95. Enyi mlio amini! Msiue wanyama wa kuwinda
nanyi mmeharimia katika Hija. Na miongoni mwenu atakaye muuwa makusudi,
basi malipo yake yatakuwa kwa kuchinja kilicho sawa na alicho kiuwa, katika
mifugo, kama wanavyo hukumu waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama huyo
apelekwe kwenye Al Kaaba, au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini; au badala
ya hayo ni kufunga, ili aonje ubaya wa jambo lake hili. Mwenyezi Mungu
amekwisha yafuta yaliyo pita; lakini atakaye fanya tena Mwenyezi Mungu
atampa adhabu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye kuadhibu.
|