253. MITUME hao tumewatukuza baadhi yao juu ya
wengineo. Katika wao wapo ambao Mwenyezi Mungu alisema nao, na wengine
akawapandisha vyeo. Na tukampa Isa mwana wa Mariyam hoja zilizo wazi, na
tukamtia nguvu kwa Roho Takatifu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu alipenda wasingeli
pigana walio kuwa baada yao baada ya kuwajia hoja zilizo wazi. Lakini walikhitalifiana.
Basi wapo kati yao walio amini, na wengine kati yao walio kufuru. Na lau
kuwa Mwenyezi Mungu alipenda wasingeli pigana. Lakini Mwenyezi Mungu hutenda
atakavyo.
|