāhi Wa Rasūlihi 'Ilá Al-Ladhīna `Āhadttum Mina Al-Mushrikīna  | 1. Huku ni kujitoa Mwenyezi Mungu na Mtume wake
kwenye jukumu la maagano na mlio ahidiana nao katika washirikina. | بَرَاءة ٌ مِنَ اللَّهِ وَرَسُولِهِ~ِ إِلَى الَّذِينَ عَاهَدتُّمْ مِنَ الْمُشْرِكِينَ |
Fasīĥū Fī Al-'Arđi 'Arba`ata 'Ash/hurin Wa A`lamū 'Annakum Ghayru Mu`jizī Allāhi Wa 'Anna Allāha Mukhzī Al-Kāfirīna  | 2. Basi tembeeni katika nchi miezi mine, na jueni
kwamba nyinyi hamwezi kumshinda Mwenyezi Mung, na kwamba Mwenyezi Mungu
ndiye anaye wahizi makafiri. | فَسِيحُوا فِي الأَرْضِ أَرْبَعَةَ أَشْهُر ٍ وَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ غَيْرُ مُعْجِزِي اللَّهِ وَأَنَّ اللَّهَ مُخْزِي الْكَافِرِينَ |
Wa 'Adhānun Mina Allāhi Wa Rasūlihi 'Ilá An-Nāsi Yawma Al-Ĥajji Al-'Akbari 'Anna Allāha Barī'un Mina Al-Mushrikīna Wa Rasūluhu Fa'in Tubtum Fahuwa Khayrun Lakum Wa 'In Tawallaytum Fā`lamū 'Annakum Ghayru Mu`jizī Allāhi Wa Bashshiri Al-Ladhīna Kafarū Bi`adhābin 'Alīmin  | 3. Na ni tangazo kutokana na Mwenyezi Mungu na
Mtume wake kwa wote siku ya Hija Kubwa kwamba Mwenyezi Mungu na Mtume wake
hawana jukumu lolote kwa washirikina. Basi mkitubu itakuwa kheri kwenu,
na mkigeuka basi jueni kuwa nyinyi hamumshindi Mwenyezi Mungu. Na wabashirie
makafiri kuwa watapata adhabu chungu. | وَأَذَان ٌ مِنَ اللَّهِ وَرَسُولِهِ~ِ إِلَى النَّاسِ يَوْمَ الْحَجِّ الأَكْبَرِ أَنَّ اللَّهَ بَرِيء ٌ مِنَ الْمُشْرِكِينَ وَرَسُولُه ُُ فَإِنْ تُبْتُمْ فَهُوَ خَيْر ٌ لَكُمْ وَإِنْ تَوَلَّيْتُمْ فَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ غَيْرُ مُعْجِزِي اللَّهِ وَبَشِّرِ الَّذِينَ كَفَرُوا بِعَذَابٍ أَلِيم ٍ |
'Illā Al-Ladhīna `Āhadttum Mina Al-Mushrikīna Thumma Lam Yanquşūkum Shay'āan Wa Lam Yužāhirū `Alaykum 'Aĥadāan Fa'atimmū 'Ilayhim `Ahdahum 'Ilá Muddatihim 'Inna Allāha Yuĥibbu Al-Muttaqīna  | 4. Isipo kuwa washirikina ambao mliahidiana nao
kisha wasikupunguzieni chochote, wala hawakumsaidia yeyote dhidi yenu,
basi hao watimizieni ahadi yao mpaka muda wao. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda
wacha-Mungu. | إِلاَّ الَّذِينَ عَاهَدتُّمْ مِنَ الْمُشْرِكِينَ ثُمَّ لَمْ يَنقُصُوكُمْ شَيْئا ً وَلَمْ يُظَاهِرُوا عَلَيْكُمْ أَحَدا ً فَأَتِمُّوا إِلَيْهِمْ عَهْدَهُمْ إِلَى مُدَّتِهِمْ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْمُتَّقِينَ |
Fa'idhā Ansalakha Al-'Ash/huru Al-Ĥurumu Fāqtulū Al-Mushrikīna Ĥaythu Wajadtumūhum Wa Khudhūhum Wa Aĥşurūhum Wāq`udū Lahum Kulla Marşadin Fa'in Tābū Wa 'Aqāmū Aş-Şalāata Wa 'Ātaw Az-Zakāata Fakhallū Sabīlahum 'Inna Allāha Ghafūrun Raĥīmun  | 5. Na ikisha miezi mitukufu basi wauweni washirikina
popote mwakutapo, na washikeni na wazungukeni, na wavizieni katika kila
njia. Lakini wakitubu, wakashika Sala, na wakatoa Zaka, basi waachilieni.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. | فَإِذَا انسَلَخَ الأَشْهُرُ الْحُرُمُ فَاقْتُلُوا الْمُشْرِكِينَ حَيْثُ وَجَدْتُمُوهُمْ وَخُذُوهُمْ وَاحْصُرُوهُمْ وَاقْعُدُوا لَهُمْ كُلَّ مَرْصَد ٍ فَإِنْ تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلاَةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَخَلُّوا سَبِيلَهُمْ إِنَّ اللَّهَ غَفُور ٌ رَحِيم ٌ |
Wa 'In 'Aĥadun Mina Al-Mushrikīna Astajāraka Fa'ajirhu Ĥattá Yasma`a Kalāma Allāhi Thumma 'Abligh/hu Ma'manahu Dhālika Bi'annahum Qawmun Lā Ya`lamūna  | 6. Na ikiwa mmoja wapo katika washirikina akikuomba
ulinzi, basi mpe ulinzi apate kusikia maneno ya Mwenyezi Mungu. Kisha mfikishe
