2. Enyi mlio amini! Msivunje hishima ya alama ya
Dini ya Mwenyezi Mungu wala mwezi mtakatifu, wala wanyama wanao pelekwa
Makka kuchinjwa, wala vigwe vyao, wala wanao elekea kwendea Nyumba Takatifu,
wakitafuta fadhila na radhi za Mola wao Mlezi. Na mkisha toka Hija yenu
basi windeni. Wala kuwachukia watu kwa kuwa wali- kuzuilieni kufika Msikiti
mtakatifu kusikupelekeeni kuwafanyia uadui. Na saidianeni katika wema na
uchamngu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui. Na mcheni Mwenyezi Mungu.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.
|