Yā 'Ayyuhā Al-Ladhīna 'Āmanū 'Idhā Jā'akum Al-Mu'uminātu Muhājirātinmtaĥinūhunna Allāhu 'A`lamu Bi'īmānihinna Fa'in `Alimtumūhunna Mu'uminātin Falā Tarji`ūhunna 'Ilaá Al-Kuffāri Lā Hunna Ĥillun Lahum Wa Lā Hum Yaĥillūna Lahunna Wa 'Ātūhum Mā 'Anfaqū Wa Lā Junāĥa `Alaykum 'An Tankiĥūhunna 'Idhā 'Ātaytumūhunna 'Ujūrahunna Wa Lā Tumsikū Bi`işami Al-Kawāfiri Wa As'alū Mā 'Anfaqtum Wa Līas'alū Mā 'Anfaqū Dhālikum Ĥukmu Allāhi Yaĥkumu Baynakum Wa Allāhu `Alīmun Ĥakīmun (Al-Mumtaĥanah: 10).

<< Previous Sūrah    <Previous Ayah    Next Ayah >    Next Sūrah >>    Recite again    
10. Enyi mlio amini! Wakikujilieni wanawake Waumini walio hama, basi wafanyieni mtihani - Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujua zaidi Imani yao. Mkiwa mnawajua kuwa ni Waumini basi msiwarudishe kwa makafiri. Wanawake hao si halali kwa hao makafiri, wala hao makafiri hawahalalikii wanawake Waumini. Na wapeni hao wanaume mahari walio toa. Wala hapana makosa kwenu kuwaoa mkiwapa mahari yao. Wala msiwaweke wanawake makafiri katika kifungo cha ndoa zenu. Na takeni mlicho kitoa, na wao watake walicho kitoa. Hiyo ndiyo hukumu ya Mwenyezi Mungu anayo kuhukumuni. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.