217. Wanakuuliza juu ya kupigana vita katika
mwezi mtakatifu. Sema: Kupigana vita wakati huo ni dhambi kubwa. Lakini
kuzuilia watu wasende katika Njia ya Mwenyezi Mungu na kumkanusha Yeye,
na kuzuilia watu wasende kwenye Msikiti Mtakatifu na kuwatoa watu wake
humo, ni makubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na fitina ni mbaya zaidi
kuliko kuuwa. Wala hawatoacha kupigana nanyi mpaka wakutoeni katika Dini
yenu kama wakiweza. Na yeyote katika nyinyi akiacha Dini yake akafa naye
ni kafiri, basi hao ndio ambao a'mali zao zimeharibika duniani na Akhera.
Na hao ndio watu wa Motoni; humo watadumu.
|