259. Au kama yule aliye pita karibu na mji ulio
kwisha kuwa magofu tu, akasema: Ataufufuaje Mwenyezi Mungu mji huu baada
ya kufa kwake? Basi Mwenyezi Mungu alimfisha yeye muda wa miaka mia. Kisha
akamfufua. Akamuuliza: Je umekaa muda gani? Akajibu: Labda nimekaa siku
moja au sehemu ya siku. Akamwambia: Bali umekaa miaka mia wewe. Hebu angalia
chakula chako na vinywaji vyako, havikuharibika. Na muangalie punda wako.
Na ili tukufanye uwe ni Ishara kwa watu iangalie hii mifupa yake jinsi
tunavyo inyanyua kisha tunaivisha nyama. Basi yalipo mbainikia alinena:
Najua kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.
|