Wa`ada Allāhu Al-Mu'uminīna Wa Al-Mu'umināti Jannātin Tajrī Min Taĥtihā Al-'Anhāru Khālidīna Fīhā Wa Masākina Ţayyibatan Fī Jannāti `Adnin Wa Riđwānun Mina Allāhi 'Akbaru Dhālika Huwa Al-Fawzu Al-`Ažīmu (At-Tawbah: 72). |
| 72. Mwenyezi Mungu amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na makaazi mema katika Bustani za kudumu, na Radhi za Mwenyezi Mungu ndio kubwa kuliko yote. Huko ndiko kufuzu kukubwa. |