61. Na mlipo sema: Ewe Musa! Hatuwezi kuvumilia
chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako Mlezi atutolee vile
vinavyo mea katika ardhi, kama mboga zake, na matango yake, na thom zake,
na adesi zake, na vitunguu vyake. Akasema: Mnabadili kilicho duni kwa kilicho
bora? Shukeni mjini, huko mtapata mlivyo viomba. Na wakapigwa na unyonge,na
umasikini, na wakastahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu
walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi Mungu, na wakiwauwa Manabii pasipo
haki. Hayo ni kwa walivyo asi na wakapindukia mipaka.
|