233. Na wazazi wanawake wawanyonyeshe watoto
wao miaka miwili kaamili kwa anaye taka kutimiza kunyonyesha. Na juu ya
baba yake chakula cha kina mama, na nguo zao kwa mujibu wa ada. Wala halazimishwi
mtu ila kwa kadiri ya uwezo wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mwanawe,
wala baba kwa ajili ya mwanawe. Na juu ya mrithi mfano wa hivyo. Na kama
wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa kwa kuridhiana na kushauriana, basi
si vibaya kwao. Na mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha
basi hapana ubaya kwenu mkitoa mlicho ahidi kwa mujibu wa ada. Na mcheni
Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayo yatenda.
|