pahala pake pa amani. Haya ni kwa kuwa hao ni watu wasiojua kitu. | وَإِنْ أَحَد ٌ مِنَ الْمُشْرِكِينَ اسْتَجَارَكَ فَأَجِرْهُ حَتَّى يَسْمَعَ كَلاَمَ اللَّهِ ثُمَّ أَبْلِغْهُ مَأْمَنَه ُُ ذَلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْم ٌ لاَ يَعْلَمُونَ |
Kayfa Yakūnu Lilmushrikīna `Ahdun `Inda Allāhi Wa `Inda Rasūlihi 'Illā Al-Ladhīna `Āhadtum `Inda Al-Masjidi Al-Ĥarāmi Famā Astaqāmū Lakum Fāstaqīmū Lahum 'Inna Allāha Yuĥibbu Al-Muttaqīna  | 7. Itakuwaje iwepo ahadi na washirikina mbele ya
Mwenyezi Mungu na mbele ya Mtume wake, ila wale mlio ahidiana nao kwenye
Msikiti Mtakatifu? Basi maadamu wanakwenda nanyi sawa, nanyi pia nendeni
sawa nao. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wachamngu | كَيْفَ يَكُونُ لِلْمُشْرِكِينَ عَهْدٌ عِنْدَ اللَّهِ وَعِنْدَ رَسُولِهِ~ِ إِلاَّ الَّذِينَ عَاهَدْتُمْ عِنْدَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ فَمَا اسْتَقَامُوا لَكُمْ فَاسْتَقِيمُوا لَهُمْ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْمُتَّقِينَ |
Kayfa Wa 'In Yažharū `Alaykum Lā Yarqubū Fīkum 'Illāan Wa Lā Dhimmatan Yurđūnakum Bi'afwāhihim Wa Ta'bá Qulūbuhum Wa 'Aktharuhum Fāsiqūna  | 8. Itakuwaje! Nao wakikushindeni hawatazami kwenu
udugu wala ahadi. Wanakufurahisheni kwa midomo yao tu, na nyoyo zao zinakataa
hayo. Na wengi wao ni wapotovu. | كَيْفَ وَإِنْ يَظْهَرُوا عَلَيْكُمْ لاَ يَرْقُبُوا فِيكُمْ إِلاّ ً وَلاَ ذِمَّة ً يُرْضُونَكُمْ بِأَفْوَاهِهِمْ وَتَأْبَى قُلُوبُهُمْ وَأَكْثَرُهُمْ فَاسِقُونَ |
Ashtaraw Bi'āyāti Allāhi Thamanāan Qalīlāan Faşaddū `An Sabīlihi 'Innahum Sā'a Mā Kānū Ya`malūna  | 9. Wamenunua thamani ndogo kwa Ishara za Mwenyezi
Mungu, na wakazuilia watu na Njia yake. Hakika hao ni maovu waliyo kuwa
wakiyatenda. | اشْتَرَوْا بِآيَاتِ اللَّهِ ثَمَنا ً قَلِيلا ً فَصَدُّوا عَنْ سَبِيلِهِ~ِ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ |
Lā Yarqubūna Fī Mu'uminin 'Illāan Wa Lā Dhimmatan Wa 'Ūlā'ika Humu Al-Mu`tadūna  | 10. Hawatazami kwa Muumini udugu wala ahadi; basi
hao ndio warukao mipaka. | لاَ يَرْقُبُونَ فِي مُؤْمِن ٍ إِلاّ ً وَلاَ ذِمَّة ً وَأُوْلَائِكَ هُمُ الْمُعْتَدُونَ |
Fa'in Tābū Wa 'Aqāmū Aş-Şalāata Wa 'Ātaw Az-Zakāata Fa'ikhwānukum Fī Ad-Dīni Wa Nufaşşilu Al-'Āyāti Liqawmin Ya`lamūna  | 11. Basi wakitubu na wakashika Sala na wakatoa
Zaka, basi ni ndugu zenu katika Dini. Na tunazichambua Aya kwa watu wajuao. | فَإِنْ تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلاَةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَإِخْوَانُكُمْ فِي الدِّينِ وَنُفَصِّلُ الآيَاتِ لِقَوْم ٍ يَعْلَمُونَ |
Wa 'In Nakathū 'Aymānahum Min Ba`di `Ahdihim Wa Ţa`anū Fī Dīnikum Faqātilū 'A'immata Al-Kufri 'Innahum Lā 'Aymāna Lahum La`allahum Yantahūna  | 12. Na wakivunja viapo vyao baada ya kuahidi kwao,
na wakatukana Dini yenu, basi piganeni na waongozi wa ukafiri. Hakika hao
hawana viapo vya kweli. Huenda (kwa hayo) wakaacha. | وَإِنْ نَكَثُوا أَيْمَانَهُمْ مِنْ بَعْدِ عَهْدِهِمْ وَطَعَنُوا فِي دِينِكُمْ فَقَاتِلُوا أَئِمَّةَ الْكُفْرِ إِنَّهُمْ لاَ أَيْمَانَ لَهُمْ لَعَلَّهُمْ يَنتَهُونَ |
'Alā Tuqātilūna Qawmāan Nakathū 'Aymānahum Wa Hammū Bi'ikhrāji Ar-Rasūli Wa Hum Bada'ūkum 'Awwala Marratin 'Atakhshawnahum Fa-Allāhu 'Aĥaqqu 'An Takhshawhu 'In Kuntum Mu'uminīna  | 13. Je, hamtapigana na watu walio vunja viapo
vyao na wakawa na hamu ya kumfukuza Mtume, nao ndio walio kuanzeni mara
ya kwanza? Je, mnawaogopa? Basi Mwenyezi Mungu anastahiki zaidi mumwogope,
