|
102. Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani
kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani
ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi, na yaliyo teremshwa kwa
Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika Baabil. Wala hao hawakumfundisha
yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani; basi usikufuru. Wakajifunza
kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe. Wala hawawezi kumdhuru
mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo wadhuru wala hayawanufaishi.
Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa na fungu lolote katika
Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao laiti wangelijua.
|