3. Mmeharimishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya
nguruwe, na mnyama aliye chinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na aliye
kufa kwa kunyongeka koo, na aliye kufa kwa kupigwa, na aliye kufa kwa kuanguka,
na aliye kufa kwa kupigwa pembe, aliye liwa na mnyama, ila mkimdiriki kumchinja.
Na pia ni haramu kula nyama aliye chinjiwa masanamu. Na ni haramu kupiga
ramli. Hayo yote ni upotovu. Leo walio kufuru wamekata tamaa na Dini yenu;
basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi. Leo nimekukamiliishieni Dini yenu,
na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini.
Na mwenye kushurutishwa na njaa, bila ya kupendelea dhambi, basi hakika
Mwenyezi Mungu ni Msamehevu na Mwenye kurehemu.
|