ikiwa nyinyi ni Waumini. | أَلاَ تُقَاتِلُونَ قَوْما ً نَكَثُوا أَيْمَانَهُمْ وَهَمُّوا بِإِخْرَاجِ الرَّسُولِ وَهُمْ بَدَءُوكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ أَتَخْشَوْنَهُمْ فَاللَّهُ أَحَقُّ أَنْ تَخْشَوْهُ إِنْ كُنتُمْ مُؤْمِنِينَ |
Qātilūhum Yu`adhdhibhumu Allāhu Bi'aydīkum Wa Yukhzihim Wa Yanşurkum `Alayhim Wa Yashfi Şudūra Qawmin Mu'uminīna  | 14. Piganeni nao, Mwenyezi Mungu awaadhibu kwa
mikono yenu, na awahizi na akunusuruni muwashinde, na avipoze vifua vya
kaumu ya Waumini, | قَاتِلُوهُمْ يُعَذِّبْهُمُ اللَّهُ بِأَيْدِيكُمْ وَيُخْزِهِمْ وَيَنْصُرْكُمْ عَلَيْهِمْ وَيَشْفِ صُدُورَ قَوْم ٍ مُؤْمِنِينَ |
Wa Yudh/hib Ghayža Qulūbihim Wa Yatūbu Allāhu `Alá Man Yashā'u Wa Allāhu `Alīmun Ĥakīmun  | 15. Na aondoe hasira ya nyoyo zao. Na Mwenyezi
Mungu humkubalia toba ya amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye
hikima. | وَيُذْهِبْ غَيْظَ قُلُوبِهِمْ وَيَتُوبُ اللَّهُ عَلَى مَنْ يَشَاءُ وَاللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيم ٌ |
'Am Ĥasibtum 'An Tutrakū Wa Lammā Ya`lami Allāhu Al-Ladhīna Jāhadū Minkum Wa Lam Yattakhidhū Min Dūni Allāhi Wa Lā Rasūlihi Wa Lā Al-Mu'uminīna Walījatan Wa Allāhu Khabīrun Bimā Ta`malūna  | 16. Je, mlidhani kuwa mtaachwa tu, bila ya Mwenyezi
Mungu kuwajuulisha wale walio pigana Jihadi kati yenu, na wala hawakumfanya
mwendani wao isipo kuwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Waumini wenziwe?
Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za yote mnayo yatenda. | أَمْ حَسِبْتُمْ أَنْ تُتْرَكُوا وَلَمَّا يَعْلَمِ اللَّهُ الَّذِينَ جَاهَدُوا مِنْكُمْ وَلَمْ يَتَّخِذُوا مِنْ دُونِ اللَّهِ وَلاَ رَسُولِه ِِ وَلاَ الْمُؤْمِنِينَ وَلِيجَة ً وَاللَّهُ خَبِير ٌ بِمَا تَعْمَلُونَ |
Mā Kāna Lilmushrikīna 'An Ya`murū Masājida Allāhi Shāhidīna `Alá 'Anfusihim Bil-Kufri 'Ūlā'ika Ĥabiţat 'A`māluhum Wa Fī An-Nāri Hum Khālidūna  | 17. Haiwi kuwa makafiri ndio waamirishe misikiti
ya Mwenyezi Mungu, hali wanajishuhudishia wenyewe ukafiri. Hao ndio ambao
vitendo vyao vimeharibika, na katika Moto watadumu. | مَا كَانَ لِلْمُشْرِكِينَ أَنْ يَعْمُرُوا مَسَاجِدَ اللَّهِ شَاهِدِينَ عَلَى أَنفُسِهِمْ بِالْكُفْرِ أُوْلَائِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ وَفِي النَّارِ هُمْ خَالِدُونَ |
'Innamā Ya`muru Masājida Allāhi Man 'Āmana Billāhi Wa Al-Yawmi Al-'Ākhiri Wa 'Aqāma Aş-Şalāata Wa 'Ātá Az-Zakāata Wa Lam Yakhsha 'Illā Allāha Fa`asá 'Ūlā'ika 'An Yakūnū Mina Al-Muhtadīna  | 18. Hakika wanao amirisha misikiti ya Mwenyezi
Mungu ni wale wanao muamini Mwenyezi Mungu, na Siku ya Mwisho, na wakashika
Sala, na wakatoa Zaka, na wala hawamchi ila Mwenyezi Mungu. Basi huenda
hao wakawa katika waongofu. | إِنَّمَا يَعْمُرُ مَسَاجِدَ اللَّهِ مَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ وَأَقَامَ الصَّلاَةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَلَمْ يَخْشَ إِلاَّ اللَّهَ فَعَسَى أُوْلَائِكَ أَنْ يَكُونُوا مِنَ الْمُهْتَدِينَ |
'Aja`altum Siqāyata Al-Ĥājji Wa `Imārata Al-Masjidi Al-Ĥarāmi Kaman 'Āmana Billāhi Wa Al-Yawmi Al-'Ākhiri Wa Jāhada Fī Sabīli Allāhi Lā Yastawūna `Inda Allāhi Wa Allāhu Lā Yahdī Al-Qawma Až-Žālimīna  | 19. Je, mnafanya kuwanywesha maji Mahujaji na
kuamirisha Msikiti Mtakatifu ni sawa na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu,
na Siku ya Mwisho, na akapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi
