41. Ewe Mtume! Wasikuhuzunishe wa fanyao haraka
kukufuru, miongoni mwa wanao sema kwa vinywa vyao: Tumeamini, na hali nyoyo
zao hazikuamini, na miongoni mwa Mayahudi, wanao sikiliza kwa ajili ya
uwongo, wanao sikiliza kwa ajili ya watu wengine wasio kufikia. Wao huyabadilisha
maneno kutoka pahala pake. Wanasema: Mkipewa haya basi yashikeni, na msipo
pewa haya tahadharini. Na mtu ambaye Mwenyezi Mungu anataka kumfitini huwezi
kuwa na madaraka naye mbele ya Mwenyezi Mungu. Hao ndio ambao Mwenyezi
Mungu hataki kuzitakasa nyoyo zao. Watakuwa na hizaya duniani, na Akhera
watakuwa na adhabu kubwa.
|