110. Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa
bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo
kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani.
Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza
udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa
idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na
ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili
ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao:
Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!
|