33. Na wajizuilie na machafu wale wasio pata
cha kuolea, mpaka Mwenyezi Mungu awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao
taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki,
basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Mwenyezi
Mungu aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi vyenu kufanya zina kwa
ajili ya kutafuta pato la maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujihishimu.
Na atakaye walazimisha basi Mwenyezi Mungu baada ya kulazimishwa kwao huko,
atawasamehe, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
|