sawa mbele ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu. | أَجَعَلْتُمْ سِقَايَةَ الْحَاجِّ وَعِمَارَةَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ كَمَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ وَجَاهَدَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ لاَ يَسْتَوُونَ عِنْدَ اللَّهِ وَاللَّهُ لاَ يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ |
Al-Ladhīna 'Āmanū Wa Hājarū Wa Jāhadū Fī Sabīli Allāhi Bi'amwālihim Wa 'Anfusihim 'A`žamu Darajatan `Inda Allāhi Wa 'Ūlā'ika Humu Al-Fā'izūna  | 20. Wale walio amini, na wakahama, na wakapigana
Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao, hao wana
cheo kikubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hao ndio wenye kufuzu. | الَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ أَعْظَمُ دَرَجَةً عِنْدَ اللَّهِ وَأُوْلَائِكَ هُمُ الْفَائِزُونَ |
Yubashshiruhum Rabbuhum Biraĥmatin Minhu Wa Riđwānin Wa Jannātin Lahum Fīhā Na`īmun Muqīmun  | 21. Mola wao Mlezi anawabashiria rehema zitokazo
kwake, na radhi, na Bustani ambazo humo watapata neema za kudumu. | يُبَشِّرُهُمْ رَبُّهُمْ بِرَحْمَة ٍ مِنْهُ وَرِضْوَان ٍ وَجَنَّات ٍ لَهُمْ فِيهَا نَعِيم ٌ مُقِيم ٌ |
Khālidīna Fīhā 'Abadāan 'Inna Allāha `Indahu 'Ajrun `Ažīmun  | 22. Watadumu humo milele. Hakika kwa Mwenyezi
Mungu yapo malipo makubwa. | خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدا ً إِنَّ اللَّهَ عِنْدَهُ~ُ أَجْرٌ عَظِيم ٌ |
Yā 'Ayyuhā Al-Ladhīna 'Āmanū Lā Tattakhidhū 'Ābā'akum Wa 'Ikhwānakum 'Awliyā'a 'Ini Astaĥabbū Al-Kufra `Alá Al-'Īmāni Wa Man Yatawallahum Minkum Fa'ūlā'ika Humu Až-Žālimūna  | 23. Enyi mlio amini! Msiwafanye baba zenu na ndugu
zenu kuwa vipenzi vyenu ikiwa wanastahabu ukafiri kuliko Imani. Na katika
nyinyi atakaye wafanya hao ndio vipenzi vyake, basi hao ndio madhaalimu. | يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لاَ تَتَّخِذُوا آبَاءَكُمْ وَإِخْوَانَكُمْ أَوْلِيَاءَ إِنِ اسْتَحَبُّوا الْكُفْرَ عَلَى الإِيمَانِ وَمَنْ يَتَوَلَّهُمْ مِنْكُمْ فَأُوْلَائِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ |
Qul 'In Kāna 'Ābā'uukum Wa 'Abnā'uukum Wa 'Ikhwānukum Wa 'Azwājukum Wa `Ashīratukum Wa 'Amwālun Aqtaraftumūhā Wa Tijāratun Takhshawna Kasādahā Wa Masākinu Tarđawnahā 'Aĥabba 'Ilaykum Mina Allāhi Wa Rasūlihi Wa Jihādin Fī Sabīlihi Fatarabbaşū Ĥattá Ya'tiya Allāhu Bi'amrihi Wa Allāhu Lā Yahdī Al-Qawma Al-Fāsiqīna  | 24. Sema: Ikiwa baba zenu, na wenenu, na ndugu
zenu, na wake zenu, na jamaa zenu, na mali mliyo yachuma, na biashara mnazo
ogopa kuharibika, na majumba mnayo yapenda, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko
Mwenyezi Mungu na Mtume wake na Jihadi katika Njia yake, basi ngojeni mpaka
Mwenyezi Mungu alete amri yake. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wapotovu. | قُلْ إِنْ كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَال ٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَة ٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُمْ مِنَ اللَّهِ وَرَسُولِه ِِ وَجِهَاد ٍ فِي سَبِيلِه ِِ فَتَرَبَّصُوا حَتَّى يَأْتِيَ اللَّهُ بِأَمْرِه ِِ وَاللَّهُ لاَ يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ |
Laqad Naşarakumu Allāhu Fī Mawāţina Kathīratin Wa Yawma Ĥunaynin 'Idh 'A`jabatkum Kathratukum Falam Tughni `Ankum Shay'āan Wa Đāqat `Alaykumu Al-'Arđu Bimā Raĥubat Thumma Wallaytum Mudbirīna  | 25. Hakika Mwenyezi Mungu amekunusuruni katika
mapigano mengi, na siku ya Hunayni ambapo wingi wenu ulikupandisheni kichwa,
lakini haukukufaeni kitu. Na ardhi ikawa dhiki kwenu juu ya upana wake.
