249. Basi Taluti alipo ondoka na majeshi alisema:
Mwenyezi Mungu atakujaribuni kwa mto. Atakaye kunywa humo si pamoja nami,
na asiye kunywa atakuwa pamoja nami: ila atakaye teka kiasi ya kitanga
cha mkono wake. Lakini walikunywa humo isipo kuwa wachache tu miongoni
mwao. Alipo vuka mto yeye na wale walio amini pamoja naye, walisema: Leo
hatumwezi Jaluti (Goliati) na majeshi yake. Wakasema wale wenye yakini
ya kukutana na Mwenyezi Mungu: Makundi mangapi madogo yameshinda makundi
makubwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu yu pamoja na wenye
kusubiri.
|