48. Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu
hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu na kuyalinda.
Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate
matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia. Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea
sharia yake na njia yake. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni
nyote umma mmoja, lakini ni kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni
kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja
kuwaambieni yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.
|