Kisha mkageuka mkarudi nyuma. | لَقَدْ نَصَرَكُمُ اللَّهُ فِي مَوَاطِنَ كَثِيرَة ٍ وَيَوْمَ حُنَيْن ٍ إِذْ أَعْجَبَتْكُمْ كَثْرَتُكُمْ فَلَمْ تُغْنِ عَنْكُمْ شَيْئا ً وَضَاقَتْ عَلَيْكُمُ الأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ ثُمَّ وَلَّيْتُمْ مُدْبِرِينَ |
Thumma 'Anzala Allāhu Sakīnatahu `Alá Rasūlihi Wa `Alá Al-Mu'uminīna Wa 'Anzala Junūdāan Lam Tarawhā Wa `Adhdhaba Al-Ladhīna Kafarū Wa Dhalika Jazā'u Al-Kāfirīna  | 26. Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake
juu ya Mtume wake na juu ya Waumini. Na akateremsha majeshi ambayo hamkuyaona,
na akawaadhibu wale walio kufuru. Na hayo ndiyo malipo ya makafiri. | ثُمَّ أَنزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَه ُُ عَلَى رَسُولِه ِِ وَعَلَى الْمُؤْمِنِينَ وَأَنزَلَ جُنُودا ً لَمْ تَرَوْهَا وَعَذَّبَ الَّذِينَ كَفَرُوا وَذَلِكَ جَزَاءُ الْكَافِرِينَ |
Thumma Yatūbu Allāhu Min Ba`di Dhālika `Alá Man Yashā'u Wa Allāhu Ghafūrun Raĥīmun  | 27. Kisha baada ya hayo Mwenyezi Mungu atawasamehe
awatakao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. | ثُمَّ يَتُوبُ اللَّهُ مِنْ بَعْدِ ذَلِكَ عَلَى مَنْ يَشَاءُ وَاللَّهُ غَفُور ٌ رَحِيم ٌ |
Yā 'Ayyuhā Al-Ladhīna 'Āmanū 'Innamā Al-Mushrikūna Najasun Falā Yaqrabū Al-Masjida Al-Ĥarāma Ba`da `Āmihim Hādhā Wa 'In Khiftum `Aylatan Fasawfa Yughnīkumu Allāhu Min Fađlihi 'In Shā'a 'Inna Allāha `Alīmun Ĥakīmun  | 28. Enyi mlio amini! Hakika washirikina ni najsi,
kwa hivyo wasiukaribie Msikiti Mtakatifu baada ya mwaka wao huu. Na ikiwa
mnakhofia umasikini, basi Mwenyezi Mungu atakutajirisheni kwa fadhila yake
akipenda. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima. | يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَس ٌ فَلاَ يَقْرَبُوا الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ بَعْدَ عَامِهِمْ هَذَا وَإِنْ خِفْتُمْ عَيْلَة ً فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ اللَّهُ مِنْ فَضْلِهِ~ِ إِنْ شَاءَ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ حَكِيم ٌ |
Qātilū Al-Ladhīna Lā Yu'uminūna Billāhi Wa Lā Bil-Yawmi Al-'Ākhiri Wa Lā Yuĥarrimūna Mā Ĥarrama Allāhu Wa Rasūluhu Wa Lā Yadīnūna Dīna Al-Ĥaqqi Mina Al-Ladhīna 'Ūtū Al-Kitāba Ĥattá Yu`ţū Al-Jizyata `An Yadin Wa Hum Şāghirūna  | 29. Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala
Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi Mungu na Mtume,
wala hawashiki Dini ya Haki, miongoni mwa walio pewa Kitabu, mpaka watoe
kodi kwa khiari yao, hali wamet'ii. | قَاتِلُوا الَّذِينَ لاَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَلاَ بِالْيَوْمِ الآخِرِ وَلاَ يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ اللَّهُ وَرَسُولُه ُُ وَلاَ يَدِينُونَ دِينَ الْحَقِّ مِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ حَتَّى يُعْطُوا الْجِزْيَةَ عَنْ يَد ٍ وَهُمْ صَاغِرُونَ |
Wa Qālati Al-Yahūdu `Uzayrun Abnu Allāhi Wa Qālati An-Naşārá Al-Masīĥu Abnu Allāhi Dhālika Qawluhum Bi'afwāhihim Yuđāhi'ūna Qawla Al-Ladhīna Kafarū Min Qablu Qātalahumu Allāhu 'Anná Yu'ufakūna  | 30. Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu.
Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa
vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu
awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa! | وَقَالَتِ الْيَهُودُ عُزَيْر ٌ ابْنُ اللَّهِ وَقَالَتِ النَّصَارَى الْمَسِيحُ ابْنُ اللَّهِ ذَلِكَ قَوْلُهُمْ بِأَفْوَاهِهِمْ يُضَاهِئُونَ قَوْلَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ قَبْلُ قَاتَلَهُمُ اللَّهُ أَنَّى يُؤْفَكُونَ |
Attakhadhū 'Aĥbārahum Wa Ruhbānahum 'Arbābāan Min Dūni Allāhi Wa Al-Masīĥa Abna Maryama Wa Mā 'Umirū 'Illā Liya`budū 'Ilahāan Wāĥidāan Lā 'Ilāha 'Illā Huwa Subĥānahu `Ammā Yushrikūna  | 31. Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa
ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu, na pia Masihi bin Maryamu. Na wala
hawakuamrishwa isipo kuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye.
Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayo mshirikisha nayo. | اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابا ً مِنْ دُونِ اللَّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلاَّ لِيَعْبُدُوا إِلَها ً وَاحِدا ً لاَ إِلَهَ~َ إِلاَّ هُوَ سُبْحَانَه ُُ عَمَّا يُشْرِكُونَ |
Yurīdūna 'An Yuţfi'ū Nūra Allāhi Bi'afwāhihim Wa Ya'bá Allāhu 'Illā 'An Yutimma Nūrahu Wa Law Kariha Al-Kāfirūna  | 32. Wanataka kuizima Nuru ya Mwenyezi Mungu kwa
vinywa vyao, na Mwenyezi Mungu anakataa ila aitimize Nuru yake ijapo kuwa
makafiri watachukia. | يُرِيدُونَ أَنْ يُطْفِئُوا نُورَ اللَّهِ بِأَفْوَاهِهِمْ وَيَأْبَى اللَّهُ إِلاَّ أَنْ يُتِمَّ نُورَه ُُ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ |
Huwa Al-Ladhī 'Arsala Rasūlahu Bil-Hudá Wa Dīni Al-Ĥaqqi Liyužhirahu `Alá Ad-Dīni Kullihi Wa Law Kariha Al-Mushrikūna  | 33. Yeye ndiye aliye mtuma Mtume wake kwa uwongofu
na Dini ya Haki ipate kushinda dini zote, ijapo kuwa washirikina watachukia. | هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَه ُُ بِالْهُدَى وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَه ُُ عَلَى الدِّينِ كُلِّه ِِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ |
Yā 'Ayyuhā Al-Ladhīna 'Āmanū 'Inna Kathīrāan Mina Al-'Aĥbāri Wa Ar-Ruhbāni Laya'kulūna 'Amwāla An-Nāsi Bil-Bāţili Wa Yaşuddūna `An Sabīli Allāhi Wa Al-Ladhīna Yaknizūna Adh-Dhahaba Wa Al-Fiđđata Wa Lā Yunfiqūnahā Fī Sabīli Allāhi Fabashshirhum Bi`adhābin 'Alīmin  | 34. Enyi mlio amini! Hakika wengi katika makuhani
na wamonaki wanakula mali za watu kwa baat'ili na wanazuilia Njia ya Mwenyezi
Mungu. Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia
ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya adhabu iliyo chungu. | يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ كَثِيرا ً مِنَ الأَحْبَارِ وَالرُّهْبَانِ لَيَأْكُلُونَ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ وَيَصُدُّونَ عَنْ سَبِيلِ اللَّهِ وَالَّذِينَ يَكْنِزُونَ الذَّهَبَ وَالْفِضَّةَ وَلاَ يُنفِقُونَهَا فِي سَبِيلِ اللَّهِ فَبَشِّرْهُمْ بِعَذَابٍ أَلِيم ٍ |
Yawma Yuĥmá `Alayhā Fī Nāri Jahannama Fatukwá Bihā Jibāhuhum Wa Junūbuhum Wa Žuhūruhum Hādhā Mā Kanaztum Li'nfusikum Fadhūqū Mā Kuntum Taknizūna  | 35. Siku zitapo tiwa moto katika Moto wa Jahannamu,
na kwazo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, wakaambiwa:
Haya ndiyo mlio jilimbikia nafsi zenu, basi onjeni mliyo kuwa mkilimbika. | يَوْمَ يُحْمَى عَلَيْهَا فِي نَارِ جَهَنَّمَ فَتُكْوَى بِهَا جِبَاهُهُمْ وَجُنُوبُهُمْ وَظُهُورُهُمْ هَذَا مَا كَنَزْتُمْ لِأنفُسِكُمْ فَذُوقُوا مَا كُنتُمْ تَكْنِزُونَ |
'Inna `Iddata Ash-Shuhūri `Inda Allāhi Athnā `Ashara Shahrāan Fī Kitābi Allāhi Yawma Khalaqa As-Samāwāti Wa Al-'Arđa Minhā 'Arba`atun Ĥurumun Dhālika Ad-Dīnu Al-Qayyimu Falā Tažlimū Fīhinna 'Anfusakum Wa Qātilū Al-Mushrikīna Kāffatan Kamā Yuqātilūnakum Kāffatan Wa A`lamū 'Anna Allāha Ma`a Al-Muttaqīna  | 36. Hakika idadi ya miezi kwa Mwenyezi Mungu ni
miezi kumi na mbili katika hukumu ya Mwenyezi Mungu tangu alipo umba mbingu
na ardhi. Katika hiyo iko mine mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa.
