10. Enyi mlio amini! Wakikujilieni wanawake Waumini
walio hama, basi wafanyieni mtihani - Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua
zaidi Imani yao. Mkiwa mnawajua kuwa ni Waumini basi msiwarudishe kwa makafiri.
Wanawake hao si halali kwa hao makafiri, wala hao makafiri hawahalalikii
wanawake Waumini. Na wapeni hao wanaume mahari walio toa. Wala hapana makosa
kwenu kuwaoa mkiwapa mahari yao. Wala msiwaweke wanawake makafiri katika
kifungo cha ndoa zenu. Na takeni mlicho kitoa, na wao watake walicho kitoa.
Hiyo ndiyo hukumu ya Mwenyezi Mungu anayo kuhukumuni. Na Mwenyezi Mungu
ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.
|