93. Nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye mzuliya
uwongo Mwenyezi Mungu, au anaye sema: Mimi nimeletewa wahyi; na hali hakuletewa
wahyi wowote. Na yule anaye sema: Nitateremsha kama alivyo teremsha Mwenyezi
Mungu. Na lau ungeli waona madhaalimu wanavyo kuwa katika mahangaiko ya
mauti, na Malaika wamewanyooshea mikono wakiwambia: Zitoeni roho zenu!
Leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyasema juu ya
Mwenyezi Mungu yasiyo ya haki, na mlivyo kuwa mkizifanyia kiburi Ishara
zake.
|