Basi msidhulumu nafsi zenu humo. Na piganeni na washirikina wote kama wao
wnavyo pigana nanyi nyote. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu. | إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِنْدَ اللَّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرا ً فِي كِتَابِ اللَّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُم ٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلاَ تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنْفُسَكُمْ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّة ً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّة ً وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ |
'Innamā An-Nasī'u Ziyādatun Fī Al-Kufri Yuđallu Bihi Al-Ladhīna Kafarū Yuĥillūnahu `Āmāan Wa Yuĥarrimūnahu `Āmāan Liyuwāţi'ū `Iddata Mā Ĥarrama Allāhu Fayuĥillū Mā Ĥarrama Allāhu Zuyyina Lahum Sū'u 'A`mālihim Wa Allāhu Lā Yahdī Al-Qawma Al-Kāfirīna  | 37. Bila ya shaka kuakhirisha (miezi) ni kuzidi
katika kukufuru; kwa hayo hupotezwa walio kufuru. Wanauhalalisha mwaka
mmoja na kuharimisha mwaka mwingine, ili wafanye kuwa sawa idadi ya ile
(miezi) aliyo itukuza Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo huhalalisha alivyo viharimisha
Mwenyezi Mungu. Wamepambiwa ubaya wa vitendo vyao hivi. Na Mwenyezi Mungu
hawaongoi watu makafiri. | إِنَّمَا النَّسِيءُ زِيَادَة ٌ فِي الْكُفْرِ يُضَلُّ بِهِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُحِلُّونَه ُُ عَاما ً وَيُحَرِّمُونَه ُُ عَاما ً لِيُوَاطِئُوا عِدَّةَ مَا حَرَّمَ اللَّهُ فَيُحِلُّوا مَا حَرَّمَ اللَّهُ زُيِّنَ لَهُمْ سُوءُ أَعْمَالِهِمْ وَاللَّهُ لاَ يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ |
Yā 'Ayyuhā Al-Ladhīna 'Āmanū Mā Lakum 'Idhā Qīla Lakum Anfirū Fī Sabīli Allāhi Aththāqaltum 'Ilá Al-'Arđi 'Arađītum Bil-Ĥayāati Ad-Dunyā Mina Al-'Ākhirati Famā Matā`u Al-Ĥayāati Ad-Dunyā Fī Al-'Ākhirati 'Illā Qalīlun  | 38. Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni
katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia
maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha
na ya Akhera ni chache. | يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمْ انفِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الأَرْضِ أَرَضِيتُمْ بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنَ الآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الآخِرَةِ إِلاَّ قَلِيل ٌ |
'Illā Tanfirū Yu`adhdhibkum `Adhābāan 'Alīmāan Wa Yastabdil Qawmāan Ghayrakum Wa Lā Tađurrūhu Shay'āan Wa Allāhu `Alá Kulli Shay'in Qadīrun  | 39. Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu,
na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi
Mungu ni Muweza wa kila kitu. | إِلاَّ تَنفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَاباً أَلِيما ً وَيَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ وَلاَ تَضُرُّوه ُُ شَيْئا ً وَاللَّهُ عَلَى كُلِّ شَيْء ٍ قَدِير ٌ |
'Illā Tanşurūhu Faqad Naşarahu Allāhu 'Idh 'Akhrajahu Al-Ladhīna Kafarū Thāniya Athnayni 'Idh Humā Fī Al-Ghāri 'Idh Yaqūlu Lişāĥibihi Lā Taĥzan 'Inna Allāha Ma`anā Fa'anzala Allāhu Sakīnatahu `Alayhi Wa 'Ayyadahu Bijunūdin Lam Tarawhā Wa Ja`ala Kalimata Al-Ladhīna Kafarū As-Suflá Wa Kalimatu Allāhi Hiya Al-`Ulyā Wa Allāhu `Azīzun Ĥakīmun  | 40. Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume, basi Mwenyezi
Mungu alikwisha mnusuru walipo mtoa walio kufuru, naye ni wa pili katika
wawili walipo kuwa katika pango, naye akamwambia sahibu yake: Usihuzunike.
Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi. Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu
wake, na akamuunga mkono kwa majeshi msiyo yaona, na akalifanya neno la
walio kufuru kuwa chini, na Neno la Mwenyezi Mungu kuwa ndilo juu. Na Mwenyezi
Mungu ndiye Mwenye nguvu Mwenye hikima. | إِلاَّ تَنصُرُوه ُُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لاَ تَحْزَنْ إِنَّ اللَّهَ مَعَنَا فَأَنزَلَ اللَّهُ سَكِينَتَه ُُ عَلَيْهِ وَأَيَّدَه ُُ بِجُنُود ٍ لَمْ تَرَوْهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَى وَكَلِمَةُ اللَّهِ هِيَ الْعُلْيَا وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيم ٌ |
Anfirū Khifāfāan Wa Thiqālāan Wa Jāhidū Bi'amwālikum Wa 'Anfusikum Fī Sabīli Allāhi Dhālikum Khayrun Lakum 'In Kuntum Ta`lamūna  | 41. Nendeni mtoke, mkiwa wepesi na wazito, na
piganeni Jihadi kwa mali yenu na nafsi zenu katika Njia ya Mwenyezi Mungu.
Haya ni kheri kwenu mkiwa mnajua. | انفِرُوا خِفَافا ً وَثِقَالا ً وَجَاهِدُوا بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ذَلِكُمْ خَيْر ٌ لَكُمْ إِنْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ |
Law Kāna `Arađāan Qarībāan Wa Safarāan Qāşidāan Lāttaba`ūka Wa Lakin Ba`udat `Alayhimu Ash-Shuqqatu Wa Sayaĥlifūna Billāhi Law Astaţa`nā Lakharajnā Ma`akum Yuhlikūna 'Anfusahum Wa Allāhu Ya`lamu 'Innahum Lakādhibūna  | 42. Na lau ingeli kuwa ipo faida ya papo kwa papo,
na safari yenyewe ni fupi, wangeli kufuata. Lakini wameona ni mbali na
kuna mashaka. Nao wataapa kwa Mwenyezi Mungu: Tungeli weza bila ya shaka
tungeli toka pamoja nanyi. Wanaziangamiza nafsi zao. Na Mwenyezi Mungu
anajua kuwa hakika hao ni waongo. | لَوْ كَانَ عَرَضا ً قَرِيبا ً وَسَفَرا ً قَاصِدا ً لاَتَّبَعُوكَ وَلَكِنْ بَعُدَتْ عَلَيْهِمُ الشُّقَّةُ وَسَيَحْلِفُونَ بِاللَّهِ لَوْ اسْتَطَعْنَا لَخَرَجْنَا مَعَكُمْ يُهْلِكُونَ أَنفُسَهُمْ وَاللَّهُ يَعْلَمُ إِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ |
`Afā Allāhu `Anka Lima 'Adhinta Lahum Ĥattá Yatabayyana Laka Al-Ladhīna Şadaqū Wa Ta`lama Al-Kādhibīna  | 43. Mwenyezi Mungu amekusamehe! Kwa nini ukawapa
ruhusa kabla ya kubainikia kwako wanao sema kweli, na ukawajua waongo? | عَفَا اللَّهُ عَنْكَ لِمَ أَذِنتَ لَهُمْ حَتَّى يَتَبَيَّنَ لَكَ الَّذِينَ صَدَقُوا وَتَعْلَمَ الْكَاذِبِينَ |
Lā Yasta'dhinuka Al-Ladhīna Yu'uminūna Billāhi Wa Al-Yawmi Al-'Ākhiri 'An Yujāhidū Bi'amwālihim Wa 'Anfusihim Wa Allāhu `Alīmun Bil-Muttaqīna  | 44. Hawatakuomba ruhusa wale wanao muamini Mwenyezi
Mungu na Siku ya Mwisho, wasende kupigana Jihadi kwa mali yao na nafsi
zao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwajua wachamngu. | لاَ يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ أَنْ يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ وَاللَّهُ عَلِيم ٌ بِالْمُتَّقِينَ |
'Innamā Yasta'dhinuka Al-Ladhīna Lā Yu'uminūna Billāhi Wa Al-Yawmi Al-'Ākhiri Wa Artābat Qulūbuhum Fahum Fī Raybihim Yataraddadūna  | 45. Wasio muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho
na nyoyo zao zikatia shaka, hao tu ndio wanao kutaka ruhusa. Basi hao wanataradadi
katika shaka zao. | إِنَّمَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ لاَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ وَارْتَابَتْ قُلُوبُهُمْ فَهُمْ فِي رَيْبِهِمْ يَتَرَدَّدُونَ |
Wa Law 'Arādū Al-Khurūja La'a`addū Lahu `Uddatan Wa Lakin Kariha Allāhu Anbi`āthahum Fathabbaţahum Wa Qīla Aq`udū Ma`a Al-Qā`idīna  | 46. Na ingeli kuwa kweli walitaka kutoka bila
ya shaka wangeli jiandalia maandalio, lakini Mwenyezi Mungu kachukia kutoka
kwao, na kwa hivyo akawazuia na ikasemwa: Kaeni pamoja na wanao kaa! | وَلَوْ أَرَادُوا الْخُرُوجَ لَأَعَدُّوا لَه ُُ عُدَّة ً وَلَكِنْ كَرِهَ اللَّهُ انْبِعَاثَهُمْ فَثَبَّطَهُمْ وَقِيلَ اقْعُدُوا مَعَ الْقَاعِدِينَ |
|